UTANIITA SHEMEJI* SEHEMU YA 10
SONGA NAYO.................
Kauli ya ole wako uinuke na inuka zilikuwa nyingi hadi nikahisi kuchanganyikiwa ikawa ni mwendo wa simama kaa kama mtoto wachekechea .
Mwisho Aunt Vero aliingilia kati na kusema " Dada!! Alvin yuko sahihi ,muache mtoto wawatu "
Kauli ya aunt Vero ilimfanya madam akaachana na Alvin na kuhamia kwake, kwa hasira akamuuliza " Vero unasemaje!! Ina maana unamuunga mkono huyu mpuuzi?"
"Sio kwamba namuunga mkono , sikia shoga angu Wardah bado ni mdogo mno hastahili kukaa kwenye nafasi unayotaka kumueweka "
"Eti mdogo anaudogo gani huyu ,na kwanza yeye kuwa mdogo au mkubwa vinanihusu nini mimi? .
Embu acheni upumbavu wenu basi na sitaki kuingiliwa kwenye maamuzi yangu tafadhali "
Alvin alitaka kuongea aunt Vero akamwambia "Alvin subiri kwanza ✋️, mama Shuu hili swala halihitaji maamuzi ni wewe kutii huwezi kutaka kumharibu mtoto wawatu na tukukalie kimya .
Fanya kama tulivyo ongea usiku ,huyo aliekuja amekuja akijua wazi anakuja kufanya nini kwa maana hiyo mpeleke yeye mwenyewe.
Ila swala la kwamba ubadilishe maamuzi na umchukue Wardah hili nakupinga ,huyu mtoto anahitaji kuwa na kesho iliyo bora "
"Hahahahahha wallah tena najionea maajabu ,na sasa nimepata picha kwanini Alvin amekuwa na ujasiri wa kusimama na kunipinga ,kumbe tayar umeshamnywesha sumu mwanangu.
Na sasa nisikie kwa makini ,huyu binti alikuja kwa hela yangu mwenyewe na siku zote amekaa kwenye nyumba yangu anakula na kulala kwangu unanielewa.
Kwa hiyo atafanya kile ninachotaka mimi nasio nyie ,eti huwezi kuruhusu ,we ninani hadi usiruhusu mwanao huyu au una ukoo nae ?"
"Sina ukoo nae ndio lakini nikiwa kama mwanamke ninaejua nini maana ya kuwa mwanamke huyu hatoki hapa?"
"😆😆eti rudia tena we ni nani ?nyooo huna haya weye,, eti me mwanamke🤧 wakiita wanawake na wewe utatoka chakubimbi wewe 😏.
Embu usinifanye nikakutolea maneno ya ajabu saizi mie ,mtu umekausha kizazi chako kwa magonjwa ya zinaa , leba hujui inafananaje wala hujui utamu wa ndimu.
Alafu unataka kunikazia mishipa ya makalio ,we cheusi kwanzia leo utaanza kwenda na mimi kazini hii sio ombi ni lazima unanielewa "
Alvin hakutaka kuendelea kusimama bure alinifuata haraka na kunivuta nusu achomoe mkono wangu🥲 ,mkuku mkuku hadi chumbani.
Huku nyuma tukaacha wakongwe wakirushiana maneno,,basi tukafika chumbani akaniachia mkono na kusema.
"Fungasha kila kilicho chako uondoke haraka sana "
"Niende wapi!!?😳"
"We ni fala eeh😡, yaani unaona tunavyo pambana kutetea hilo tubwasha lako lisiende kuuzwa na kutumika hovyo alafu bado unauliza maswali ya kibwege oya👉 nitakufumua mikofi huo ushamba ukutoke .
Embu fungasha vurago chap usepe "
Nilimuangalia Alvin kwa huruma sana nakumuuliza " bado sijaelewa nini haswa ambacho kinaendelea maana naona mnagombana na madam bila sababu ya msingi.
Kama ni kuhusu kazi me nipo tayari kufanya kazi yoyote wala haina shida "
"Aaa mamae wewe😡 👉 nitakufumua h......" hakumalizia kuongea akaingia Shuu huku akisema .
"Kwanini unataka kumlazimisha wakati ameshasema anaweza? , mwaya Wardah kama unaona unaweza usimsikilize huyu anawivu tu ,ila ukweli hiyo kazi ina pesa nzuri .
Na najua unamajukumu mengi ambayo yanahitaji hela ya kutosha so binti mwenzangu nak.........." Alvin hakumuacha amalize alimvuta mkuku mkuku akamsukuma na kumsindikiza na bete la makalio.
Kwa hasira akafunga mlango na kunirudia akanambia" umesema uko tayari kufanya hiyo kazi ?"
Nikaitikia ndio kwa kutikisa kichwa , akasema " Wallah ushamba mzigo, hivi unajua utachokua unafanya au unaropokwa tu ?"
"Alvin ! Kazi ni kazi nitafanya tu haina namna "
"Kwa hiyo uko tayari kuuza thamani yako kama mtoto wakike kisa hela ? Okay basi acha niwe mteja wako wa kwanza "
Aliongea na kuanza kufungua mkanda wa suruali yake nilimuangalia kwa mshangao huku nikijiuliza anataka kufanya nini , sijakaa sawa nikashangaa anafungua zipu .😳
Weee niliruka kama kuku alikoswa koswa kuchinjwa , haraka akanidaka nikamwambia" Alvin hapana naomba unisifanyie hivyo tafadhali 🥺🙏."
"Nisifanye nini we siumesema uko tayari kufanya hii kazi ,sasa acha niwe mteja wako wakwanza haya sogea hapo nikupe baraka zangu"
Baada ya kusema hivyo ndio nikamuelewa alikuwa ana maana gani 🥺, nilijikuta nikianza kulia kwa uchungu ,ina maana nilikua naenda kuuzwa kwa wanaume 😭.
Alvin alinituliza na kunambia " usilie hizi ni changamoto za maisha na uzuri umeshavuka ,sasa kinachotakiwa ni kujiandaa kwaajili ya hatua inayofuata."
"Sasa nitaenda wapi 😥?"
"Utaenda wapi kwani hauna kwenu ?, binti embu cha kupoteza mda "
Niliinamisha uso chini na kusema "Sina nauli?"
"Hauna nauli ukimaanisha nini 🧐?"
"Kweli sina hela ,mshahara wangu wa mwezi uliopita nilituma nyumbani na mwezi huu bado hajanipa"
"Beki tatu wote akili zenu zinakomaga hapo , ina maana wewe ukipata hela kitu unafanya nikutuma nyumbani, kuweka akiba aaaah .
Haya sasa ndo ishatokea dharula haya nambie unaondokaje hapa ?"
Nilikaa kimya huku nikiangalia chini , akanambia " chukua nguo zako tuondoke "
"Tunaenda wapi ?"
"We acha maswali na ufunge tuondoke haraka maana nikikupa mgongo utaletewa njemba zilizo Shiba kisawa sawa "
Kweli kinyonge nilikusanya nguo zangu zote nilivyo maliza akanishika mkono tukatoka hadi sebleni mda huo bado madam na Aunt Vero wanachambana.
Bila kusimama Alvin aliongoza kuelekea mlango wa kutokea huku akinambia " angalia mbele ukigeuka tu unakuwa jiwe la chumvi " 😃 niseme nini zaidi ya kusema ndio na kufuata sharti.
Bila kugeuka nyuma wote tukatoka nje ,tukafunguliwa geti dogo haooo hadi bara barani akasimama na kunambia " bado hutakiwi kugeuka na kulia ni mwiko "
Nikajibu sawa ,bajaji ikaja tukapanda safari ya kuelekea nisipo pajua ikaanza .
Hatua mpya kurasa mpya 😊.
ITAENDELEA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni