MR GENERAL : KUMBE ULINIPENDA EEE SEHEMU YA 18
“Ehee, nikataka kujua zaidi mwamba wngu alikuja na swaga gani…
Aisee alikuwa analalamika kila siku, akawa anakuja ananiambia kuwa akilala mwenyewe anakuona, na anateseka sana, ila ubaya ulishaapa kuwa hautakaa uolewe na mjeda, hilo neno lilikuwa linamchanganya sana, ila ukweli ni kuwa bro anakupenda sana, akaendelea kusema mdogo wake…
“Sasa ilikuwaje mpaka baba yake akakubali kumsaidia, mpaka nikajua kuwa naolewa na mzee? Ikabidi na mimi niulize sasa…
“Nadhan alivyokuwa analalamika sana mzee atakuwa anamuonea huruma akaamua kujivisha mabomu, na kingine mzee yupo karibu sana na bro kuliko mimi, si unaona wameshachukuana wanaenda kupanga mipango yao, huenda hata vitu vingine watakuwa wameongea ndio maana mzee akaamua kubeba majukum, ila nisikudanganye, sijawah kumuona bro amevurugwa kama kipindi ambacho alianza kukupenda wewe, naomba mpende sana aiseee maana utakuja kumtoa roho…
Nikatabasamu kisha nikasema “Nitahakikisha hata nikimtoa roho, namtoa roho ya chuki abaki akinipenda mimi tu, akatabasamu kisha akasema “Kwa maneno hayo ni kheri achanganyikiwe…
Nikaanza kucheka
“Mnacheka cheka nini hapo? Tukasikia sauti nyuma yetu ikabidi tugeuke na shemu akawah na kusema “Kuwa na amani bro sikuibii, kisha akaondoka zake…
“Ulikuwa unaongea nini na dogo? Akauliza…
“Ni mambo yetu tu, twende tukapumzike, nikasema, akanishika mkono tukaenda mezan tukala, ilikuwa ni familia yenye upendo sana, mpaka mimi mwenyewe nilikuwa nafurahia sana kuwa karibu nao, baada ya hapo tukaenda chumban kulala, na kulipopambazuka, niliona namna ambavyo walikuwa na ushirikiano ile familia, kila mtu ameamka mapema na bila kuwaza kuwa ameshika kazi gani, yaan mimi ni mkamwana na ndio mtoto wa kike, naamka nakuta kila kitu kimefanywa, niliona aibu, ila mume wangu alikuja na kunishika mkono na kunambia “Usijisikie vibaya najua ulitaman na wewe kufanya kazi ila bado wewe ni bikra wetu, ndio nimekutoa ubikra mara ya kwanza kwa kukuleta kwetu, ukishakuwa mzoefu utafanya kazi, nikatabasamu…
Basi nikaoga kisha tukanywa chai, na baada ya hapo tukarudi nyumban na mume wangu akaitwa kazin, hakuwa anapatikana kwa karibu mwezi mzima, sijui hata hizi kazi za jeshi na kutopatikana kunakuwaga na muingiliano gani…
Sasa wakati anarudi nilikuwa siku vizuri kiafya, nilikuwa kila siku asubuh natapika na sikuwa najua ni kwanini, nilikuwa naogopa hata kwenda hospital sijui hata nilikuwa nawaza nini…
Basi aliporudi akanikuta nimedhoofu akaniangalia na kunambia “Shida nini mamaa…
“Wiki ya pili sasa natapika kila siku asubuh na sijui nina shida gani, nikashangaa mwamba kanibeba kisha akawa anashangilia, hakutaka hata nijiandae, nikashangaa tunaenda hospital akawa anasema “Mpimeni mimba huyu…
Na kwakuwa alikuwa na magwanda yake ya kijeshi, vipimo vilikuwa ni haraka haraka sana, kweli nikapimwa mimba na ninakutwa na ujauzito wa mwezi mmoja, aiseee nilishangaa mume wangu kanikumbatia kwa nguvu mpaka chozi likamtoka, na baada ya hapo akanambia “Mke wangu, sikuwah kufikiria kama utakuwa tayar kubeba mtoto wangu, na kuahidi kwa moyo na kauli zangu, nitapambana sana wewe na mtoto wetu muishi maisha mazuri sana…
Nikatabasamu tu pale, basi hao tukarudi nyumban, alikuwa ananilea vizuri sana, mpaka nikawa najihisi mwenye bahati sana, baada ya mateso ya muda mrefu ambayo nilikuwa nayapata kwa shangazi, sasa hatimae na mimi nimepata faraja, eee Mungu wangu nijalie na mimi niwe na furaha na amani kwenye maisha yangu, hio ndio ilikuwa dua yangu ya kila siku…
Basi kweli kama tunavyojua siku hazisimami , miezi tisa ilipita ingawa ilikuwa ni kwa tabu sana, maana huwa naumwa umwa sana ….
Hatimae siku ikafika nikajifungua mtoto wa kike, kama dua zangu zilijibiwa vile, maana alikuwa anafananana na mimi lakin alikuwa na rangi ya baba yake…
Basi maisha yakaenda, familia yake ni familia ya upendo sana, siku moja shangazi ananipigia ananiambia kuwa “Yule mzee amekuja kudai mahari zake bila kujua ndio mkwe wangu…
ITAENDELEA ….
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi