PENZI LA OMBA OMBA 10
“ zamu yako kufanya nini, maana siku hizi umekuja na tabia sizielewi kabisa, nikasema, akaniangalia kisha akacheka na kusema “ najua wewe huelewag ila usijal mdogo mdogo utaelewa kila kitu, akasema …
Basi siku hio simu yangu alikaa nayo shureymu na wakat wote ilikuwa imezimwa, basi tukashinda pale tukiwa tunasaidiana usafi, tukapika pamoja, tukala na kuanza kupiga story na shureymu alikuwa anaonekana kama anafuraha sana akiwa na mimi, na kila wakat alikuwa ananiambia kuwa nimuahidi kuwa siwez kuwa mbali na yeye, na mm mtoto wa watu sikuwa na hiyana nikamuahidi pale, na alikuwa anaonekana kama ananipenda sana, kwa maana kuna muda alikuwa anaweza akawa ananiangalia tu huku aacheka, nikimuuliza shida nini, anaishia kusema “ mwanao kabarikiwa sana kupata mama kama wewe…..
Basi tumekaa pale, na kwenye majira ya kama saa kumi jioni tukasikia ari linaingia, shureymu ikabidi achungulie ni nani huyo, nikashangaa anasonya kisha akasema “ mamamaaaa, kisha akaend chumban kwake na kuvaa vzr, maana siku nzima alishinda akiwa kifua wazi….
Kweli akaingia ndani, mwanamama flani hivi wa kwenda, alikuwa amevaa madhaabu kama ugomvi, na libazee, alikuwa anaonekana kabisa ni jimama la kishua, na alikuwa anaongozana na bint , ambae alikuwa anaoenekana kama hana zaidi ya miaka 25, alikuwa amevaa na yeye abaya na mtandio, wakaingian ndani, ikabidi niwakaribishe ndani, Yule mama akaniangalia sana, nikamsalimia, akaitika kisha akasema “ angalau mwanangu amepata mfanya kazi kwa maana nyumba inanukia vzr kuliko alipokuwa anaishi pekee yake….
Sikumjibu kitu, zaidi sana nikawauliza wanakunywa nn…
‘ niletee maji, akasema Yule mama, na Yule bint akasema kinywaji chochote, kweli nikaleta maji na juice nikawapatia, mara shureymu akatoka akiwa amenuna huyo…
“ unanuna nini, kwani mimi ndio nilisababisha usioe mpaka sasa hivi, akasema mama yake mara baada ya kumuona shureymu….
“ mama lakin, kwani nimeseka siowi, nimeshampata mwanamke wa maisha yangu naomba mnipe muda na nitakuja kuwatambulisha kwenu siku sio nyingi, akasema shureymu…
“ nakujua wewe, na najua kabisa hapo unataka kunipooza tu na huenda hauna mtu yoyote Yule ambae umepenga kumuoa, sasa sitaki kupoteza muda, unamuona huyu bint niliekuja nae, anaitwa wahida, ni mtoto wa rafiki yangu, ni mrembo kama unavyomuona, naomba umuangalie kwa makin kisha uhakikishe unakuja na jibun zuri kwangu, akasema mama yake shureymu kisha akanyanyuka na kuondoka zake, akamuacha wahida pale…..
Shureymu alikuwa amenuna huyo, yaan muda mwingin alikuwa anautumia kukaa na mm na sio huyo mwanamke alieletewa na mama yake, yaan ni kama hakuwa anataka mazoea nae hata kidoo, mwisho akaona asipindishe pindishe akamfata kisha akamuambia kuwa “ mm kuna mwanamke Namenda, naomba nisikupotezee muda, kama unaweza kupata mwanaume naomba uhakikishe kuwa anakuoa, kwa maana naweza nikasema nimekukubali, nikakutumia na kukuacha kwa maana sina hisia kabisa na wewe, akasema shureymu…
Wahida alishusha pumzi kisha akasema “lakin mm nakupenda na unajua kabisa kuwa nakupenda kwa muda mrefu sana, na nimeshkuru sana kwa mama yako kutaka niolewe na wewe , na nimeridhika kabisa, naomba usimvunje moyo mama yako, na kingine kwenye kikao cha bodi unaakiwa kumtambulisha mke na mwanao, najua mtoto huna ila angalau uwe na mke, na mm nimekubali kabisa kwa moyo wangu mmoja kuwa mke wako, akasema wahida…
Shureymu aacheka kisha akasema “ aliekuambia kuwa mimi sina mke na mtoto ni nani, kwa maana mke ninae na mtoto ninae, na kuhusu utambulisho kwenye kikao cha bodi hilo niachie mimi, kwa maana wewe huna nafasi machoni wala moyoni, ni kweli wewe ni mzuri ila tafuta mwanaume ambae anaweza kuuona uzuri wako, akasema shureymu, Yule bint alishusha pumzi kisha akasema “ ni kweli nimekuelewa , naomba nikutakie maisha mema, akasema wahida kisha akaondoka zake…
“ sasa kwenye hicho kikao utampeleka nani, kwa sababu ninaamin kuwa hauna mwanamke kwa sasa na ndio maana unapataga muda wa kuongea na mm siku nzima, na usiku kucha, nikasema…
“ ni kwamba unanisimanga au unaniambia, ni kweli sina mpenzi, ila kwani wewe huwez kuwa mpenzi wangu na ukanikomboa kwenye hilo tatizo, akasema shureymu….
“ wewe mm siwez kuigiza, kwa maana nina my wangu na anawivu, si unamjua, nikasema, nikashangaa shureeymu amehema kwa nguvu, kisha akasema kwa saut ya unyonge kuwa “ sio wewe ila nilikuwa nataka tu kukutolea mfano, nan i kweli sijui nitampata wapi huyo mwanamke wakumpeleka, ila naamin nikitangaza dau wanawake watakuja, ila nina uhakika tangazo litaonekana na ndio maana nataka kufanya hili jambo kimya kimya, akasema shureymu…
Alafu kuna wazo nimepata, naomba unisaidie kama hutajal, akaendelea kusema shureymu…
“ jambo gani?...
“ nataka kukulipa, unaonaje kama nikikulipa alafu tukaenda wote kwenye party, alafu nikutambulishe pale , kwa maana wewe vigezo vyote unavyo, kwa maana una mtoto, akasema shureym..
“ sipendag kudanganya mm, naomba ufanye mambo yako mwenyewe, nikajibu kisha nikawa nataka kuondoka niende zangu ninapoishi kwa maana siku hio nilishinda na shureymu siku nzima….
“ naomba unisaidie plz, nitakulipam pesa yoyoteb ile unayoitaka, akasema shureymu, nikagoma kisha nikamuambia kuwa “ mwanaume wangu akijua ataniacha, kwa maana ataona kama namuigizia kuwa nae, na wakat nampenda kweli, nikasema nikashangaa shureymu kashusha pumzi kisha akatabasamu na kusema “ yaan unavyomtaja huyo mwanaume kila dakika, utasema ndio mwanaume pekee duniani, ila ni sawa nitatafuta namna nyingine ya kufanya ili nisije nikadhaliliakla akasema shureymu, na kunitaka nisiondoke nilale siku hio pale kwake, kiukweli sikukataa, kwa maana ilen nyumba ya shureymu ilikuwa ni kubwa na inazaidi ya vyumba vitano vya kulala, hivyo kulala pale haikuwa tatizo kabisa……
Basi kwakuwa muda ulikuwa tayar umeshaenda basi tukaagana na kwenda kulala, kila mtu akaenda kulala anapostahili, kwa maana mimi nilienda kulala na mwanangu na shureymu akaenda kulala chumban kwake, sasa nikiwa nimelala nikaanza kuhisi kama kuna mtu ananishika nywele nikawa nahisi ananiambia “ sijui imekuwaje mpaka nimejikuta nakupenda sana, ila jaman unajua sana kujal naomba uelewe sasa hisia zangu, sasa kwa namna nilivyokuwa na kichwa mbovu nikajua kuwa nilikuwa naota, yaan nilipoamka tu kitu cha kwanza nikamfata shureymu na kumuambia kuwa nimemuota…
“ eheee umeniotaje…
“ ety unasema unanipenda, au usikute unanipenda kweli wewe, nikasema ..
“ nani mimi!, yaan mm nikose kazi ya kufanya nianze kukupenda wewe si nitakuwa nimechanganyikiwa, akasema shureymu, mara simu yangu ikaanza kuita, na mtu pekee ambae alikuwa akinipigia alikuwa ni muswahabu, basi nikapokea simu yake, na alikuwa anaongea kwa wasiwasi muda wote huo, akawa ananiuliza kilitokea nn mpaka sipokei simu zake mara sipatikani, nikashangaa sauti inatoka nyuma yanu ikisema ‘ alikuwa na mm, huyo mwanamke ni mwanamke wangu yaan mpaka muswaabu akanywea, akajua kuwa hana chake tena akaamua kukata simu, alafu shureymu akawa anafanya mambo yake kana kwamba hakuna kitu chochote kile alichokifanya…
NAKUJA…
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni