AAAAAAAH IMETOSHA BOSSππ N0 33ππ
Baada ya kumkuta hakim akiwa na boxa peke yake nilitoa machoπππ hee ana limutango yule jamaaa nilichokifanya nilijidondosha chini nikajidai nimezimiaπ€£π€£ nilimuomba mungu kimoyomoyo anisaidie niweze kubana pumzi kwa muda mrefuπΉπΉπΉ baada ya kudondoka hakim alikimbia kuja kuniokota pale chini alifika akanibeba akaniinua pale chini akanilaza kitandani alikuwa ananiita na kuniomba msamaha alinitikisa tikisa sana lakini sikuamkaπ€£π€£ nyie ila kubana pumzi ni kaziπππ nilikuwa nategeshea muda anaonitikisa tikisa ndo na mimi navuta pumzi chapuπππ alivyoona siamki alichukua simu akaanza kutafuta usafiri zile tax za online nahisi alikosa tax akaamua kuvaa nguo akafungua mlango akatoka vile ametoka tu mimi nilichukua nguo haraka nikavaa vitu vyangu vingine niliviacha kule chumbani sikukumbuka kubeba kitu zaidi ya kujiokoa tu kutoka mikononi mwa hakim! Nilifungua mlango taratibu nikatoka kule chumbani nilianza kushuka chini lakini nilihofia kukutana na hakim make alishuka chini kutafuta usafiri! Nikiwa nimeganda pale nawaza pa kuelekea nilimsikia hakim kwa mbali akiwa anaongea na cm ni kama vile anikuwa anaongea na dreva tax akawa anamwelekeza pale hotelini......
Niliwaza pa kwenda ni wapi nikiangalia vyumba vyote pale vimefungwa na ni usiku sana nilichokifanya nilirudi chumbani haraka nikapanga mito pale kitandani then nikaifunika blanket baada ya hapo nilijificha kule nyuma ya mlango ili hakim akija akifungua mlango akipiga jicho kitandani akiiona ile mito atajua ni mimi hivyo ataelekea kitandani mojo kwa moja na mimi nitapata muda wa kukimbia hakim alifika pale mlangoni akafungua mlango haraka akakimbilia pale kitandani vile ameingia mimi tayari nilikuwa nimeshauchomoa ufunguo niko nao mkononi nilitoka haraka nikamfungia hakim kule chumbani funguo nikakimbia nazo ili asijefunguliwa kabla cjafika mbali nilifanikiwa kutoka nje ya ile hotel.....
Nilikimbia umbali mrefu kutokea kule hotelini tulipokuwepo nilifika katika mtaa fulani hivi kulikuwepo na jengo moja la ghorofa ambalo lilikuwa halijaisha nilikaa pale usiku mzima baridi ilikuwa ni kali sana nilikaa hadi pakakucha sikuwa na pesa zozote zile nilichokifanya baada ya kupambazuka nilienda katika nyumba moja nikagonga getini alikuja kunifungulia kaka aliyejitambulisha kwa jina hemed alinikaribisha ndani kisha akaniuliza vipi una shida gani nikusaidie nini vipi tunafahamiana?! Nilimwambia mimi naitwa Recho ni mwenyeji wa jijini dar nilikuja huku kwa ajiri ya kutafuta kazi nakuomba kama hautojali uweze kunipatia kazi yoyote..... kazi gani unataka?! Yoyote tu kaka yangu....na mbona hauna mzigo wowote hata bag la nguo?! Niliibiwa vitu vyote etπ₯Ήπ₯ΉJana nilopofika zanzibar sikuwa na sehemu ya kufikia usiku ulipoingia nilijilaza nje katika jengo moja ambako nilivamiwa na vibaka wakanitoa kila kituπ₯Ήπ₯Ή nilidanganya hadi nikalia vyote nilifanya ili kujitilisha huruma kwa hemed ili anipatie msaada alinikaribisha ndani kwake nikaket sebleni yeye alikuwa yuko nje anaimwagilia maji bustani yake ya maua alimaliza kumwagilia akarudi ndani alinihoji vimaswali pale nikawa namdanganya lakini alinihurumia akaniruhusu nikae naye pale nyumbani kwake hemed alidai ya kwamba yeye zanzibar huwa anakujaga tu vocation akiwa yuko likizo kazi zake huwa anafanyia usa....tulifahamiana kijuujuu japo mimi kila kitu nilimdanganya sikumwambia ukweli juu ya kile kilichonikuta kwa kuwa bado ilikuwa ni asubuhi sana hemed alinionyesha chumba cha wageni akaniambia niende nikaoge kisha nipumzike.... nilimwambia asante niliingia kule chumba ni chumba kikubwa kizuri sana niliingia washing room nikaoga baada ya hapo nilingia kulala..... nililala hadi mida ya saa tano asubuhi nikagongewa mlango nikaamka kwenda kufungua alikuwa ni hemed aliniuliza vipi unajisikiaje bado una usingizi?! Hapana kaka niko sawa usingizi umeisha..... niite hemed karibu tunywe chai utalala badae tena.... niliongozana naye kwenda mezani tuliletewa chai tukanywa aliyeleta chai ni mkaka hivi nazani ni house boy kule ndani baada ya chai hemed aliniomba nimwandikie mahitaji ya vitu ninavyovihitaji ili akitoka mjini anichukulie au kama vipi tunaweza kutoka wote alinimbia.... hapana hemed kwa leo siwezi kutoka lbda siku nyingine.... nilimwandikia kila kitu nikampatia kile kikaratasi akaondoka nilitoa vyombo mezani nikapeleka jikoni nikajipa majuku ya kuviosha kwa muda huo Idris alikuwa kaenda kumfungulia hemed geit! Hehehe jamani weye ni mgeni et ungeviacha tu mimi ningeosha... aliniambia idris baada ya kunikuta nikiwa naosha vile vyombo.... ucjali idris hata mimi naweza wacha nikusaidie......
Nilimaliza kuosha vyombo huku nikiwa napiga story mbili tatu na idris kule jikoni nilimuomba anisaidie dawa za maumivu make mwili wote ulikuwa unauma..... aliniletea dawa nikanywa baada ya hapo nilienda sitting room kuangalia movie.... ile nyumba ni jumba kubwa sana la kifahari na kule ndani alikuwa anakaa idris tu make hemed huwa anakuja likizo tu na kuondoka likizo ikishaisha..... tuliendelea kuwatch movie huku tukiwa tunapiga story na idris ni mcheshi sana alinipigisha story mbalimbali akanisimulia kuhusu boss wake hemed jinsi alivyo mtu mwema namna alivyomsaidia vitu vingi kimaisha mida ya saa nane tulipika zetu wali wa nazi na maharage mboga za majani na samaki tukala tukarudi zetu kwenye movie jioni mida ya saa 12 boss hemed alirudi nyumbani idris alikuwa yuko bafuni ilibidi mimi ndo niende kumfungulia geit..... nilifungua geit akaingia alinijulia hali baada ya hapo alipeleka gari parking akatelemka alifungua but na kuanza kushusha mizigo nilikwenda mpokea alinipatia vitu alivyonunua kwa ajiri yangu vingine aliniambia niachane navyo idris atakuja kupeleka ndani..... hemed ni mkaka fulani hivi siyo mkubwa kwa haraka haraka ana miaka kama 28 au 30...ni shombeshombe yupo kama mwarabu hivi ni mpole siyo mtu wa mambo mengi nilipokea vile vitu nikaanza kuondoka kuelekea ndani kabla cjapiga hatua nyingi hemed aliniita.....
""Recho""
""Abee niliitika then nikarudi kumsikiliza...""
""Be free ukiwa na shida yoyote usisite kuniambia nitakutafutia kazi huku zanzibar ikikosekana nitakuangalizia hata huko marekani kwani umesomea nini?! Nilimwambia kitengo nilichosomea akanipromise kunitafutia kazi!....""
Nilienda ndani nikafungua vile vitu alivyoniletea hemedππ hadi chupiπ€£π€£ alf kama vile alinipima jomonππ chupi zilinifit ile mbaya.... alininunulia product za ngozi nguo viatu pamoja na cm.... nilivipanga vile vitu kabatini baada ya hapo nilienda kutoa asante kwa hemed aliniambia ni sawa recho be free kwangu niambie chochote..... nilimuiza kama atakula chochote aliniomba juice nilienda nikamchukulia juice nikamletea then mimi nilirudi chumbani kwangu..... ilifika mida ya saa moja moja hemed akaingia jimu ila lizuriππ ana jimu ndogo pale nyumbani kwake alipiga mazoezi mie nikawa namchabo dirishaniπΉπΉ
Uuuwww ni gentlemen na nusuπΉπΉ hemed alimaliza kufanya mazoezi nikakimbilia zangu jikoni niliingia jikoni nikapasha pasha msosi hemed alipotoka kwenye mazoezi alielekea bafuni alipotoka bafuni alikuja jikoni kwa muda huo idris alikuwa katoka...
""Wow vinanukia sana..... alinimbia hemed""
""Nilismile then nikamwambia kidogo tu et siyo sanaππ""
""Hahahaa haya bn unapika nini?!""
""Nilipika mchana wali samaki, maharage na mboga za majaniππ""
'""Wow π«°kitakuwa kitamu sana ehπ«°""
""Hahahaaa cha kawaida et""
""Hii hapa line utaweka kwenye simu yako....""
""Thank youππ""
"" ni sawa usiwe na shaka kuna chochote kingine unahitaji?! Usiogope niambie tu....""
""Hakuna kitu hemed basi nikihitaji chochote nitakwambia...""
""Sawa recho basi mie niko zangu sitting hapo nataka nicheki game mara moja kama hautojali unaweza kuja tukaangalie wote... sawa basi wacha nimalizie kupakua chakula kwenye hotpot then nitakujoin..... we shabiki wa team gan rechoi?! Hahahaa mimi ni simba etππ wow kesho nitakununulia jez umenifurahisha sana kuwa mwanasimba hemed aliniambia hivyo then akanigeiππ baada ya hapo alitoka kwenda sebleni kuangalia mpira mimi nikabakia jikoni napakua chakula.... basi nilijikuta nasmile etππ nikasahau na kipigo cha jana usiku kutoka kwa hakim! Nilimaliza kupakua chakula nikapeleka dinning hemed aliniomba tu nipakue chakula chetu mimi na yeye nipeleke pale sebleni tule huku tukiwa tunaendelea kuangalia mpira idris alikwenda kucheki mpira bandani yeye alidai nyumbani hakuna vibe tulikula mimi na hemed taratibu huku tukiwa tunaendelea kuangalia mpira..... mazungumzo ya hapa na pale yaliendelea kati yangu mimi na hemed line alinipatia ya kwake nilikuta kaniungia bando la mwezi na namba yake kanisevia tayariππ
Usiku nilimuaga nikaelekea chumbani kwangu kwenda kulala amani ya moyo ilirudi niliona ni kama tayari nimeshapata sehemu ya kujificha ili hakim asinipate..... niliendelea kukaa pale nyumbani kwa hemed walikuwa wakarimu sana kwangu kila asubuhi hemed alikuwa akiwahi kuamka na kwenda kuimwagilizia maji bustani yake ya maua kila aliponikuta nafanya kazi yoyote alinisaidia.....siku moja aliniuliza kama ninaweza pata vyeti vyangu vya form four pamoja na vya chuoni ili anitumie maombi ya kazi tuone kama nitafanikiwa kupata kazi zanzibar au usa..... alikuwa kabakiwa na siku chache tu za kukaa visiwani zanzibar...... nilimwambia vyeti vipo nitafanya mpango nikavifuate huko dar! Niliwaza nitafanyaje ili niweze kuvipata vyeti vyangu bila kuonana na wazazi wangu kwa kile walichonifanyia sikutamani hata kuwatia machoni kwangu niliwaogopa sana niliwaona kama maadui zangu wa kwanza katika dunia hii.... nilikaa pale nyumbani kwa hemed kwa takribani mwezi mzima.... siku moja usiku nikiwa chumbani kwangu najiandaa kulala nilipanga safari ya kurudi jijini dar kesho asubuhi na mapema kwa ajiri ya kwenda kuvichukua vyeti vyangu kule nyumbani kwetu nilipanga pia kwenda kuchungulia kule nyumbani kwa paschal kama yupo au laa! Nilikuwa na wasiwasi sana juu ya hiyo safari yangu lakini sikuwa na budi ilikuwa ni lazima niende....
Itaendeleaaaaaaa
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi