FATE TO LOVE YOU π 13 MTUNZI UHURU MEDIA Ule usiku Jerry aliamua kutoka nyumbani kwake na kwenda kuonana na rafiki yake kipenzi Nabir. Walikaa na kuanza
" Hivi leo upo sawa kweli? Nabir alimuuliza.
" Kwakweli simba dume nimeshikika, sina ujanja .
" Unamaana gani kusema hivyo?
" Nabir ninezama penzi ni lakini sijui najiweka vipi kwenye hili penzi na mbaya zaidi kuna kitoto kimoja naona kinaniingilia .
Nabir Kumuangalia Jerry huku akicheka sana.
" pole sana rafiki yangu , udhaifu wako naujua huwezi kubembeleza wala kutongoza, sijui huyo msichana utaanzia wapi kumvuta kwako.
" Tayari yupo karibu na mimi ila kumueleza hisia zangu ndio bado.
" Ni nani huyo?
" Yule binti aliekuwa anafanya kazi kwa Maxwell.
" Si uliniambia ana uhusiano na mtoto wa Maxwell?
" Ndio lakini sasa ni chuo na paka , Lina aliacha kazi na sasa yupo kwangu.
" Yupo kwako kivipi?
" Nimemuweka kama pambo la nyumba yangu, nikimuona anazunguka zunguka pale ndani basi moyo wangu burudani.
" Wakati huo mwenyewe hajui kama ni pambo.
" Hajui kabisaaa...
" ππππ Jerry acha usoni zege ukichelewa yule loverboy atamvutia kwake.
" Sitakubali ila kuna mambo nitafanya ili kumvutia kwangu , sitaki kumwambia kwa maneno bali nataka Lina atambue kwa vitendo kuwa nampenda na hakuna mwanaume anayempenda zaidi yangu.
Siku zilienda Jerry alijaribu kumfanya lina kama rafiki, walikaa pamoja na kuongea huku wakibadilishana mawazo, walitoka matembezi pamoja hata kumfanyia shopping ya nguo, viatu na vitu vingine vya kike na kila mara alikuwa akimpa pesa kwaajili ya matumizi.
Kwa muda mfupi lina alizidi kunawili alipendeza na kuonekana tofauti na yule wa mwanzo aliekuwa akihangaika jikoni na kufokewa ovyo.
Siku moja asubuhi Jerry alikuwa kwenye chumba cha ofisi yake akifanya kazi zake za kiofisi. Mara kuna ujumbe uliingia kwenye barua pepe yake . Alipofungua na kusoma aliachia tabasamu.
Pale pale alichukua simu yake ya mkononi na kumpigia Lina.
" Lina njoo ofisini kwangu.
" Sawa.
Lina alikuwa amekaa kitandani kwake alishuka na kuelekea kwenye chumba cha ofisi, aligonga na Jerry akaitiiia.
" Karibu .
Lina alifungua mlango akaingia ndani.
" Habari za asubuhi Boss.
" Salama. Lakini itakuwaje kama ukinikuta jina langu yani Jerry, double J au J?
" Kama ukipenda basi nitafanya hivyo.
" Napenda sasa kazi kwako.
" Sawa J. Alijibu Lina na wote wakacheka.
" Lina kuna habari nzuri zimelifikia mapema hii.
" Habari gani?
" Maombi iliyotuma kwaajili ya kujiunga na chuo yamekubaliwa.
" Waoooo. J sikutegemea kama utakuwa makini hivi na hili jambo .
" Ilikuwa lazima nipambane.
" Jamani sijui nianzie wapi kushukuru , umenipa nafasi ya pili ambayo siku wahi kuifikiria . Aliongea Lina huku machozi yakishuka mashavuni kwake.
Jerry alizunguka upande wa pili wa meza , alitoa kitambaa na kumfuta machozi.
" Usilie, wewe ni jasiri sana , natamani ufikie lengo lako.
Aliongea Jerry huku akishika kiganja cha Lina na kukipapasa. Mara Kuna alihisi joto la tofauti likipenya kwenye mwili wake, alinyanyua macho yake kumuangalia usoni , hapo alihisi kuwa Jerry ni mwanaume salama kwake na ni mwanaume ambae anajua maana ya utu pia alihisi kuna chembechembe ya upendo.
" Jerry.... Lina aliita
" Naaam.. Jerry aliitikia kwa sauti nzito.
" Asante kwa kuitambua thamani yangu.
Baada ya maongezi lina alitoka ofisini , Jerry aliachia tabasamu.
" Bila shaka mtoto kashaanza kunielewa jicho alimuangalia na sauti yake vinanioa matumaini makubwa sana.
Ilipofika usiku Lina akiwa chumbani kwake hakupata usingizi mapema, kila alipojaribu kufumba macho alivuta kumbukumbu ya sura ya Jerry. Alianza kukumbuka matukio mbalimbali ya Jerry, pia alikumbuka siku ya kwanza walipokutana na Jerry wakampiga busu.
Alikuwa akitabasamu kila mara na kujisemea.
" Jerry wewe ndio mwanaume unaweza kubadilisha kila kitu kwenye maisha yangu. Lakini moyo wangu upo tayari kuanza safari mpya ya mapenzi baada ya maumivu ya nyuma?
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi