AAAAAAAH IMETOSHA BOSSππ N0 35ππ
Nilifika kule nyumbani kwetu nilikuta nyumba yetu imewekewa matangazo ya kuuzwa palionekana kama sehemu ambayo hakai mtu yeyote..... nilijiuliza wazazi wangu watakuwa wapi kipi kiliwakuta au hakim aliwaumiza wazazi wangu?! Sikuwa na cha kufanya zaidi nilirudi kule lodge nililala kesho yake mapema niliamkia makaburini kule alikozikwa mama yake na paschal nilipeleka maua kule katika kaburi lake nilienda nikakaa juu ya lile kaburi na kuanza kulia huku nikiwa namuomba mama paschal msamaha kwa sababu yale yote aliyoniomba kuyatimiza hakuna hata limoja nililolifanikisha...... nilijiinamia kwenye lile kaburi kama mtu aliyekata tamaa...... nikiwa bado naendelea kulia juu ya lile kaburi ghafla niliguswa bega nilipogeuka nilikutana uso kwa uso na baba yake na paschal nilimkumbatia aliyafuta machozi yangu..... aliniuliza kuhusiana na hali yangu nilimwambia niko sawa.... baba paschal alikuja pale makaburini kufanya usafi kwenye kaburi la aliyekuwa mke wake nilimsaidia kufanya usafi baada ya hapo tulirudishia maua pale kaburini tulisali na baada ya hapo nilimuaga yule mzee nilianza kuondoka pale makaburini lakini baba paschal aliniita akaniuliza vipi umeshapata sehemu nyingine ya kufanyia kazi?! Mmmhh niliwaza why kaniuliza vile nilinyamaza kwanza aniambia kama bado haujapata unaonaje tukaongozana sote kwenda marekani uende ukaendelee na kazi yako kama kawaida.... kwani baba mmesha ihamisha campuni tyr? Samahani mimi nilipata dharula kidogo nikawa nimeacha kazi kule katika campuni ya boss paschal.... sijasikia chochote mwanangu ni kipi kilichotokea kwani au uligombana na mwenzako?! Hapana baba nilipata dharula nyingine lakini mimi na paschal tuko sawa hatuna tofauti yoyote...... lakini unaonekana kama mtu unayejificha ni kama vile hutaki kuonana na watu je kuna kitu unachonificha pendo!?.....hapana baba niko sawa! Sisi tutaondoka hapa Tanzania kesho kutwa tunahamia rasmi nchini marekani lakini kama ukihitaji chochote usisite kuniambia na kama ukihitaji kurudi kazini usiache kunitaarifu hata kama kuna tofauti yoyote kati yako wewe na paschal niambie mimi nitaitatua ....... aliniambia baba yake paschal baada ya hapo alielekea kwenye gari lake alifungua mlango akachukua pesa akaja akanikabidhi pamoja na namba yake ya simu alinipatia pesa nyingi sana nilimshukuru baada ya hapo niondoka nikamuacha pale......
Nilirudi kule lodge nilikuwa nawaza tu jinsi nitakavyoijua sehemu waliko wazazi wangu ili niende nikachukue vitu vyangu nilipata wazo la kwenda kijiweni kwa yule dreva tax wangu ambaye ni jimmy nilikwenda kumtafuta ili nimuulize kama anaweza akajua sehemu waliko wazazi wangu nilibahatika kumpata jimmy aliniambia kuwa wazazi wangu wako kwa mjomba wangu na yule hakim baada ya kunikosa mimi ilibidi wazitaifishe mali zote za wazazi wangu ili kufidia deni walilokuwa wanadaiwa...... baada ya kuzipata zile taarifa kutoka kwa jimmy nilienda zangu kupumzika then jioni nilifunga safari kuelekea kule nyumbani kwa mjomba wangu ilikuwa ni siku ya ijumaa nakumbuka nilifika katika eneo jirani na kule nyumbani kwa mjomba nikawa nimekaa hapo ndani ya kama dkk 30 niliwaona wazazi wangu wakitelemka kwenye bajaji ni kama vile walikuwa wametokea kazini maskini hata gari hawanatenaπ₯π₯....... waligonga getini wakafunguliwa wakawa wameingia kule ndani kwa mjomba nilipata uhakika kweli ya kwamba wanakaa pale nilipanga kurudi kesho yake kwa sababu siku ya jmosi wote watakuwa wameenda kanisani namimi nitapata urahisi wa kuvichukua vitu vyangu...... niliondoka sehemu ile nikarudi kule lodge nililala then kesho yake mapema mida ya saa tatu nilianza safari kuelekea kule nyumbani kwa mjomba wangu niligonga getini akaja kunifungulia amina ambaye ni binti wa kazi kule nyumbani kwa mjomba! Tulisalimiana kawaida kabla hajanifahamu kwa sababu nilikuwa nimeificha sura yangu nilimuuliza kama kuna watu alinimbia tayari wameshaondoka kuelekea kanisani..... baada ya kuniambia kuwa kule ndani hakunapo mtu nilijifunua sura yangu amina akaniona aliniita da pendoπ₯Ήπ₯Ή kumbe upo hai bora hata umerudi kila mtu hapa nyumbani alikuwa na wasiwasi sana juu yako karibu ndani......
Amina alinikaribisha ndani niliingia kule ndani amina aliniambia nibakie nyumbani yeye aende akawaite wale walio kwenda kanisani awapatie taarifa njema za kurudi kwangu niliwaza haraka haraka cha kumwambia yule binti ili kimuweke busy kwanza nifanye kile kilichonipeleka kule ndani nilifikilia haraka haraka nilimuuliza kuna juice gani huku ndani tayari alikuwa ameshanipatia chai nipo nakunywa ila kwa sababu sikutaka yeye atoke kwenda kuwaita wazazi wangu nilihitaji kumsumbua tu ili aendelee kubakia kule ndani nilimuomba simu yake nikajidai kuna mtu nampigia nilikuwa najidai kupiga lakini wala sikumpigia yeyote nilianza kulalamika kuwa simu ya amina haina networkπ£π£ yote ilikuwa ni kumzubaisha tu niendelee kubakia na simu yake asijewapigia wazazi wangu kuwajulisha kuwa niko pale nyumbani...... kuna juice gani? Nilimuuliza amina aliniambia kuna juice ya embe na parachichi..... nilimuomba aende akamenye machungwa ya kutosha anisagie juice ya chungwa peke yake nilihitaji kitu kichachu zaidi...... ukishamaliza utaniacha nikiwa nakunywa juice yangu wewe utakwenda kumuita daddy and mom....... amina alikubali alielekea jikoni na mimi nikamwbia kuwa naelekea chumbani kupumzika....
Muda ambao amina alikuwa yuko busy kumenya matunda kule jikoni mimi nilikuwa busy kuvipakia vitu vyangu ili niondoke navyo kutoka kule nyumbani kwa mjomba wangu...... nilipakia kila kitu baada ya hapo nilimpigia jimmy nikamuomba asogee maeneo jirani na kule kwa mjomba ili aweze kunichukua mimi na vitu vyangu baada ya hapo nilielekea jikoni kwenda kumuangalia amina kama tayari ameshamaliza au laah..... nilimkuta yupo anaichuja juice alimaliza kuichuja akanimiminia kwa glass akanipatia nikaanza kunywa..... jimmy alinitext akaniambia tayari yuko nje .... nilimuomba sasa amina akwende akawaite wale waliokwenda church lengo langu nilitaka tu anipishe ili niweze kuondoka..... amina aliniaga akatoka baada tu ya yeye kuondoka mimi nilitoa mabag yangu nje nikapakiza kwenye tax ya jimmy baada ya hapo nilirudishia milango ya kule kwa uncle nikawa nmeondoka .........
Nilirudi hadi lodge huku kamoyo kangu kakiwa kananienda mbio sanaππ niliwaza kuondoka siku ileile kurudi zanzibar nilipumzika kidogo baada ya hapo nilianza safari yangu kutokea dar es salaam kuelekea zanzibar baada ya kufika zanzibar nilimkabidhi Hemed vyeti vyangu vyenye majina yangu halisi nilimuomba radhi kwa kumdanganya jina langu kipindi chanyuma nilipokwenda kuomba msaada kwake...... nilimwelezea mkasa mzima ulionipata mimi hadi nikajikuta nikiwa katika njia panda alinipa pole na aliniahidi kunisaidia......usiku ule alinifanyia mchakato wa kunitumia barua za maombi ya kazi katika sehemu tatu mbili usa moja zanzibar! Zilipita siku 14 bila majibu yoyote kutoka katika sehemu zote nilizoomba kazi ilibidi hemed aondoke zake kurudi kazini lakini aliniahidi ya kwamba hatochoka kunitafutia kazi endapo kama itapatikana basi nitakwenda nikaishi naye huko usa.....nilikaa zanzibar kwa takribani kama miezi miwili hiviii baada ya hapo hemed alinipatia taarifa njema juu ya mimi kupata kazi huko nchini marekani na nilitakiwa kureport haraka iwezekanavyo......
Ilikuwa ni jioni moja hivi niliondoka zanzibar kwenda kulala jijini dar kwa ajiri ya kupandia huko ndege nililala kesho yake asubuhi nilielekea airpot kwa ajir ya kuianza safari yangu kuelekea nchini marekani..... nilipanda kwenye ndege nikatulia zangu kwenye siti yangu sikuwa na kazi yoyote nyingine zaidi ya kujisnap na kuangaza macho yangu huku na kule.....zikiwa zimebakia dkk 18 za ndege kuanza kupaa nilimuona boss paschal akiwa anapanda ndani ya ile ndege niliyokuwa nimeipanda mimiπππ nilitoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlangoπΉπΉ bahati nzuri kwenye mkoba nilikuwa na mjitandio niliuchukua haraka nikajifunika kichwani na baadhi ya sehemu za usoni..... paschal alikuja akakaa kwenye siti ya mbele yanguπππ hakuniona na wala hakunigundua......
Itaendeleaaaaa......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi