VYOTE NDANI GONGA94
NILIZAA NA BOSI KWA BAHATI MBAYA SEHEMU YA 05
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Aliponivuta karibu na kifua chake, nilihisi pumzi ikinikatika.
Moyo wangu ulipiga kwa kasi isiyoelezeka, nikawa nahema huku nikimtazama usoni.
Alikuwa ametulia sana, kana kwamba hakujali kabisa macho yote yaliyokuwa yanatuangalia.
“Bosi…” nilisema kwa sauti ya chini, “watu wanatuangalia.”
Akanitazama kwa makini, macho yake yakiwa makali lakini tulivu.
“Waache waangalie,” alisema, “maisha ni yako, si yao.”
Maneno yale yalinifanya nihisi nguvu fulani ndani yangu, lakini wakati huohuo woga ulinizidi. Nilikuwa mfanyakazi mpya, mwanamke maskini, na yeye alikuwa bosi mwenye heshima, mwenye mamlaka.
Aliniachia mkono taratibu.
“Nenda ofisini kwako. Usichelewe kazi,” alisema kwa sauti ya amri lakini yenye upole.
Nikatikisa kichwa, nikageuka haraka na kuingia ndani ya jengo.
Lakini kila nilipopiga hatua, nilihisi macho ya wafanyakazi yananichoma mgongoni.
Siku hiyo kazini sikufanya kazi kwa umakini.
Kila nikiandika, mawazo yangu yalirudi:
Mkono wake kiunoni
Maneno yake
Namna alivyoniangalia
Na zaidi ya yote, nguo nilizovaa.
Nilijiuliza:
Kama yeye ni bachelor… hizi nguo zilikuwa za nani?
Hakuna aliyeniuliza chochote moja kwa moja, lakini nilihisi uvumi unaanza kuota. Tabasamu za pembeni, kunong’ona, macho ya wivu hasa kutoka kwa wanawake.
Jioni ilipofika, nilikuwa nimechoka kiakili kuliko kimwili.
Simu yangu ikatetemeka.
Ujumbe mpya:
“Radhia, before you leave, come to my office.”
Nilisita.
Nilijua kabisa, nikikanyaga pale tena, kuna kitu kingebadilika kabisa ndani yangu ama kwa kazi yangu, ama kwa maisha yangu yote.
Nikavuta pumzi ndefu.
Nikainuka.
Nikapiga hodi.
“Ingia,” sauti yake ilisikika ndani.
Niliingia akaanza kunipa makazi mara beba faili hili peleka huku lile peleka kule yaani ofisini mulebilikuwa kivumbi na jasho .Mwishowe akaniambia kuwa nimsaidie kujaza baadhi ya document zote za muhimu....
Basi nilfanya kazi hiyo nikiwa nimekaa ofisini kwake Wafanyakazi wengine waliniangalia kwa jicho baya na siku chache nishalala nyumbani kwa bosi ,kanibeba kwenye gari lake wakati wengine ni mwendo wa daradara tu ....Nilianza kuhisi haja ndogo imenibana ....
Nilitoka kuelekea uwani nikiwa bado na mawazo mengi kichwani.
Kila hatua niliyopiga ilionekana nzito kuliko kawaida, kana kwamba ardhi ilikuwa inanivuta nyuma.
Nilipofika karibu na bustani ndogo ya kampuni, nilisikia sauti za kunong’ona.
Nilisimama ghafla.
“Unamjua huyu Radhia?”
“Anajifanya mpole, kumbe ni malaya wa kutupwa ”
“Ndiyo maana bosi kadata vile siku chache tu kapewa nguo ,kalala nyumbani kwa bosi na anapanda gari la bosi.”
“Acha tu, tutamfundisha adabu. Ujuwe nimefanya kazi miaka mingi sijuwi hata gari la bosi ndani likoje”
Maneno yale yalinikata kama kisu.
Nilihisi tumbo likiuma, mikono ikatetemeka. Nilijaribu kuendelea kutembea kana kwamba sikusikia chochote, lakini miguu ilikataa kunitii.
“Huyu msichana hatadumu hapa,kuna mambo tutamfanyia afukuzwe kazi hiki ni kirusi hapa”
mmoja wao alisema kwa sauti ya uhakika.
“Tutahakikisha anajilaumu mwenyewe.”
Machozi yalinijaa, lakini sikutaka yalionekane.
Nilijifunza tangu nikiwa mdogo kulia mbele ya watu ni kuwapa ushindi.
Nilitembea haraka kuelekea upande wa nyuma wa jengo, nikatafuta sehemu ya kujisitiri. Nilikaa kwenye benchi la saruji, nikavuta pumzi ndefu mara kadhaa.
“Nimekosea wapi?”
“Ni kwa sababu ya nguo?”
“Au kwa sababu tu mimi ni maskini?”
Nilifanya kilichonipeleka kule nikarudi na kumkuta bosi kakaa machoni nilikuwa na chembe chembe za machozi .Aliniuliza nilichokuwa nalilia lakini sikumjibu.
Ghafla alinivuta na kunipakata then taratibu akawa anayafuta machozi yangu
" Sipendi kuliona chozi lako likimwagika "huku ananitazama
ITAENDELEA.......
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi nilizaa-na-bosi-kwa-bahati-mbaya-sehemu-ya