VYOTE NDANI GONGA94
MFALME KIPOFU 11
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Ilipoishia sehemu iliyopita........
Katika jumba la kifalme baada ya mfalme Tengu kugundua binti yake hayupo alipata mashaka na kujua, huenda atakuwa katika mikono isiyo salama, sababu haikuwa kawaida kuondoka bira kuaga aliagiza vijana wake wamtafute haraka na...
ENDELEA NAYO.......
Mfalme Tengu akiwa anahangika kumtafuta binti yake,
Upande wa pili nyumbani kwa Lindiwe story zilichukua nafasi baada ya Princess Nailet kukalibishwa na kumkuta Prince Yao ndani. ilikuwa ni furaha kwake kumuona na kuzidi kukagua uzuri wa mwanaume yule aliovutiwa nae,
Lindiwe aliligundua hilo baada ya kuona Princess anamuangalia sana Yao na pia hakuna chochote cha maana alichozungumza Princess tangu awasili pale.
"Princess, Mfalme atakuwa ana wasiwasi na wewe ni usiku sana??".
"Ata usijali kwakuwa nimepafahamu kila siku nitakuwa na kuja kuwaona na ata kesho pia nitakuja".
Princess Nailet aliamua kuondoka maeneo yale huku akiwa na furaha isiyokuwa ya kawaida,
"Princess unafuraha sana siku ya leo??"
"Ni lazima niwe na furaha kwa sababu leo ni siku yangu ya kuzaliwa, pia nimeona kitu nilichokuwa nikikitafuta kwa mda mrefu"
"Unataka kusema tayali umempenda yule kijana kipofu???"
"Hayo ni ya kwangu mimi".
Princess Nailet anafika nyumbani na kumkuta Mfalme akiwa na hasira sana juu ya yeye kuondoka bira ruhusa,
"Tabia gani hii umeanzisha ya kuondoka bira ruhusa???,mfalme alifoka kwa hasira"
"Baba leo ni siku yangu hupaswi kuwa na hasira juu yangu"
Princess Nailet alijua mfalme anampenda sana mana ndie mtoto pekee kwake.
******************
Ni siku nyingine mpya baada ya safari ya mda mrefu ya usiku kucha ya asikari wa ADELI waliotumwa na mfalme pamoja na Cheki kijana waliyempata,
wanakaribia kufika katika kasili la kifalme la ADELI na tarifa zinapelekwa kwa mfalme juu ya ujio wao.
"Tayali kijana ameshapatikana kama ulivyotoa wazo lako".
Mfalme Kojo alimfikishia tarifa zile Malikia Andwaa.
"Haitakiwi achukue mda kukaa hapa inatakiwa tuongeze nguvu ya kumtafuta kijana wetu lazima nimtafute mwanangu , Malikia andwaa aliongea kuonyesha bado anatamani kujua Prince Yao alipo".
"Akija muonyeshe upendo mbele za watu ili watu wasishituke kama sio mtoto wako,mfalme aliongea na kuondoka".
Tarifa zilisambaa za chini juu ya Prince kuonekana na kesho ndio ilikuwa siku ya utambulisho wake.
Mlinzi mkuu Nzegi alielekea gerezani kwenda kumpa tarifa zile General,
"Hii ni habari njema sana kwangu,acha leo wafurahi ila kesho wakisikia nimetoka furaha yote itapotea"
"Ni kweli General ngoja nikaweke mipango sawa"
"Nakuamini Nzegi kijana wangu".
Mpango uliendelea kuwa palepale wa General kutoroka siku ya utambulisho wa Prince katika ufalme huo wa ADELI.
**************
Katika ufalme wa YUNDI, wafanyakazi katika jumba hilo la kifalme walishangaa kuona Princess Nailet anaamka asubuhi na mapema na haikuwa kawaida yake.
"Usiku kwangu ulikuwa mrefu sana sura ya Yao hainitoki katika kichwa changu, ni lazima nimuone asubuhi hii",ni maneno aliyokuwa akizungumza na nafsi yake Princess Nailet
Aliondoka katika Jumba la kifalme bira kuwa na msaidizi yeyote na kuelekea katika makazi ya Prince Yao,
Lindiwe alishangaa kumuona Princess asubuhi na mapema nyumbani kwake tena bira walinzi akiwa peke yake.
Walisalimiana kama ilivyo mila na desturi
"Mama najua unashangaa kuniona asubuhi hii katika makazi yako ila nina shida na Yao na maongezi nae".
Lindiwe hakuwa na kipingamizi alimfata Prince Yao, Princess Nailet alimshika mkono Yao na kumsogeza pembeni kwa ajali ya maongezi zaidi.
Wakati yote yanaendele binti Yunde alishuhudia tukio lile la Princess kumshika mkono Yao nakujikuta wivu ukimuingia,
"Hapana haiwezekani tangu lini ana mazoea na Yao, kwanza asubuhi hii huyu anafanya nini na Yao?,au wamelala wote????,
Pasipo kufikili mara mbili roho ya wivu ikamuingia hakuta kuona mwanamke yoyote anakaa karibu na Yao zaidi yake yeye,
Aliondoka mbiombio mpaka katika jumba la kifalme......ITAENDELEA
Kijana cheki anafikishwa katika ufalme wa ADELI je? atafanyikiwa kutambulishwa??,na Vipi kuhusu Yunde anayeenda kutoa tarifa kwenye jumba la kifalme nini kitatokea? Tukutane hatua ya 12.
SHUKRANI – Emidee ft. Mbacho Wizzy (Official Lyrics Video) ? Produced by: Gift Record ? Released: 20
Wimbo wenye ubunifu imechanga kiarabu kiswahili na amapiano wimbo wa kushukuru kwa maisha na upendo Sasa sikiliza na ku download hapa gonga94.com
Sikiliza Wimbo Kamili
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mfalme-kipofu
MFALME KIPOFU Sehemi..ya............01 Anza nayo...... Ni katika ufalme wa ADELI,majira ya usiku katika jumba kubwa la kifalme
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............08 Ilipoishia sehemu iliyopita........ "Tarifa gani???" "Inasemekana baada ya siku tatu Prince
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............04 Ilipoishia sehemu iliyopita........ Farasi ilifika Lindiwe pamoja na prince Yao walipanda na safari ikaanza kutoka katika jengo
Story.....................MFALME KIPOFU Ilipoishia sehemu iliyopita.. General Tengeli anataman kuwa mfalme na ndio sababu ilimfanya atengeneza jeshi
Story MFALME KIPOFU Sehemi..ya............02 Ilipoishia sehemu iliyopita... "Mbona unazunguka mtabili emu niambie mwanangu niliyemzaa leo anatatizo gani???