GENERAL SILI SILALI JUU YAKO Niliwatizama waliniona ila walinipotezea kabisa kisha General aliinuka na kuondoka wale wasichana wambea wakaanza kusema:
WhatsApp 0742133100
SEHEMU YA 07.
Niliwatizama waliniona ila walinipotezea kabisa kisha General aliinuka na kuondoka wale wasichana wambea wakaanza kusema:
"Nancy anabahati sana jamani General anampenda kilamsichana hapa kambini anatamani kupata nafasi ya kuwa na gentleman kama General kiukweli Nancy anaraha sana"
Nilijikuta naumia mno na nachanganyikiwa kusikia maneno kama hayo, nikainuka kwa hasira na kuanza kuelekea bwenini Nancy alinikimbilia na kuniita:
"Laura!.... samahani"
Nilijifanya sijamsikia kabisa ndio kwanza niliongeza mwendo, na kuwahi bwenini kwetu nilipofika nilipanda kitandani na kujifunika shuka langu, alikuja moja kwa moja Nancy hadi bwenini na kuja nilipokuwa nimelala, akaanza kuniambia:
"Laura ndio nini nakusemesha umenikimbia, mbona sikuelewi umefika sasahivi tuu na usingizi tayari umeupata, tafadhali nisikilize basi, hembu inuka nikuambie"
Sikuinuka hata niliendelea kulala, na wala sikumjibu kitu nilikuwa kimya, mwisho alichoka na kuamua kuondoka zake, kiukweli nilijikuta ninamuonea wivu roho inaniuma sana, hasa yale maneno ya wale wambea yaliniuma, nilipohisi ukimya nikafumbua macho na kumtiza, alikuwa hayupo kweli bweni zima, ndio nikajilaza vizuri kitandani kwangu na kupitiwa usingizi, wiki moja ilisonga na mimi na General hatukuwa sawa, yaani kilammoja alikuwa kivyake, na maranyingi General alikuwa bize akifanya kazi ofisini kwake, kuonekana kwake ilikuwa marachache sana mudamwingi alikuwa bize, siku moja nikiwa natoka kula kantini naelekea bwenini, alikuja General na kunishika mkono wangu kwanguvu, alinipeleka moja kwa moja pembezoni mwa ukuta, na kuniegemesha ukutani kisha alinikiss romance kwa nguvu , huwezi amini nilijikuta nalegea kabisa kwanza nimemmis hatari, nilihisi utulivu wa moyo kuwa kifuani kwake, mala baada ya fahamu kunirudia nilimsukuma pembeni na kutaka kukimbia, alinivuta tena mkono na kisha akaniambia:
"Utakimbia hadi lini nijue eeh!, huoni kuwa unaupinga ukweli wako mwenyewe Laura, na kujua vizuri na hata hujifichi unanipenda unanipenda sana Laura"
"Nini? Nani kakudanganya eeh! Nakuuliza wewe hahahaa, kwataarifa yako sina hata hisia nawewe wala sitarajii naona unajiogopea tuu mwenyewe, pole sana kwahilo na utuuzima wako nitakupeleka wapi mie"
Wakati naongea hayo yoote General alikuwa kimya tuu akinitizam, kisha nilipomaliza nikaanza kuondokazangu, ile natoa mguu tuu alinivuta tena, nahivi nilivyo chaupepo sasa, kisha akanidaka na kuniweka tena karibu yake, mithiri kama anataka kuninyonya shingo yangu hiviii, alinikumbatia vizuri sana karibu yake nilijikuta mapigo ya moyo yananienda mbio, nilitulia sana nilikuwa tayari kwachochote kile, yaani kisha General akiwa amenimaliza kabisa hapo kwa manjonjo yake ya kimahaba, hapo aliniambia kwa sauti yachini akiwa anafanya kama anataka kuninyonya shingo:
"Samahani Laura nilikuwa nakuaga naondoka keho alfajiri, ninasafari ya nje ya nchi, na samahani kwa usumbufu wangu"
Nikashtuka hapo na kujichomoa mikononi mwa General taratibu, kisha nilimjibu:
"Ok sawa safari njema"
Na baada ya hapo nikaanza kuondoka kuelekea bwenini, General akaniambia:
"Nakutakia mazoezi mema sidhani kama nitakukuta, kwani sirudi hivi karibuni"
Nilisimama nikasikiliza kwa umakini, kisha nilimjibu:
"Kwani Nancy nae umemuaga, maana ndio mtu sahihi wakumuaga"
Alitabasam kidogo General, nakisha akanijibu:
"Ndio kakuambia eeh basi sawa nitamuaga, usiku mwema sasa by"
General aliondoka na kwenda kwenye chumba chake, niondoka kwenda bwenini nikiwa mithili ya mtu kawekwa zege miguuni, ila nilijipa ujasiri na kujiambia hawezi kuniacha ananipenda pia, nilifika bweni nikaingia na kupanda kitandani tayari kulala, nililala kwatabu sana kwani nilikuwa nawaza hadi kulikucha alfajiri, tuliamka na kwenda mazoezini kama kawaida, ila akilini nilikuwa na mtafuta General tuu nimuone nijihakikishie kama yupo, lakini wapi sikumuona hadi muda ulienda siku iliisha sikamuona labisa, mwisho nilikata tamaa kabisa kwani siku zilienda mwezi ulikata General Ethane hakurudi kabini kwetu, nilianza kuwa na udhuni sikuwa naraha kabini, nilikuwa nafanya sana mazoezi hata muda wakula sikuwa naenda kula, niliona hakuna maana yakula ikiwa nimpendae hata hajali kuhusu mimi, nilitamani arudi hata dakika moja tuu nimuambie jinsi ninavyo jisikia juu yake, lakini haikuwezekana kwa muda huo, ilifikia hatua usiku nilikuwa nagara gara tuu sipati hata usingizi tena, kisha nikizidiwa na hisia naanza kulia pekeangu, nilikonda na nilikuwa sina raha kabisa, hadi siku moja mkuu wa kikosi changu namba saba aliniita ofisini kwake, akaniuliza:
"Unatatizo gani Laura, maana sikuhizi nakuona haupo sawa kabisa"
"Mkuu mbona sina shida nipo sawa mimi"
"Nakujua tangu unaingia kambini hadi leo hii, nimeambiwa nawenzio chukula huli, na mala nyingi umekuwa mnyonge sana kunamuda unalia pekeako, niambie tatizo nini?
"Mkuu mimi sina tatizo, na hao walikudanganya mimi niko sawa kabisa"
Wakati tunaongea hayo na mkuu wangu wakikosi, gafla simu iliita tukiwa wote nisimu ya mezani, mkuu wangu akaniambia:
"Samahani napokea simu maramoja tulia hapa hapa"
Kisha akaipokea hiyo simu
"Hallow"
"Hallow General hapa naongea"
Gafla mkuu wa kikos alipiga sarut huku akisema:
"Heshima yako mkuu General"
Nilishtuka nikainuka huku nikiwa naitazama simu
Je nini kitatokea hapo .............
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi