Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo
Gonga94 · Stories
09 Dec 2025
129 views
VYOTE NDANI GONGA94
Sophia (Urvashi Sharma) binti anayeendesha maisha yake Goa
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Sophia (Urvashi Sharma) binti anayeendesha maisha yake Goa alifuatiliwa na kushambuliwa na mbakaji aliyeitwa Rakesh. Baadaye anaamua kuhamisha makazi yake Dubai anapanga nyumba ya tajiri aliyeitwa Karan Oberoi (Bobby Deol). Miezi sita baadaye Karan anafikisha ombi la kutaka kumuoa na binti analikubali.
Muda mfupi kabla ya ndoa Sophia anakutana na mwigizaji anayejitafuta anayeitwa Vikram 'Vicky' Malhotra (Akshay Khanna) anavutiwa naye sana ila anaamua kuendelea na mpango wake wa ndoa. ila alikuja kubadilika akiwa madhabauni alipoamua kumkataa Karan na kumdhalilisha vibaya kisha akaenda zake kwa Vicky. Jambo lile lilipelekea Karan kuumia na kuchukua uamuzi wa kujiua.
Sophia alipokuja kujua alijuta sana na alijiona wazi yeye ndiyo chanzo cha kifo chake. Baadaye inakuja kujulikana Vicky ndiyo chanzo, Alipewa nafasi na mwongoza filamu aliyeitwa Rohit Shroff, akitakiwa kuigiza filamu ya kuhusu maisha yake. Akatakiwa aingie kwenye maisha ya Sophia. Binti aliwaka sana na kumwambia ampigie huyo Rohit aje hapo muda huo, naye akatii na kumpigia kumwita. Bwana wee Rohit anawasili hapo na inajulikana kumbe yule Karan ni Rohit na hakufa.
Inakuja kujulikana kumbe Karan au Rohit alitaka kupiga pesa akaamua kutengeneza filamh kuhusu maisha ya Sophia na akamwajiri Vicky aingie kwenye maisha yake wawe wapenzi. Baadaye akaja kuunda tukio feki la kifo chake likiwa ni sehemu ya filamu na si kweli.
Kibaya zaidi Sophia kuna siku alipewa karatasi asaini akajua nu mambo yao ya ndoa, kumbe alisainishwa mkataba wa filamh hawezi kushtaki kwani kuna saini yake. Humo ndani walipoishi aliwafungia kamera, karekodi kila kitu wakibanjuka. Akawatishia watulie kama hawataki video zao zivuje mitandaoni wawe mastaa wa filamu ya ngono. Wakaishia kuwa wapole waache filamu itoke.
Miezi mitatu baadaye filamu ikazinduliwa, Karan alipanga siku hiyo ya uzinduzi kuwepo na tukio bandia la yeye kupigwa risasi kuongeza mvuto zaidi. Basi watu wawili katika kundi la utayarishaji wakaamua kuwajaza upepo Vicky na Sophia wasikubali aliwatumia. Wakachukua bastola zilizoandaliwa kwa ajili ya tukio wakamtungua Karan.
Kumbe bunduki zina risasi halisi si bandia Karan akaumizwa vibaya na baadaye alijeruhiwa vibaya akapelekwa hospitali. Janga lote likawa kwa watayarishaji tukio lile, huku Vicky akiachiwa kuonekana hana kosa lolote. Akaenda hospitali alipopelekwa Karana akamkuta Sophia ambaye alimpa habari ya kufariki Karan.
Kumbe aliyebadilisha zile bastola kusudi ni Sophia na mpango waliufanya na Karan, ushahidi ukawaangukia wale ambao walichochoea wakafungwa. Sophia akachukua mali za Karan, Vicky akawa mwigizaji maarufu kwani hiyo filamu iliweka rekodi yake sokoni..
Ni NAQAAB yaani KINYAGO, Bobby alipoamua kufanya mchezo mchafu maisha ya watu. Matokeo filamu iliuza na hakunufaika na chochote.
#Mambosreview
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
NINI KITATOKEA ENDAPO FAR RABAT ATAFUNGWA NA YANGA ATASHINDA MCHEZO WA MWISHO? MAANA YAKE WATALINGANA ALAMA
. Kwa mujibu wa kanuni za CAF yafuatayo yatatazamwa kwa hatua. 1- Aliyekusanya alama nyingi kutoka kwa mwenzake walipoku...
Je wajua filamu ya Deadly Prey ya mwaka 1987 ilitayarishwa na David Trior ambaye alimpa nafasi ndugu yake Ted Prior kucheza uhusika mkuu(main character)
filamu iliyotengenezwa kwa bajeti ya chini sanaa kiasi mwanzo mwisho wa filamu jamaa alikuwa na kipensi tuu vibanda umiz...
Mwandishi aliuliza je neno mshangazi maana yake nini, Kajala akajibu mshangazi ni mwanamke mwenye umbo kuuubwa, Wolper akisema mshangazi ni mwanamke mwenye umri
mkubwa kama sisi hapa yani kama mimi, Kajala, Auntyezekiel na Irene Uwoya Irene Uwoya akasema hapana sisi sio mishangaz...
*DAKTARI WA JESHI SI UNGENIOMBA TUU* *1-5* Kuna wakati kwenye maisha hatuwezi kabisa kuamua hatma zetu, nadhan ni kwa sababu huwa hatujui maisha yetu yamebebwa na nini... Umaskin, shida na tabu za maisha huwa ni funzo kubwa sana kwetu, na kwa baadhi yet
ndio njia ya kutuongezea juhudi katika upambanaji wetu... Naitwa alice ndio jina ambalo nimepewa na wazaz wangu, nimeza...
Sophia (Urvashi Sharma) binti anayeendesha maisha yake Goa
Sophia (Urvashi Sharma) binti anayeendesha maisha yake Goa alifuatiliwa na kushambuliwa na mbakaji aliyeitwa Rakesh. Baadaye anaamua kuhamisha makazi yake Dubai anapanga nyumba ya tajiri aliyeitwa Karan Oberoi (Bobby Deol). Miezi sita baadaye Karan anafikisha ombi la kutaka kumuoa na binti analikubali.
Muda mfupi kabla ya ndoa Sophia anakutana na mwigizaji anayejitafuta anayeitwa Vikram 'Vicky' Malhotra (Akshay Khanna) anavutiwa naye sana ila anaamua kuendelea na mpango wake wa ndoa. ila alikuja kubadilika akiwa madhabauni alipoamua kumkataa Karan na kumdhalilisha vibaya kisha akaenda zake kwa Vicky. Jambo lile lilipelekea Karan kuumia na kuchukua uamuzi wa kujiua. ...
👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/sophia-urvashi-sharma-binti-anayeendesha-maisha-yake-goa