CEO SIKIMBII TENA NITAVUMILIA*1---2 *____________________________________* SEHEMU YA 1 Kama uliwahi sikia mtu kaokota dodo chini ya mpera basi ni mimi. Naitwa Nasma Majid ni mtoto wa pekee kwa mama yangu na baba yangu licha ya kwamba tuna maisha ya kuung
Sasa leo kwenye pita pita zangu nilikua natembea tu kusipo na direction mitaa ya kwetu Buguruni, kuna mtaa nilipita kulikua kimya sana lakin kwa mbal naskia minong’ono kwenye jumba moja bovuu kweli yani , nikajikuta nataka kujua kuna nini maana mimi nae ni mmbea sio poa ila ukinitizama hat uzanii nazid kusogea nasikia ‘huyu si anajifanya mbishi sana sasa tumpige risasi kwa sababu tunachotaka anajifanya hawezi kutupa tutashughulika na mtu mwingine kwenye familia yake tuliambiwa akiweza kusema akimaliza tumuue na asiposema pia tumuue kupoteza ushahidi’ nikajikuta tu nachungulia kuangalia si ndy kukuta mkaka wa watu katekwa kafungwa miguu na mikono na inavyoonekana kashapigwa sana…
maan tu kwa alivyochakaa hapana yule jambazi akatoa pistol anataka kushoot, nikajikuta Napata mzuka wa kwenda kukingaa ile risasi hata sijui ujasiri niliutoa wapi….
Baada ya kukinga ile risasi sijui wale majambazi walijua nimekuja na polisi wakaondoka haraka , nikabaki na yule mtekwaji akabaki ananikodolea mimacho tu, akajitahidi akajifungua pale alipokuwa amefungwa, ili anisaidie kuniwahisha kupata tiba, lakini hakuweza, alikuwa na hali mbaya mno, bahati nzuri walinzi wake walifika ni kama bahati tu alikuwa na kichip cha kujua alipo alikiweka kwenye kifungo cha shart yake, walifika na kutuokoa,
Yule kaka alivyofunguliwa tu japo alikuwa na maumivu lakini alijitahidi akaja nilipodondoka, akanibeba akawa ananitoa nje, ndio kumbukumbu zikawa zimekata nilianza kuona tu giza sikujua tena nini kiliendelea, nakumbuka nimekuja kuzindika nipo kwenye chumba tena nipo peke yangu ila kunavyoonekana sio hospital ni chumba cha mtu nikawa najiuliza kichwani "hichi ni chumba analala mtu au ni sehem zile wanaogiziaga wahindi" mara naskia mlango unafunguliwa anaingia yule mtekwaji akaniulza "upo sawa now?" nikaitika kwa kichwa kuonesha kwamba nipo sawa akaakaa pembeni yangu akaniambia "asante , naitwa Nasser Mohammed "huku akinipatia simu yangu "ilikua inaita sana alikuwa mama yako nimemuelekeza ulipo anakuja na baba yako wana wasi wasi sana nimewaambia upo sawa" nilitikisa tu kichwa kuuumanisha nimekubali maan hata nguvu ya kuongea sina kwa jinsi nilivyochoka na maamivu maan sio kuuona tu na kupigwa juu toka nizaliwe sijawah hata kufikiri kam ntakujaga hata kuishuhudia bastola ila hili la leo lazma ntaaliandika , kwenye diary maan sio kuuona tu na kupigwa juuu…
ITAENDELEA.....
SEHEMU YA 2
Tunaeendelea tulipoishia nilipitiwa tena na usingizi nikaja kuamshwa na yule mtekwaji yaan Nasser kueguka pembeni namuona mama na baba wamekaa , mama akanikumbatia nakuniuliza kama nipo sawa nikamjibu kwa kichwa baba ananiangalia tu maan kashindwa hata aseme nini mama ndy akaamua kumuuliza Naseer ilikuaje mpaka nikapigwa risasi Naseer ikabidi awaelezee kila kitu kilivyokua Naseer ilibidi awaelezee kila kitu na kuwaomba kwamba nibaki nae pale kwa ajili ya usalamaa wangu kwasababu wale watu hawatoacha kunifuatilia mama angu akaanza kulia na kulaumu kwanini nimejiingiza kwenye mambo yasio nihusu baba alijaribu kukataa na kumwambia kwamba mimi ni mtoto wa kike nabakije na mtoto wa kiume humu ndani…
nyumba nzima kwasababu inavyoonekana Naseer anaishi peke yake, Naseer akamtuliza baba akamuelewesha mpaka baba akaja kwenye mfumo na kukubali ,baba na Nasser walitoka nje kidogo mama akabaki na mimi hapo kuongea hata siwezi nipo nipo tu yaan….
Mama akaniambia niwe makini nipo na mtoto wa kiume nisijiachie sanaa, nikaitika kwa kichwa kumaanisha kwamba nimeelewa mama nae akatoka nikaendelea tena kulala nakuja kushtuka usiku sana naangalia pembeni namkuta Naseer kalala pembeni yangu, kajikunyata hapo nguvu za kujiinua nilikua nazo nikainuka nikamfunika shuka nikawa sina usingizi hata kidogo yaani, ikabidi tu nikae maana jeraha bado linaniuma si ndy nikaanza kukagua chumba sasa kilivyoo jamn ni bungalow bonge la chumba nikasema hivi jaman huyu analala peke ake humu haogopi hapo hata nje sipajui nichumbani tu humo maan nilifika nimezima na damu nyingi zilikua zimemwagika, hivyo lazima ningezima tu hata ingewezekana kufa ningekufa tuu, nilikaa nilikua sijui ni saa ngapi hata usingiz ukanipitia nakuja kushtuka tena asubuhi kuangalia pembeni Naseer hayupo, hata sikujali sana na wala sikuwazaa nimekaa naskia mlango unafunguliwa anaingia Nasser na mdada na kumwambia Naseer atoke nje Nasser akatoka yule mdad akanambia inabidi aniogeshee ni mwanamke mwenzangu, ila namuonea aibu hhh😆 jaman nikamwambia asijal nawez mwenyew akacheka akaniuliza "unaona aibu?"….
Nesi aliniuliza huku ananitizama kwa makin nilitabasamu tu huku natizama chini akanambia "Nasma huwezi simama mwenyew basi nikusiadie tu" hapo nikakubal japo kishingo upande akaenda akaniogesha vizur tu akaniweka kitandani huku nina taulo tu akanifunika shuka maan zile nguo nilizokua nimepigwa nazo risasi ndy nilikua nimezivaa toka muda ule hapo akatoka nje na kumuita Naseer, Nasser akaingia ndani akapewa dawa na maelekezo akaambiwa nitakaa sawa soon tu …
Zilipita wiki 2 sasa asa hivi naweza inuka nikatembea vizuri sasa sijawahi kutoka mle chumbani hata kwa bahati mbaya toka nilipoingia ,leo Nasser akaniambia nitoke nae sebleni kwasababu sasa naeza tembea bila tatizo lolote lile, nikasema sawa nikatoka nae yeye mbele mimi nyuma jaman hhhh nacheka kama mazuri kumbe kuna watu wanaishi afu kuna sisi tunaoishia😃😆😆 jaman mhhhhh nilishangaa huyu anaishi kwenye nyumba au kwenye hoteli, ila najiulizia moyoni tu tukaenda mpaka sebleni wenzetu wana dining room sisi tushazoea kula kwenye mikeka hhh😆😆 jamni aibu naona mimi, nikakaa kulikuwa kushapangwa pale kila kitu sasa nikawa nashangaa mbona sioni mtu hapa ndani ,alielewa ninachowaza akanambia, "naishi mwenyew ,wazazi wangu hawapo wapo London ndio wanapoishi hivyo huku Tanzania mimi nimewekeza biashara zangu ndio maan nipo huku" aliongea huku ananitizama kwa umakini kweli yaani nikataka kumuuliza kwa nini ile siku ulitekwa tena ulitekewa uswahilini ila moyoni nikasema niache umbea hayanihusu akaendelea kuongea "asante sana kwa ile siku maan ningekufa kama usingejitokeza" nikasema kwa chin chini "kwan mimi nisingekufa ila watu wenye hela bhan😏" akaendelea kusema "sina cha kukulipa ila ntafanya kwa uwezo wangu najua unajiuliza kwa nini nilitekwa tena mazingira ya uswahilini wale ni maadui wa baba angu kwa muda mrefu na wanamtafuta kama sindano iliopotea hivyo waliniteka ili niweze kuwaeleza baba angu yupo wapi lakin sikuweza kusema wamekua wakimuandama sana baba angu hadi kuna kipindi walimfuata huko Loss Angels, na ndio sababu baba angu kuhamia London na familia yake sasa walifuatilia na kujua kwamba huku kuna mtoto wake wakaona wakiniteka itakua njia nzuri ya kumpata na nisiposema waniue kabisa ili baba aogope na ajitokeze, lakin kabla ya kushoot ukatokea wewe hapo nashukuru sana" nikasema "sawa pole enhe nataka kwenda kwetu"….
akaniangalia akanambia "huwezi kwenda kwasababu wew hapo unafatiliwa pia ushaingia kwenye haya mambo na ukikaa bila ulinzi unaeza ukauliwa" ,wewee😱😱 niliogopa sio poa nikaamua nitulie tu maan mhh ni hatari sio kidogo huku nimeanza kutetemeka akainuka akanisogelea na kunishika mkono akanambia "usijal upo sehem salama hapa kuna heavy security hakuna wa kukupata ukiwa hapa unaeza kukaa hapa " nikasema kwa sauti ya chini na kwa taratibu mnoo "ila natka kwenda kwetu"….
akanambia "ukienda kwenu unaweza sababisha matatizo hadi kwa familia yako binafsi hata hivi nimewaamisha mkoa baba na mama yako kwa ulinzi zaidi na huko nimewajengea nyumba, wale majambazi ni watu wakubwa hawashindwi kuipata familia yako kwa muda mfupi ", nikamuuliza "kwahyo familia yangu ipo kwenye matatizo?" akanamby "usijali kwa sasa ipo salama kabisa hakuna shida", nikawa najiuliza kwahyo nitaisshi na huyu mwanume niliekutana nae kwa bahati mbaya milele?, akanitizama akaniambia "naelewa hofu yako hata hivi baba ako alinieleza kila kitu kuhusu wewe hivyoo nimekuajiri unakua personal assistance wangu." nilishtuka miaka yote natafuta kazi hata mtu wa mapokezi kweli asa hivi kila kitu connection kiutani utani tu Napata kazi akasema kazi itaanza kesho tutaondoka wote hapa nyumbani usijali…
Nikaona kwa namna nyingine nimepata ahueni na mimi nina kazi kwa sasa nitapumua kidogo akanambia natoka naenda kazini jisikie huruu ukitaka kupika, kufanya chochote we fanya tu usiwe na wasi wasi jiskie Amani akawa katoka nikabaki mwenyewe
ITAENDELEA……..
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

