VYOTE NDANI GONGA94
MR GENERAL : KUMBE ULINIPENDA EEE SEHEMU YA 14
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
“Una maanisha nini? Ikabidi na mimi niulize…
“Mimi ndio niliekuoa, akasema ..
Nikatoa macho, kisha nikamuuliza
“Kwani unaitwa nani…
“Naitwa Erick Resmund na nadhani ndio jina ulilolisikia wakati nakuoa, au ulisikia jina lingine tofauti?..
“Kumbe wewe ndio Erick , sasa kwanini haukunambia wakati wote huo mpaka nikajua umeniteka, nikazidi kuongea, akatabasamu kisha akanambia “Yaan akili yako ni ndogo sana, ndio nimekuteka ila haujawah hata mara moja kujiuliza kwanini ulivyofika nyumban kwangu ulikuwa kaparty kidogo, ujue kuwa nilikuwa nimejipanga ila si unajua mm ni muhuni, nilitaka kumchukua mke wangu kwa namna ya tofauti tu, akasema …
“Sasa Yule mzee ni nani? Ikabidi niulize…
“Embu tuache kuongelea watu, wewe nambia unanipenda kiasi gani, na ulianza kunipenda lini, nimekuwa nakuwaza sana, nikihisi nimeingia cha kike, kumbe ulikuwa na wewe unanielewa sana tu, ila hata ishara haukuwah kuonesha jamani, au ulitaka niote? Akaendelea kusema…
“Kuna siku ulikuja ulikuwa umependaza, kwa mara ya kwanza niijikuta kila nikikuangalia Napata msisimko, kwa kuwa nilikuwa nakuchukulia kama mkombozi na muokozi wangu, sikutaka hata kukukera, nikaingia zangu chumban, sasa kuanzia nafika chumban akili yangu iligoma kabisa kutulia, nikawa kama nikikufikiria napatwa na msisimko wa ajabu, nikajikuta naanza kujichukulia sheria mkononi, mpaka uliponikuta, nikawa sasa sikujui jina lako ndio maana nikawa naishia kusema mjeda mjeda, ila Yule mjeda alikuwa wewe…
Aisee aliangua kicheko, na kusema “Siamin kama na mimi ni bongolala kiasi KIle, ila nahisi niliendekeza wivu sana mpaka nikawa sifikirii, nilishaamin kuwa unipendi ndio maana nikawa nahisi kama unaweza kuniacha wakati wowote ule ndio maana nilikuwa kama nimechanganyikiwa, ila nilitakiwa nielewe maana ulikuwa unaonekana kabisa ulikuwa una hisia na mimi, maana hata shoo uliitoa kwa uhakika licha ya kuona nimesusiwa mzigo ila uliziweka mbele hisia zako kuliko uoga, sasa hapa nani alaumiwe…
“Wewe ndio ulaumiwe, ulishindwa nini kunambia kama unanipenda, nikasema..
“Weee kwanza wewe ulitakiwa uwe unaniwekea mitego wakati wote, uone kama nisingeingia, nilikuwa nashindwa hata kukuangalia, maana nilikuwa hata nikikuangalia nashindwa kujizuia, ndio maana nikawa naishi na wewe kama mpita njia, kwa kuwa nikijilegeza kidogo nina uhakika ningeshindwa kuvumilia na kutaka kamchezo…
“Na ukawa huna uhakika kama hako kamchezo na mimi nakapendaga, nikasema, nikashangaa mwamba amehema kisha akanambia “Naomba basi kidogo….
Weeee nilikurupuka na kuruka mpaka chini ya kitanda na kutaka kuondoka maana niliona ningeendelea kukaa vile, basi dakika sio nyingi, ufisi wa mume wangu ungeshindikana kabisa kujificha…
Akanirukia kisha akanishika kiuno, akawa ananiangalia kisha akanambia “Naomba kiss tu…
“Safari moja huwa ina kawaida ya kuanzisha safari nyingine, naomba nikalale, kwa leo inatosha, nikajitetea…
Ila hata hakubishana na mimi, akaanza kunikiss, sasa alikuwa ni good kisser kiasi kwamba nikashindwa hata kuendelea kukataa, tukajikuta tunakiss, aisee tulikiss kwa dakika kadhaa mwisho akanambia,
“Mamaa nenda kalale, sitaki kukuumiza tena, nikataka kwenda chumban kwangu ila akanizuia na kunambia
“Niamin sitakugusa mamaa, ila nataka joto lako, basi nikamsikiliza nikapanda zangu kitandani nikalala sina hata hili wala lile, na wakati wote huo alikuwa amenikumbatia, nimekuja kushtuka nataka kwenda uani, nikajua labda kaitwa kwenye kazi zake, maana namjua, unaweza ukashinda nae vizuri ila dakika chache unashangaa hayupo na anaweza kushangaa asirudi hata mwezi mzima…
ITAENDELEA …
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mr-general-kumbe-ulinipenda-eee-sehemu-ya