Hadithi:*POOR RICHMAN* (Alijifanya amefirisika na Kuwa Masikini ili kuwajua wanafiki kwenye Maisha Yake) Sehemu Ya 4
Jovin akiwa kajiinamia anamwaga chozi alishituliwa na Maji machafu ambayo alimwagiwa mwilini mwake.
"Pumbavu ondoka haraka hapa Kwangu!! Baba Yasinta ebu muondoe huyu kenge wako kabla sijafanya kitu kibaya!" Baada Ya kumumwagia Maji machafu, Mama Damian aliendelea kufoka!.
Muda huo huo Bwana Damian alifika pale nyumbani, kitu kilicho muuma zaidi Jovin ni Kwamba Damian alikuwa kaambatana na Nuru!.
Yaani Bila aibu walikuwa wameshikana viuno pasina kumhofia Jovin.
Kumbuka kipindi hicho Damian Yeye Bado alikuwa anafanya kazi kwenye kampuni ambayo ilikuwa inasadika kwa kipindi hicho inamilikiwa na Mr Tahir!.
Basi Jovin Roho ikiwa inamuuma aliamua kuondoka na kurudi nyumbani, kama kawaida Siku iliyo fuata aliingia mtaani kupiga madili ya saidia fundi!.
Lakini alipo rudi nyumbani Mida ya Jioni pale nyumbani Jovin alikuta ndani ni kama uwanja Wa mpira, yaani kulikuwa hakuna kitu hata kimoja, mpaka vijiko Nuru alikuwa kabeba!.
Kiukweli Jovin aliumia Muno, Baada ya kupeleleza aligundua kwamba vitu vyote Nuru kaenda kuviuza kwa Madalali na tena alikuwa kaambatana na Damian!.
Jovin hakuwa na la kufanya aliendelea kujifanya mjinga ili kuwajua wanafiki Wote kwenye maisha Yake.
Jovin alijikuta anapoteza marafiki karibia wote kutokana na ile Hali Yake, hakuna hata Mmoja aliye Chagua kumsaidia Jovin pindi alipo omba msaada!.
Kitu kilicho muuma Jovin zaidi ilikuwa ni Mara Baada ya kugundua kwamba Damian anaishi na Nuru kama mume na Mke, yaani Damian alikuwa kamchukua Nuru mazima!.
Kiukweli Jovin uvumilivu ulimshinda, kitu alicho kifanya aliamua kutuma ujumbe kwa meneja Wa Kampuni Zake ambapo meneja Huyo alikuwa anajua ukweli Wote na mpango mzima Wa Jovin.
Ujumbe alio utuma Jovin ilikuwa ni kwamba Damian afukuzwe Kazi, maana Sasa bwana huyo alikuwa kazidi na alikuwa anatamba na Pesa bila kujua Mtu anaye mpa huo mshahara ni Huyo huyo Jovin.
Basi Siku hiyo kama kawaida bwana Damian akiwa kajichomekea na Suti Yake Huku akiwa anatembelea Gari ya kampuni, Baada ya kufika tu ofisini alikutana na Barua mapokezi, ilikuwa ni Barua ya kufukuzwa Kazi!.
Kwanza bwana Damian jicho lilimtoka na mapigo ya Moyo yalianza kwenda kasi!.
Aliuliza Sababu za kufukuzwa Kazi, alicho jibiwa ilikuwa ni kwamba aende akamuulize meneja!.
Ni kweli Bwana Damian alichanganya pariga Zake mpaka kwenye ofisi ya meneja!.
"Wewe kufukuzwa kazi ni agizo kutoka juu, na tabia Zako ndo zimefanya ufukuzwe Kazi, maana unachafua taswira ya kampuni!" Hayo Ndo maelezo ambayo Damian alipewa!.
Kiukweli Siku Hiyo ilikuwa ngumu Muno kwa kijana Damian, maana ile Kazi Ndo ilikuwa kila kitu chake, yaani Ndo ilikuwa inamuweka Mjini na pia alikuwa anawasaidia wazazi Wake kupitia ile Kazi, maana alikuwa anapewa mshahara munono!.
Damian alijikuta amekuwa Sasa Mtu Wa mawazo Huku tulizo lake likiwa ni pombe!.
"Huyu mpuuzi ngoja visenti vyake vya akiba viishe kama ataniona tena, muache abweteke badala ya kutafuta Kazi!" Hayo yalikuwa maneno ya Nuru ambayo alikuwa anajiongelesha mwenyewe Mara Baada ya Damian kurudi amelewa Siku Hiyo!.
Basi miezi kama miwili ilipita maisha Ya Damian yalianza kuwa magumu, pia Huku kwa Mr Jailo nako Hali ilianza kuteteleka, maana Damian Ndo alikuwa Mtu anaye wafanya waende chooni kwa pesa ambazo alikuwa anawapatia!.
Na ni kama mwezi ulikuwa umesalia tu Damian atimuliwe pale kwenye nyumba anazo kaa, maana nyumba zilikuwa za kampuni na alikuwa kapewa miezi kadhaa awe ameondoka.
Kama Bahati tu Siku Hiyo Damian akiwa Hana hili wala lile Huku mfukoni kukiwa kunanuka tu vumbi!, gafla alipokea Namba Mpya kwenye Simu Yake, na zilikuwa taarifa njema kwamba kesho Yake aende kazini!.
Aisee Bwana Damian aliruka kama masai kapandisha mori.
Ni kweli Kesho Yake asubuhi na mapema Damian alifika kazini, bwana Huyo alipewa Gari Ya ofisi, alikabidhiwa funguo ya ofisi maana pale kwenye kampuni alikuwa kwenye kitengo kama afisa masoko!!.
Pia ile notisi ya kuhama kwenye nyumba ya kampuni ambayo alikuwa kapewa iliondolewa, kwa Maana hiyo alirudishwa rasmi kazini!.
Siyo Damian tu ambaye alifurahi, mpaka familia nzima ya Mr Jailo nayo ilifurahi, Nuru naye ilikuwa mwendo Wa kukenua tu Japo alikuwa na mpango Wa kumuacha Damian!.
"Uuuuu aisee ningeumbuka vibaya!! Yaani ilibaki kiduchu nimkache Huyu boya sijui ningeweka wapi Sura Yangu, Bora nilikuwa na kauvumilivu Japo kidogo!"Hayo Ndo Mambo ambayo Nuru alikuwa anajiwazia Baada ya Damian kurudishwa kazini.
Bwana Jovin alipata taarifa kwamba Damian karudishwa kazini!.
"Shiiiitiiii nani Huyo kamrudisha Yule mpuuzi kazini, inamana Mr Antonio Kaanza kunipuuzia Siyo!" Kwa hasira Damian alijiongelesha Baada ya zile taarifa!.
Pale pale Jovin alichukua Simu na kumpigia meneja Wa Kampuni ambaye anaitwa Mr Antonio, lakini Simu ya Meneja Huyo iliita pasina kupokelewa, Mwishowe ilianza kukatwa na hatimaye kuzimwa kabisa!.
Kwa hasira Jovin aliona inatosha kama ni kuwajua wanafiki kashawajua, aliondoka pale kwake mpaka kwenye kampuni!, kwanza kufika getini tu aliambiwa kuna maagizo kwamba hatakiwi kuingia!.
Ilikuwa kitu cha maajabu kwa bwana Jovin kampuni Yake alafu anaambiwa asiingie, Bwana Huyo ilibidi aanze kutumia Nguvu lakini aliishia kupigwa virungu kama Siyo Yeye!.
"Ebu niitieni meneja Wa hii kampuni haraka Sana, lasivyo Wote mtafutwa kazi!" Yalikuwa maneno ya Jovin ambayo yalifanya Wengi walio yasikia wabaki wanacheka!.
Pale kwenye kampuni ni Meneja pekee Yake ambaye alikuwa anajua ukweli Wa mambo!.
Ni kweli walimtendea Haki taarifa zilipelekwa kwa meneja kwamba Jovin anataka kumuona lakini meneja Huyo alisema hana Muda mchafu Wa kuchezea na aliamuru wamtimue tena kwa kipigo!.
Na kweli walinzi walitendea Haki agizo la Boss, Jovin alipigwa kipigo cha mbwa mwizi na kutimuliwa kama mwizi, Muda huo huo Jovin aliliona Gari la kifahari huku ndani ya Gari akiwamo Mr Tamir linaingia pale getini!.
Jovin alijaribu kusimamisha lile Gari na kumuita tajiri yule kwa Majina Yote, lakini tajiri yule Wa kihindi alishusha vioo vya Gari na kuchungulia Mara Moja kisha alivipandisha tena!.
"Heeeee hii imekuwaje tena!? Mbona kama naota!?" Jovin akiwa anaugulia maumivu alijiuliza swali ambalo hata hivyo hakupata majibu ya haraka haraka!.
Je imekuwaje tena? Ndo Mambo yameharibika kweli au kuna Siri ipo nyuma ya pazia!? Kutoka kwenye kuigiza umasikini, Sasa ni kama umasikini kweli unaanza kumnyemelea Bwana Jovin itakuwaje!???
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni