VYOTE NDANI GONGA94
BINAMU WEWE UNGEWEZA? SEHEMU 09
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
ENDELEA........
Nimepindua meza sasa na hakuna kitu mtaweza kunifanya" Baada ya kusema hayo wawili hao waliondoka.
Mama na mdogo wangu walinifariji. Sikuwaelewa kwakweli kwa jinsi ninavyompenda Sony tena ndiye mwanaume wangu wa kwanza niliumia mno.
Siku hiyo nililala nyumbani. Majira ya asubuhi niliamka nikajianda kwenda kazini kama kawaida.
Nilifika kazini boss alipofika tu aliniita ofisini kwake.
"Nice nisamehe najua nimekuumiza" Alianza kujiongelesha.
"Hapa sio mahala pake boss"
"Yaani unataka kunipangia cha kufanya au cha kuongea umesahau mimi ni nani kwako?" Sony aliongea kwa ukali
"Lakini Sony kwanini unapenda kuniumiza eeeeeh! Kosa langu mimi ni nini mpaka umekuwa mwiba moyoni mwangu?"
"Najua nimekukosea ila Manka ni mjamzito siwezi kuiacha damu yangu iteketee"
"Vipi kama na mimi ni mjamzito utamuacha Manka?"
"Una mimba?, Sony aliniuliza.
"Nimekuuliza tu kwa wema"
"Manka siwezi kumuacha kwa sasa nipo nae karibu kwaajili ya mimba tu ila akijifungua nitamchukua mtoto wangu na kuachana nae kabisa"
"Hivi Sony nguvu za kulala na Manka ulizitoa wapi na unajua kabisa yule ni ndugu yangu. Umenikosea sana"
"Ndo maana naomba msamaha siwezi kuelezea ilikuaje"
Niliona ananivulugha tu. Nilitoka ofisini kwake nikaenda eneo langu la kazi.
Majira ya saa kumi jioni kabda ya kutoka kaxini nilishangaa Baada ya kumuona Iron.
"Huamini kama nipo hapa kwaajili yako?"
"Wewe huyo upo hapa kwaajili yangu?"
"Yes my Lady"
"Heeeee! Makubwa haya"
"Tena madogo yana afadhali" alivyonijibu hivyo niliangua kicheko ๐๐๐.
Basi mie nacheka yeye ananiangalia kwa tabasamu.
"Una lips nzuri sana, tabasamu lako pia ni bomba sana Nice. Naomba kama hutojali leo usiku tutoke dinner"
Muda Iron ananiambia kutoka Dinner Sony alikuwa anatoka ofisini kwake kwaiyo alisikia. Kwa kumkomoa Sony nilikubali kutoka Dinner na Iron.
Iron mwenyewe hata hakumuona Sony alifurahi mwenyewe kwa kukubali ombi lake aliniachia kadi ya namba yake na yenye wadhifa wake huyo akaondoka.
Baada ya Iron kutokomea Sony alinifuata kwa hasira.
"Umeanza uma....laya?"
"Unaongea kuhusu nini?"
"Nipe hiyo code aliyokupa" Nilitaka kumgomea ila kwa namna alivyokuwa anaongea kwa makasiriko nilikubali kumpatia, baada ya kumpa alichukua mkasi alianza kuikata kata.........ITAENDELEA.........
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi binamu-wewe-ungeweza-sehemu