FATE TO LOVE YOU π 6 MTUNZI UHURU MEDIA Lina alishuka kwenye gari na kuelekea kwenye lango kuu la hotel anasalimiana na mlinzi kisha akampatia
Mlinzi akipokea na kuangalia jina.
" Nenda ghorofa ya pili chumba namba 56.
Alisema mlinzi huku akiwa anamrudishia Lina ile kadi.
Lina aliingia ndani alikuwa hajui aanzie wapi mpaka afike ghorofa ya pili. Mara alifika muhudumu mmoja akiwa na tabasamu mwanana usoni kwake.
"Habari mrembo.
" Salama.
" Naweza kukusaidia?
" Ndio nahitaji kufika ghorofa ya pili chumba namba 56.
" Sawa nifuate tafadhali.
Lina alimfuata yule muhudumu mpaka kwenye lift . Lift ilianza kupanda mpaka ilipofika ghorofa ya pili ilisimama mlango ukafungwa wakatoka na kuelekea chumba ni 56.
" Hiki ndio chumba namba 56.
" Asante .
" Unakaribishwa.
Yule muhudumu aliondoka , lina alisimama mlangoni akiwa anajushauri kugonga mlango. Baada ya kunifikiria alinyanyua mpango na kutaka kugonga lakini ghafla alishitukia ameshika mkono.....
Lina alishituka na kugeuka haraka kumuangalia aliemshika mkono akakutana na sura ya mwanaume ambae hakuwa anamjua.
Waliangaliana usoni ,lina alikuwa huenda huyo mwanaume ndio Jovin.
" Mr Jovin?
" Hapana unatakiwa kunifuata huku.
" Wapi? Mimi niliambiwa natakiwa kuingia namba 56.
" Msisikilize mimi madam.
Lina hakutaka kuendelea kubisha alimfuata nlyule mwanaume mpaka ghorofa ya tatu wakaingia kwenye chumba kimoja ambacho kilikuwa na mwanga hafifu oakini kilikuwa na muonekano mzuri mno.
Kwa mbali alimuona mwanaume mmoja akiwa amekaa kwenye kiti.
" Karibu miss Lina.
Lina alipiga hatua ndogo huku akiwa na uwoga mkubwa mpaka akafika karibu na huyo mwanaume, lina alikata macho yake kumuangalia lakini hakuwa amemtambua.
Yule mwanaume alinyanyuka na kumsogelea, alimzunguka wakati huo Lina alikuwa anatetea kwa hofu.
" Wewe ndio Mr Jovin?
" Hapana. Lina alishituka
" Kama sio mr Jovin wewe ni nani?
Yule mwanaume alikuwa ameshika kitu kama limot akabonyeza na taa za mwanga zikiwaka hapo ndipo Lina alipoiona sura yake na kumtambua kuwa ni Jerryson.
" Wewe .....
" Ndio ni mimi yule yule Jerryson.
Lina alikuwa haelewi imekuwaje kuwaje mpaka Mishely aliamua kumkutanisha na huyu mtu.
" Wewe ndio nilipaswa kuonana na wewe?
" Hapana sio mimi ila sipendi wewe ukutani na mwanaume ambae anataka kukutumia kama chombo cha starehe.
Lina aliona aibu akainama chini kisha akauliza.
" Kwanini?
" Kwasababu kustahili hutakiwi kupitia haya.
Lina alizidi kuona aibu , Jerry aliushika mkono wake na kwenda kukaa nae kwenye sofa.
" Nahitaji tuongee kama marafiki uniambie shida yako kubwa ni ipi mpaka ukaamua kujitoa sadaka kiasi hiki.
" Kwani wewe umefuata nini hapa?
" Achana na mambo yangu nataka kujua yako kwanza.
Lina aliona aibu kusema shida zake kwa mwanaume ambae hakumkuta vizuri .
" Lina naelewa umeondika nyumbani kwa kina Stephen niambie unataka nini kutoka kwangu ili niweze kukusaidia.
Lina bado alikuwa kimnya.
" Sitaki ufanye kazi ya kuuza mwili wako kwaajili ya kufanya maisha yako yaende.
" Sijui nahitaji nini maana hata nikisema pesa basi hakuna mtu wa kunipa pesa ambayo itanitosheleza , muhimu ni mimi kufanya kazi , kupambana kupata pesa ambayo itatokana na jasho langu hata kama ni kazi ...... Lina hakumaliza kuongea lakini Jerry akawa ameshamuelewa.
" Kazi ya kujiuza si ndio?
Lina alikaa kimnya, Jerry akaendelea kusema.
" Kama unataka hivyo basi naweza kuwa mteja wako nitakununua kila utakapokuwa tayari kufanya biashara. Au kama utataka nikupe kazi basi unanitafuta kwa hii namba.
Jerry alitoa kadi yenye namba zake za simu na kumpatia. Pia alitoa kiasi cha pesa na kumpatia.
" Hizi zitakusogeza siku mbili hizi ukiwa bado unajishsiri.
Kwakuwa lina alikuwa anashinda alichukua kile kibanda cha pesa na kuweka kwenye pochi yake.
" Hakikisha jibu utakalopata unanijulisha.
" Asante . Lina alishukuru kisha akanyanyuka na kuondoka. Huku Jerry akimuangalia kwa makini kama vile anahesabu hatua anazopiga
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi