BILLIONEA ALIYENITEKA ILI NIWE WAKE 1 to 5
SEHEMU YA 1
ANZA NAYO.....
Dah nimeamini ule msemo ambao moyo hupenda wenyewe bila kuangalia sura au muonekano wa mtu vile vile moyo hupenda kutokana na mazingira tofauti ambayo tunakutana nayo sisi wanadamu
Mnajua moyo ni wa ajabu sana tena sana, katika njia zangu zote sijawahi kukutana na mwanaume nikampenda ila kuna siku bwana hii siku sitaisahau kabisa kwenye maisha yangu
Imagine mtu umeenda msibani ila baada ya kufika huko huwazii kabisa wafiwa we unawaza mwanaume ambae umekutana nae hapo.
Sijui mnanielewa au, niite Shamim, Shamim kama Shamimπ mimi bwana kabila langu ni mgogo nina sifa zote za ugogo ikiwemo kuongea sana basi mimi ni miongoni mwao.
Nataka niwape story yangu ilivyokuwa ni kweli bwana siwezi kuongea vitu vya uongo, basi mimi Shamim ndio dada mkubwa wa familia, na ndie mtoto wa kwanza kuzaliwa wa mama Bella
Simjui baba ila nasikia ni shekhe maarufu sana ila simjui na sijawahi kumuona maana mimi na dini haviingiliani kabisa, hapa nilipo sijui kuswali au kusali maana mama yangu ni mkristo baada ya kunizaa mimi aliachana na baba yangu na akaolewa na mwanaume mwingine
Ambaye ndie alienae mpaka sasa na wamezaa watoto wawili wote wakiwa wakike, kuwa na watoto wa kike hasara tupu ila kuna muda wana faida tena kubwa π₯°
Sisi bwana tunaishi huku Moro yani nafahamika kalibia mtaaa mzima kwa kuitwa Shamii, mama Bella bwana yeye kazi yake ni kuuza miguu ya kuku harafu sie mabinti zake kila siku ni kununua nguo
Hatuna kazi yoyote zaidi tumekuwa tukiongwa pesa na wanaume harafu tunapita kushoto, mwanaume atatutafuta kalibia siku nzima tunampiga block kubwaa na maisha yanaendeleaππ
Sasa bwana sisi hatupokei pesa ndogo yani kuanzia kwenye 30 keshi na kuendelea kama huna hupati no,π eeh maneno mengi ya nini bwana ikiwa mmeshanifahamu
Umri wangu mimi ni miaka 25 na ninakaa nyumbani sina kazi yoyote hata kusema nitafute kazi siwezi yani nikubweteka matako masaa 24 na kudoea miguu ya mama Bella hapo basi ndio nasikia raha
Basi bwana hako ni kautambulisho kangu kafupi ikiwa nimewapa mengine ambayo hayatakiwi kabisa, tuanze na story yetu ambayo kwa namna moja au nyingine inaweza kukufanya uenjoy.
SONGA NAYO SASA......
Ni majira ya usku familia nzima tulikuwa tumekusanyika mezani tukipata chakula cha usiku, ooh my God nimekosea yani tumekusanyika kwenye mkeka π maisha ya kununua meza sie hatuna hizo hela kabisa.
Basi tulikuwa kimya kama sio sisi ambao mchana kutwa tunapiga makelele nyumba za jirani, chakula kilikuwa kitamu mpaka nikasahau jina langu kwa muda π₯° chezea mama Bella wewe anajua kupika huyu mama na nyumbani sitoki ng'o.π
"Kilioooooo kilioooo.."
Chakula kikiwa kimenoga bwana tukasikia filimbi harafu ikafuatia kilio, kwanza nikastop kula maana kwa umbea huu mimi ni namba moja.
Nikakaa kusikiliza kwa makini..
"Kilioo kwa mama Maggie, wakazi wote mnaombwa kwa moyo mmoja kesho mkusanyike tukampe buriani za pole kwa ndugu na familia ya mzee juma kwa kumpoteza mama yake.."
Huyo mtangazaji alikuwa anaongea kwa mbwebwe kama kuna sherehe vile, sijui kwa vile aliyekufa ni mzee sana, nikasonya kwanza maana aalinikera namna alivyokuwa anatangaza.
"Endelea kusonya tu, huku ugali unaisha.."
Bella aliniambia ndio nikakumbuka kama nakula ile nageuka nakuta kiugali kimebaki kidogo na sijashiba,π« nikachukia nikanyanyua matako yangu huyo mpaka nje
Kipindi hiki bwana kilikuwa ni kipindi cha joto mwezi wa sita wewe kulikuwa na joto balaa kukaa ndani huwezi na usiku ukifika tunawaza namna ya kulala wengine hulala kwenye vibalaza kwa sababu ya joto.
Basi nikatoka zangu nje hata kunawa sikunawa kabisa, ile natoka nje nikakutana na kundi la wamama wamekaa wanaongea awee kwenye umbea na mimi nimo basi nikasogea maana sie tunaishi nyumba za kupanga tena zile za uswahilini kabisa
Kwahiyo watu kama hawa hawakosi kabisa, unakuta mtu ameacha mboga jikoni anatoka nje kupiga umbea akija kurudi ndani mboga yote imekuwa nyeusi, pua anazo ila kusikia akhaaa baadae ndio anaanza kujilaumu eti kwanini sijasikia π
"Kuna nini kwani..??"
Baada ya kutoka nje nikauliza huku nikitafuta kitofali nikakalia.
"Hivi Shamii wewe ulikuwa wapi wakati wanatangaza..??"
Aliuliza mdada mmoja ambaye ndio kwanza ana mwezi mmoja toka aolewe na hajui kama natembea na mume wake. π
"Unazani sijasikia, nimesikia vizuri sana ila hapo panapo ongeleawa ndio sipafahamu kabisa.."
"Ni mtaa wa pili huko.."
Mwanamke mwingine akadakia.
"Kama mtaa wa pili me siendi Bola nimsaidie mama Bella kukaanga miguu ya kuku ila huko me siendi.."
Niliongea huku nikinyanyuka na kuingia ndani huku nikiwaacha wananisema, eti mdada anajishauwa huyu, me hata sikujali kikubwa Mungu kanipa vyote basi ya nini kupigizana kelele na watu wasiokuwa na shape wala makalio ππ.
Basi bwana hii siku ilipita kwa shida kutokana na joto la Moro, asubuhi mida ya saa tatu mtoto wa kike ndio nikaamka namkuta mama Bella kashafanya usafi mpaka vyombo kaosha yani mama anajituma huyu
Kuna muda namuonea huruma kabisa maana wamama wenzake huwa wanamsema sana eti anatulea vibaya lakini pamoja na kusemwa wala hajawahi kutuambia kitu sijui kupika au kufanya nini kazi zote hufanya yeye
Na sio kama anapenda la hasha mama yangu ni mtu wa kitofauti kabisa akiongea kitu kwa mdomo mmoja harudii tena kama utamuelewa sawa usipomuelewa unaendelea na maisha yako ila siku yakikutokea usimwambie chochote
Yani ukimwambia basi hasira zake zoote alizonazo kwa muda mrefu anazimalizia kwako....
ITAENDELEA
SEHEMU YA 2
SONGA NAYO.....
Basi baada ya kuamka mtoto wa kike nikamsogelea mama ambae muda huo alikuwa anachambua mchele.
"Mama shkamoo ..."
Nilimsalimu.
"Marhaba, haya umeamka jiandae uende msibani kwa ajiri yangu maana kama unavyoona hapa miguu inauma pia imevimba sana.."
"Lakini mama..."
"Shamim unataka kunipanda kichwani si ndio, baada ya baba yako kunipa mimba akanitelekeza nikakulea kwa shida leo nakuagiza unakataa nakuuliza we mbilikimo ??"
Eeh asubuhi asubuhi mama akaanza kunichamba, na sio kawaida yake kabisa basi nikajishusha.
"Basi mama nisamehe nitaenda.."
Nilisema huku nikinyanyuka kwenye mkeka
"Kazi kujazia nyuma tu, kufanya kazi aaah na sijui mume kama utapata kweli maana kwa tabia zenu nyie watoto mmenichosha.."
Mama akaendelea kugomba.
"Ndio malezi hayo, sasa unakula ulichopanda.."
Yule mdada ambae natoka na mume wake akaongea basi wakacheka, mimi moyoni nina hasira nawaza siku akijua natoka na mume wake sijui atafanyaje maana anamdomo sana huyu..
Nikaingia ndani na kutafuta kijora kisha nikavaa sikukumbuka hata kuoga sababu ya mama kunigombeza nilichofanya mimi ni kuswaki na kunawa miguu kisha huyo nikaondoka zangu.
Hata sipajui ninapoelekea maana msiba upo mtaa wa pili kweli nikabaki nyuma ya nyumba yetu nazunguka tu ili mradi mda uende.
"We bado upo hapa..??"
Nikiwa nazunguka yule mdada akaja na kunikuta bado nikiwa pale, huyu dada simpendi maana kwanza anajikuta sana kisa mumewe ana kazi nzuri na wanakula vizuri nakwambia kila siku wali, kuku, siku nyingine pilau nikikumbuka mumewe ananihonga elf tano ndio nashikwa hasira π
"Hayakuhusu.."
Nilimwambia kisha nikageukia upande wa pili yule dada akaondoka na muda huo Bella na Maria wakaja hawa ni wadogo zangu
"Hee we Shamii bado upo hapa..??"
Bella aliniuliza.
"We acha tu, huo msiba wenyewe sifahamu ulipo kabisa sa naendaje.."
"Mh, pole mwaya hebu twende tunaweza kuulizia huko mbele kwa mbele.."
Basi mtu tatu tukaondoka pale, kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa kunipa hawa π₯° maana wamekuwa zaidi ya ndugu wananipenda na kuniheshimu kama dada yao.
Pili hawa watu ni watu muhimu sana kwenye maisha yangu maana kwenye maumivu na furaha tupo pamoja.
Cha mwisho kabisa ni kwamba Mungu katuumba bila upendeleo wote tuna nyashiπshape ndio kabisa pia na ule weupe tunao so hakuna cha kuoneana wivu hapo upo π
Basi tuliongozana tukiwa tumevaa vijora haoo mpaka mtaa wa pili sema msiba huwa haupotei maana chapu tukawa tumefika msibani tulikuta watu wengi balaa
Watu wengi hasa hawa wenye magari ndio kabisa magari yalijazana mpaka sehemu ya kukaa ikakosekana, tukabaki tunajibana bana kama mbuzi zizini
"Dah hii kali aisee..."
Nilisema baada ya mimi kubanwa sana wakati tukiwa kwenye foleni kwenda kuaga marehemu, ndugu zangu sio kama nililazimishwa kwenda hapana bali niliona kule ambapo walisimama ndugu zake kulikuwa na wakaka wazuri wako kama sita hivi tena walikuwa wamependeza na zile suit zao nyeusi awee
Basi me nilikuwa naona hatufiki, mwendo wa taratibu hii ni kwa sababu watu walikuwa wengi sasa katika kujibalance vizuri ili nipate nafasi si nikashika kitu kigumu π
Ngoja kwanza nikageuka kuona aliye nyuma yangu nililaani vibaya baada ya kuona jibaba li mtu lizima likiwa na kitambi ndio lilikiwa linanigusa gusa na tumbo lake π«
Hakuishia hapo akawa anajisogeza sogeza kwenye makalio yangu ili mradi tuu ayaguse alinikera sana nikageuka kwa hasira
"We baba vipi.."
Niliongea kwa ukali nikasahau kabisa kama nipo msibani harafu palikuwa pametulia hivyo sauti yangu ilisikika vyema..
"Binti taratibu sawa tupo msibani hapa.."
Lile baba lilininong'oneza sikioni hapo nikatulia maana watu wengi macho waliyageuzia kwangu, basi binti wa shekhe ikabidi nitulie lakini ndio hivyo lile baba halikuacha kunibambia kwa nyuma π«
Hatimae tulifika badala ya kuangalia mwili wa marehemu nikaangalia wakaka wazuri waliokuwa mbele ya jeneza, baada ya kuona hao vijana wanahuzuni sana na mimi nikaongeza huzuni
Sikuishia hapo nikaanza kulia kwa nguvu, huku nikiita bibi, ila mimi huenda Mungu aliniona kabisa lile baba lililokuwa nyuma yangu likanishika huku likiniambia, pole binti jikaze basi tupite hapa..
Moyoni nikajisemea we mzee hunijui nikajiangusha chini na michozi hiyo yani nalia kama aliekufa ndugu yangu, basi kuna watu maalumu wakaja kunibeba mkuku mkuku mpaka ndani.
Mda huo nalia tu yani hakuna kitu kigumu kama kuigiza π maana wakati me naigiza mara wakaja na mkaka mwingine nae alikuwa analia jamaa hajiwezi yani mpaka huruma
Badala ya kuendelea kulia nikabaki namtazama yeye, π mkaka alikuwa analia ki gentlemen yani uwiii kuna sie hapa tunalia midomo ewaaa ππ
Wakati yule kaka analia me ndio nikapata wasaa wa kumchunguza vizuri, dah kuna watu wazuri harafu kuna sisi hapa ambapo kila kukicha tunajisifia wazuri badala ya kusifiwa
Yani mkaka alikuwa mzuri alafu mweupe sio sana maji ya kunde, ndevu zake zilikuwa ndefu kidogo lakini zilikuwa zimenyolewa kwa mpangilio mzuri yani ni mkaka lakini kuna baadhi ya ndevu ni mvi πππ
Nikabaki namshangaa huyu kaka, sasa katika kushangaa sana si nikajisahau bwana nikabaki uso mkavu ila machozi ya huruma ndio yanatoka..
"Binti.."
Nikiwa ndio kwanza naendelea kujiliza nilisika kuitwa, alikuwa ni kijana flan hivi nazani alikuwa hapo kwa ajiri ya kuangalia watu wale ambao wana pepo za kulia ππ, yule kaka aliniita zaidi ya mara mbili sikugeuka hata nalia chini chini
Basi akaja na kunishika kisha akaninyanyua huku ananisaidia kuingia nyumba kubwa kabisa maana hapo kulikuwa na nyumba kama nne hivi, nyumba tatu ujenzi wake ulikuwa wa kawaida sana ila ile moja ilikuwa kubwa yani inavutia na ilijengwa kisasa.
Basi akaniingiza mpaka humo ndani, me naendelea na maigizo yangu ungekuwa unaniona ungejua kabisa huyo aliekufa alikuwa ni rafiki yangu wa karibu lakini pia ndugu yangu wa damu.
Baada ya kuingizwa humo ndani aisee nilikuta watu kama kumi hivi wakiwa wamevalia vizuri lakini pia walionekana watu wazito miongoni mwao alikuwemo yule kaka aliekuwa kule nyumba ndogo
Nikabaki sielewi kafikaje fikaje humo, mie mgeni humu ndani na hata sehemu ya kukaa haikuwepo kabisa nikabaki natetemeka mpaka yule kijana aliekuwa kanisaidia kunishika akihisi natetemeka maana nilikuwa natetemeka mpaka kaka wa watu na yeye anatetemeka ππ
ITAENDELEA
SEHEMU YA 3
SONGA NAYO.......
Niliendelea kutetemeka lakini hata hao watu waliokuwa humo ndani hawakuwa na muda na mimi wengi walikuwa na huzuni, yule kijana ikabidi anafatie kiti kisha akaniletea nikaa
Nilikuwa nimekaa kwa tahadhari kubwa, basi muda ulikimbia bado tumo ndani mpaka inafika saa nane ndio nikaanza kuona watu wanaingia na kutoka ikabidi na mimi niinuke lakini ndio kwa kuogopa hivyo
Wakati najishauri kuinuka ka simu kangu ka batani kakalia ukizingatia nipo msibani kelele hamna pako kimya harafu watu wote waliokuwa humo nawaona wana smartphone ndio kabisa nashindwa kupokea sim
"Dada simu yako inaita.."
Nikiwa nimekaa kizembe zembe kuna katoto kana umri kama miaka 16 hivi kalinisemesha basi nikaingiza mkono kwenye nyonyo π nyie nilikuwa nazalilika yani nilikuwa naomba baada ya kutoka hapa sitafanya maigizo tena kwenye misiba ya watu.
Basi nikaitoa hivyo hivyo nikiwa mkavu na sura ya huruma nikaangalia kwanza mpigaji alikuwa Bella nikapokea.
"Hello.."
Niliongea sauti ya puani aisee hata hawa watu waliokuwa humu nazani walijiuliza huyu binti ako na matatizo ya akili.
"Shamiii uko wapi maana tumekutafuta sana na tumesikia umeanguka eti ni kweli..??"
Aliniuliza Bella basi ikabidi ninyanyuke niende nje kabisa huku moyoni nikihaidi sirudi tena humu.
"We dada hebu taratibu basi, me nipo nyumba kubwa humu.."
Niliongea
"Usinitanie nyumba kubwa umefikaje..??"
Bella aliuliza kama haamini.
"Kwa kupaa.."
Nilijibu huku nikiendelea kutembea, sasa bahati mbaya nikagongana na mtu na kusababisha aangushe simu yake lakini pia na yangu..
"Dah, leo nimekuwa kama namikosi yani.."
Niliongea bila kumtazama huyo mtu, nikainama kuokota kisimu changu lakini nilishangaa baada ya kuona simu kubwa hapo chini basi na yenyewe nikaiokota kisha nikanyanyuka.
Kisha nikampa simu hapo ndio nikshtuka baada ya kumuona yule kaka, aisee huyu kaka kila nilipo yupo mpaka nikaanza kumfikiria vibaya π
"Samahani jamani haikuwa makusudi.."
Nikaomba msamaha pale huku nikikiwasha kisimu changu ambacho baada ya kuanguka kilizima kabisa. Yule kaka hakujibu kitu zaidi aliniangalia yani ananipandisha na kunishusha nyiee huyu kaka alinifanya nijione mimi kinyesi π
Maana kwa ule mtazamo wake tu shoga enu nilinywea kama maji mtungini nikawa kama sio Shamim yule mwenye maneno mengi, yule kaka baada ya kuniangalia vile akaondoka zake tena kwa kunipiga kikumbo kabisa
Katika siku ambayo nilijiona mbwa na sina thamani basi ni hii siku, kila nilipokuwa nikikumbuka namna yule kaka alivyonitazama ndio kabisa nanywea yani nakuwa mpole
Basi ikabidi nirudi nyumbani na njaa yangu maana watu walikuwa ndio kwanza wanapakuliwa chakula ila mimi nikaamua kuondoka, hapo sijala tangu asubuhi
Nikashika njia mpaka nyumbani, nikamkuta mama Bella amelala kwenye mkeka na mimi nikakaa pembeni yake huku nimenyong'onyea.
"Mh mwenzetu vipi..??"
Mama aliniuliza baada ya kuona nimebadilika gafla.
"Walaa ni njaa tu mama.."
Nilimuongopea.
"Kwani huko utokako hujala..??"
"Aah mama unajua kule kulikuwa na watu wengi mpaka sehemu za kukaa hamna, chakula wameivisha saa sita watu kupanga foleni mpaka saa nane watu bado hawajaisha tu.."
Nilijieleza.
"Haya kwa ninavyokujua, humo ndani kuna ugali wa baba yako nilikuwa nimemtunzia lakini kasema haji saivi ko nenda kale huo arafu akija mpikie.."
Mama Bella alitoa maelezo, nikanyanyuka mimi na matako yangu haoo mpaka ndani nikafikia kwanza kunywa maji kisha nikashusha pumzi ndefu maana kwa sakata la leo sio la kitoto.
Baada ya hapo nikajibebea chakula changu mpaka nje alipokuwa amelala mama Bella, basi nikakaa na kuanza kula, kisimu changu kikaita tena kriiii kriii kutazama ni Bella huyu binti kila siku ye kunipigia.
"Hello.."
Nikapokea na tonge la ugali mdomoni πππ
"Oya we shekhe unasikia sie tumeingia nyumba kubwa hatukuoni upo wapi..??"
"Mwenzenu naongelea kwa mama Bella muda huu kwani nyie mpo wapi..??"
"Tupo huku, ila kuna mtu anakuulizia.."
"Mtu gani, na yupoje yupoje..??"
"Ni mubaba fulani hivi ako na kitambi.."
Kusikia ni mubaba nikajua ni lile lile lililokuwa linanibambia msibani.
"Bwanae kama mmekoswa kitu cha kuongea naomba ukate simu.."
"Sawa lakini anatusumbua sana.."
"Kwani hamuwezi kumtukana..??"
"Wamtukane nani..??"
Mama akaniuliza, nikabaki nababaika tu nisijue nimpe jibu gani.
"Aah mama haya mambo hayakuhusu.."
"Shamii we wakunijibu mimi hivi, kumbuka me ni mama yako ohoooo"
Mama alisema kisha akanyanyuka na kuingia ndani, niliona kweli nimemkosea mama yangu, nikakata simu na kuingia ndani ambapo nilimkuta anapanga panga nguo.
"Mama.."
Nilimuita
"Nisamehe mama kiukweli nimekosea sana kukujibu vile.."
"Hebu nitokee hapa, tena shika hii hela peleka kwenye msiba hii pesa ni mchango sasa ole wako ifike pungufu"
Mama alisema kisha akanitupia pesa, basi kinyonge nikainama na kuiokota huku nikiwa na majuto moyoni kwa kumjibu mama yangu vibaya..
ITAENDELEA
SEHEMU YA 4
SONGA NAYO.....
Nikaokota ile pesa na kuondoka kuelekea huko msibani huku moyoni nikiwa najilaumu sana kumbukeni hata ugali sijamaliza kuula na nimekula tonge kama tano hivi nikaagizwa
Basi nilitembea haraka haraka ili niwahi kurudi niweze kuumalizia ugali wangu, kweli bana niliweza kufika huko msibani nilikuta watu wamepungua sana hata magari yalibaki ya kuhesabu.
Basi bwana kimbembe kikaanza kwenye kumtafuta anayepokea michango, nilitafuta tafuta lakini wapi nikaona cha kujichosha nini nikaamua kuulizia
Nikasogea sehem fulan kulikuwa na mdada amekaa anapekua pekua simu yake, basi nikamsogelea hapo.
"Habari yako..??"
Nilimsalim yule dada.
"Salama.."
Alijibu huku akiwa ameangalia kwenye simu, nyie watu ambao wanamiliki simu kubwa huwa wanajikuta wao sijui nani sasa kuniangalia tu atakuwa kapungukiwa na nini.π©
"Samahani dada nilikuwa naulizia mkusanyaji wa michango ila jina nimemsahau.."
Nilijieleza, yule dada hata hakuniangalia badala yake alinielekeza sehemu kwamba nikamuangalie labda kwenye nyumba hizo naweza kumuona
Sikutaka maneno mengi nikamshukuru pale kisha huyo nikaondoka zangu huku nikijiuliza namna nitakavyoingia kwenye zile nyumba.
Basi bwana nikaanza na nyumba ya kwanza niliingia humo nikakuta magunia tu yananishangaa, nikatoka nasonya nikaingia nyumba ya pili humo nikakuta vyombo vimelundikwa kuna yale masufuria makubwa yani makubwa
Nikaangalia kidogo kisha kikatoka, nikaingia nyumba ya tatu humo nikakuta wamama wamekaa wengi kweli wakiwa na nyuso za huzni nikasalimia salamu moja wa kuitukia wakaitikia wa kukaa kimya wakaa.
"Samahani mama zangu, nilikuwa namuulizia mkusanya michango kaelekea wapi..??"
"Yupo nyumba kubwa.."
Mwanamke mmoja alinijibu..
"Asante.."
Kisha nikatoka nikijiuliza namna ya kuingia mule, basi bwana nikajipa roho ya ujasiri nikaingia, e bwana wee nilikuta vijana kama 10 hivi wazuri yani wazuri wengi wao walikuwa na ule ushombe shombe wa uarabu
Mh nikaguna kwanza maana hawa wakaka walikuwa wazuri ila sasa walikuwa serious, basi nikajikaza huku jasho jembemba likianza kunitoka..
"Samahanini kaka zangu.."
Niliongea kwa sauti ya kitetemeshi, Shamim mimi nilikamatika hii siku.
"Bila samahani mrembo.."
Mkaka mmoja akajibu, sasa bwana kitendo cha yule kaka kuniita mrembo yule mkaka ambae nimekutana nae zaidi ya mara tatu akanyanyuka na kuanza kunifuata nilipo
Moyo puh, maana kila nikikumbuka huyu kaka alivyonitazama mpaka nikajiona kinyesi nazidi kuogopa ila nikajikaza, akaja huku ananiangalia huyu kaka ana macho mazuri balaa
Umalaya huu Mungu niepushe nao, yule kaka alipokaribia kunifikia akapita pembeni huyo akatoka nje. Aah hata sikujalia nikajitutumua pale kuongea na waliobaki.
"Nilikuwa namuulizia mpokea mchango nimeelekezwa kaingia nyumba hii.."
Nilijieleza shida yangu..
"Ohooo " Kuna mkaka akajibu hivyo kisha akanyanyuka na kuingia kwenye chumba flani hivi, akakaa humo kama dakika mbili akarudi akiwa ameongozana na lile libaba lililokuwa linanibambia pale kwenye foleni
Nilipoliona tu hofu yote ikaniisha nikapata hasira za gafla, kumbe huyu ndio mpkea mchango nikasonya kisha nikageukia nje.
"Hatiame tumekutana.."
Yule mubaba baada ya kufika nilipo akaniuliza nikabaki kimya, nikatoa pesa kwenye nyonyo maana ndio wallet yanguπ nikampa ilikuwa elf tano.
"Shika hiyo andika mama Bella..."
Nilisema kisha nikaanza kupiga hatua za kuondoka muda wote yale yanaendelea wale wakaka walikuwa wanatazama uelekeo wetu mahali tulipokuwa tumesimama.
"Subiri kwanza, kwahiyo hii ndio inatosha..??"
Aliniuliza kwa kejeli, sikumjibu bali nikarudi mpaka alipokuwa.
"Hii ni pesa ya mchango na nimejitolea kulipa maana mimi na marehemu tulikuwa marafiki walioshibana, harafu nani alekwambia kuwa pesa ya mchango inatosha we vipi bwana.."
Nilijibu kwa hasira huku nikigeuka kuondoka nikashangaa nimedakwa mkono kwa mawazo yangu nikajua ni lile libaba nikageuka kwa hasira ili kulizaba kibao lakini nilisita hii ni baada ya kumuona kijana mzuri akiwa kanishika mkono.
"Dah samahani dada.."
Alisema yule kijana, hapo nikaweka uso wa upole ila moyoni najua mwenyewe π.
"Dada, naomba tusogee pembeni tuzungumze.."
Alisema kwa sauti ya upole, nikakubali ila mkono wangu nikautoa kwenye mikono yake tukasogea mpaka pale walipokuwa wale wenzake, akanionyesha kukaa kwenye sofa ambalo bei yake ni kubwa
Kwa mara ya kwanza Shamim mimi nikakalia sofa tena haya bei yake inaweza kuwa mahali yangu kabisa π, kisha nikakaa huku nikiwa makini kumsikiliza huyu kijana ataongea nini.
"Kwanza kabisa nikupe pole.."
Alisema mkaka mmoja, kwanza nikajiuliza pole ya nini nikabaki sielewi wajameni ππ
"Nashindwa hata sijui nikuelezeeje ukweli ni kwamba bibi yangu aliwahi kuniambia habari zako, na sikuwahi kabisa kukujua ila leo ndio nimekutana nawe ikiwa bibi yangu tayari marehem.."
Sikumjibu nilikuwa kimya, maana hata ningeongea basi ningeharibu kila kitu hivyo nikakaa kimya.
"Napenda uendelee kubakia hapa mpaka pale arobaini ya bibi itakapopita, lakini pia ningependa kukulipa japo kidogo tu kwa moyo wako wa upendo ulioonyesha kwa bibi yetu mpaka umauti kumkuta.."
" Asante.. "
Sasa nijibu nini ikiwa bahati imekuja yenyewe na kama mnavyoona hapa hawa watu wanaonekana wazito kwao pesa ipo maana kwa mavazi yao na zile perfume walizokuwa wamejipulizia zilionyesha zina bei kubwa.
Basi bwana siku hiyo bana pale nyumbani palichangamka baada ya Kuniona mimi, yani mambo yalikuwa π₯ kwa sababu inasemekana kuna binti ambaye alikuwa ana mtreat bibi yao sijui bibi au mama ila sasa huyo binti hayupo
Kutokana na kuigiza kwangu bwana nikapata sapoti tena kubwa π nyie nimeamini kabisa ule msemo wa kuwa unalala maskini unaamka tajiri ndio huu ulionikuta mimi
Shamim mimi kwa siku moja nilionekana binti wa kishua, maana walijua kunibadilisha vibaya mno, yani kile kijora ambacho nilitoka nacho kwa mama Bella nilivulishwa na kupewa mavazi mazuri ambayo sijawahi kabisa kuyatia mwilini.
Wakati yote hayo yakiendelea yule mkaka ambae nilikutana nae zaidi ya mara nne hivi alikuwa akiniangalia kwa jicho la hasira sana, kutokana na mawazo yangu nikafikiria labda anahasira na mimi kwa sababu ya kumuangushia simu yake
Hivyo nikaona nisipokuwa makini huyu kaka anaweza kunipa presha wallah, maana kwa ule mtazamo wake tu na nikikumbuka namna alivyoniangalia muda ule shoga enu naishiwa pawa π
Hivi ulishawahi kujiona mbwa kwa mwanaume, achana na hawa wanawake wenzetu twende upande wa wanaume imagine mkaka umetokea kuvutiwa nae lakini yeye hana time na wewe na pia anakuchukia tena ile chuki ya wazi wazi
Unajitahidi kadri ya uwezo wako akupende au labda akutamani lakini anakupuuza tena kile kipuuzo cha dharau mpaka unajiona mbwa au kinyesi ?? Nauliza ilishakukuta ??
Kama yalishakukuta naomba unipe pole kwanza lakini kama bado hayajakukuta nikupe pole na pia nikupe hata ka ushauri kadogo tu
"Hawa wanume ni mbwa π yani naposema mbwa naomba uelewe kabisa maana tabia za mbwa unazijua hasa hasa kuna ile ya mbwa kutoka kimapenzi na mbwa yeyote yule,π ndio sawa na hawa wanaume yani yeye hawezi tulia na mwanamke mmoja sijui atakufa au hilo me sifahamu
Kikubwa ishi nao kwa akili hawa viumbe wanaoitwa wanaume, usimuonyeshe kama unampenda kwa dhati wewe msikilize na fuata maneno yake anayokwambia
Ili kulinda ndoa yako au mpenzi wako usijiweke hadharani na kumwambia hisia zako kuwa UNAMPENDA kama utamwambia shoga angu utakuja kukumbuka maneno yangu"
Nakwambia sasa ila moyoni unakana "oooh Shamim we muongo wanaume wote hawako hivyo," Sasa endelea kupumbazwa na maneno yake ipo siku utakumbuka hili
Na sio kama nipo hapa kukufanya ujisikie vibaya, hapana dada zangu me naongea yale yenye ukweli ndani yake maana yalinikuta kwa mwanaume mmoja hivi fala sana huyo mwanaume na kuanzia hiyo siku nikajiapizia sitaonyesha upendo wa dhati kwa mwanaume yoyote yule
Maana alijua kuniumiza, nilikuwa namuamini kupita kiasi chochote alichokuwa akiniambia niliamini kwa asilimia mia moja, lakini kuna siku hii siku bwana aaah sitaisahau kwenye maisha yangu....
ITAENDELEA DEARS........
SEHEMU YA 5
SONGA NAYO........
Basi bwana baada ya kukaa sana pale msibani na yule mkaka hakuacha kuniangalia kabisa nikaona sio mbaya kama nitaenda kumuomba msamaha ili nijisikie amani. Maana kwa namna alivyokuwa akanitazama nilikuwa nashindwa kujiamini kabisa
Basi nikanyanyuka mpaka alipokuwa amekaa wakati huo watu wachache sana ndio tulikuwa tumebaki mle ndani na wengi wao walikuwa bize sana, nikasogeza makalio yangu na kukaa pembeni yake.
"Habari...??"
Nilimsalimia, hakunijibu akachukua tissue na kujiziba pua, mnajua nilijisikiaje π nawauliza nilijisikaje mnajua ??? Kwa mara ya kwanza nilijiona nanuka ππ
Huyu kaka alijua kunifanya nijione takataka, kinyesi, na pia kujiona mbaya. Kwanza kabisa baada ya yule kaka kujiziba pua na tissue nilishtukaπ
Nilipokumbuka kuwa nilitoka nyumbani sijaoga nikajua kweli nanuka π nikaanza kwanza na kujinusa kwapa zangu ππ
Baada ya kujihakikisha kuwa sinuki nikamgeukia yule kaka.
Nilimuangalia yule kaka bila kummaliza kisha nikanyanyuka nikiwa na hasira sana, yani katika siku nilijiona na mikosi ni hii siku moyoni nilikuwa najilaumu sana basi nikanyanyuka ili kutoka nje nikashangaa nimeshikwa mkono
Ikabidi nigeuke kuona nani ambaye akanishika nilistaajabu baada ya kuona katoto kazuri umri wake kama miaka 10 hivi kama sio kumi basi 11
Basi nikainama ili kukasikiliza
"Auntie kuna mtu anaikuita.."
Kaliongea kale katoto.
"Ni nani..??"
Nilimuuliza
"Ni mwanaume anakuita.."
"Yupo wapi..??"
"Kuleeee..."
Kalisema huku kakinyooshea kidole sehem ambayo palikuwa pamejificha kidogo, nikaangalia sikuona mtu nikamgeukia yule mtoto.
"Kwani huyo mtu yupoje yupoje..??"
Nilimuuliza
"Aah ana tumbo kubwaaa kama la ng'ombe..."
"Mh.."
Nikaguna kwanza, maana kwenye maisha yangu sijawahi kuona mtu ana tumbo kubwa kama la ng'ombe, nikiwa sielewi elewi nikasikia kama kuna mtu kacheka harafu akanyamaza
Nikainua kichwa kutazama nikakuta pametulia zaidi yule kaka alikuwa anachezea simu yake, yule mtoto aliondoka huku akiniacha nikiwa sieleiw "eti tumbo kubwaa kama la ngombe "
Nikawa narudia maneno ya yule mtoto, nikapotezea nikijua utoto unamsumbua yule dogo nikaendelea kukaa, yakapita kama masaa mawili hivi muda huo imefika saa kumi na moja jioni
Kwa mbali nikaona kuna mtu anakuja uelekeo wangu na ukiangalia nilikuwa nje nimekaa zangu na watu walikuwa bize na majukumu yao.
Basi yule mtu baada ya kufika nilipo alikuwa kijana mdogo sana kwa kukadiria basi ana miaka 17, yule kijana akaja mpaka nilipokuwa.
"Habari yako..??"
Alinisalimia, sikumjibu nikamuangalia tuu kisha nikanyamaza maana kupigizana kelele na kijana ambaye hajui kusalimia ni sawa na kuumiza figo..
"We ni bubu..??"
Akaniuliza tena, sikumjibu moyoni nilikuwa na hasira kwa sababu kaniita mimi bubu yule kijana akabaki anacheka kwa kejeli kisha akazungumza.
"Unaitwa na bwana ako huko.."
Alisema yule kijana kisha akaondoka, nikabaki sielewi bwana gani ambae ananiita maana mimi kama mabwana ninao wengi tena wengine mpaka nawasahau kabisa..
Basi ninyanyuka huku nikielekea kule alipokuwa kanielekeza yule mtoto basi nikaelekea huko palikuwa nyuma ya nyumba kubwa hivyo nikaenda kufika huko bwana nikakuta huyo bwana angu eti ni yule baba aliekuwa ananibamba pale kwenye foleni
Kwa hasira niliyokuwa nayo nikageuka kuondoka lakini akadaka mkono wangu na kuushika kwa nguvu.
"Nini bana niachie.."
Nilifoka kwa sauti ya ukali, lakini yule baba alikuwa na nguvu sana akanisogeza mpaka kwake na kunikumbatia kwa nguvu hata kufurukuta sikuweza kutonakana na ule mkumbato wake nikahisi kitu kigumu kikinigusa kunako ikulu
Nikajua hapa kuna uwezekano wa kuliwa kama nisipokuwa makini hivyo ikabidi nitumie busara na maneno ya mahaba ili angalau anisikie.
"Aaah we mzee utaniua unajua umenikumbatia tuu nikajisikia raha yani ambayo sijawahi kuipata kabisa maisha yangu yote.."
Nilimwambia huku nikijaribu kujitoa.
"Kwelii??."
Aliniuliza, huku akipumua kwa shida.
"Kabisa yani, hapa sina hali kabisa.."
"Me pia, ila ningependa unipe hata kidogo mwenzio siwezi kuvumilia.."
Aliniambia, hapo sasa macho yakanitoka jamani pamoja na kuwa binti machachari sana sizijui sehemu za siri za mwanaume zilivyo bali navijua vile vya watoto wadogo ambavyo bado vidogo mno.
Kingine msichokijua binti wa mama Bella mimi bado bikra, πyani bado mpya kabisa toka nitoke kwenye tumbo la mama yangu sijawahi kukwichi kwichi π na sijui hata uume wa mwanaume unaingiaje huko kwa bibiπ
Basi bwana yule mbaba akaendelea kunishika shika mala anibinye makalio mala chuchu zangu nikawa naona Kero kabisa maana mwanaume sikuwa na hisia nae na pia sikumpenda
Akawa anaendelea na mipapaso nimetulia tu napanga tukio la kumfanya mbwa huyu, na atagharimu pesa kubwa kwa sababu ya kuushika mwili wangu.
Basi bwana yule mubaba akaendelea na mambo yake kuna muda ile mipapaso yake ikawa inanisisimua shoga enu natamani kumpa ushirikiano lakini nashindwa kabisa
Kila nikikumbuka maneno ya mama aliyoniambia najikuta napata hasira na maumivu kwa upande mwingine, hapo sasa nikashikwa na hasira kabisa nikamsukuma yule mubaba kwa nguvu sana
Akaenda kupepesuka huko, kisha nikaokota mtandio wangu uliokuwa umeanguka nikajifunga kiunoni nikatengeneza dera langu vizuri na kukaa stand-by kwa ajiri ya mapambanoπ
"Ukijaribu kunisogelea natoka na taya zako za juu.."
Nilimwambia, nilipomtazama vizuri kwenye suruali yake niliona pametuna sana, nikasema hapa ni kutimua tuu maana niliwahi kusikia habari za wanaume kuwa wakiwa wamepandisha nizuka yao huwa na nguvu sana
Vile vile huwa hawana huruma hata kidogo wanaweza kubaka mtu harafu baadae ndio wanaanza kujutia, chapu nikainama na kushika sendo zangu mkononi na kutimia mbio kuelekea kule walipokuwa watu
Katika kukimbia kwwangu huku nageuka nyuma kuangalia kama yule mubaba ananifatilia niligongana na mtu, nikashtuka kwanza baada ya kujua kuwa niliemgonga ni yule mkaka
Mabalaa juu ya mabalaa nikabaki nauma uma meno kama sina hakili nzuri maana hata ningejitetea ningeishiwa kushushuliwa na mwisho nijisikie vibaya.
"We ni chizi...??"
Nikiwa nawaza cha kuongea nikashangaa naulizwa hilo swali, ambalo kwa namna moja au nyingine lilinikera sana yani mimi wa kufananishwa na chizi ikiwa mtaani kwangu naongoza kwa
INAENDELEA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi