WAMEIRUHUSU IPITE (Baada ya Kugundua hawana undugu) 1 - - - - - 5
SEHEMU YA 1
Kama utani hivi lakini kura zilipigwa usiku wa manane Nyamizi Mimi pamoja na my big brother Nico twende Jijini Dar es salaam tukapambane kwa ajili ya familia yetu π
Navyo liogopa hilo Jiji sasa π© ingawa sijawahi kufika nilijikuta nikitishika. Story zake huwa nazisikia tu kwa Mwantumu aliyewahi kutia miguu yake huko.
Sijui Baba yangu ana nini lakini aling'ang'ania twende Dar es salaam na si Dodoma wala Arusha.
"Moyo wangu unaniambia huko ndiko kuna urithi wetu. Wewe na Kaka yako ni lazima muende kuuchukua β" Baba yangu alirahisisha mambo π eti huko ndiko kuna urithi wetu, sasa si angeenda kuchukua mwenyewe enzi za ujana wake.
Mimi na Kaka yangu tulitazamana tu
"Nyamizi ukisikia neno Wanaume kichwani mwako unapata picha gani π" Baba yangu aliniuliza akiwa kanikazia macho
Maswali yake huwa ni ya kichokozi, mie huyu nilivunga kama sina ufahamu π kuliko nijibu niibue vita isiyoisha ni heri kuinama kama kobe
"Hujui eeeh, sasa nitakueleza Wanaume ni kikosi kidogo cha waasi, endapo utashirikiana nao kwa njia yoyote ile utapotea β. Hivyo naomba ukae mbali nao" Baba yangu aliongea kisha akamkabidhi Kaka yangu nauli
Nilitarajia na yeye ataambiwa kuwa Wanawake ni kikosi kidogo cha waasi lakini haikuwa hivyo π
"Ni saa nane na nusu, hebu changamkeni kujiandaa, hamna haja ya kubeba mizigo mingi si mnajua tena hakuna Shangazi yenu huko..... basi linaloelekea Jijini Dar es salaam linaondoka saa tisa na nusu. Changamkeni pia msije kuachwa β" Baba aliongea kisha akasimama sijui ni kitu gani alikumbuka alitugeukia
"Dar es salaam mnaenda kuchukua tu urithi wetu na si vinginevyo. Mume, mke sijui watoto wote mtakuja kuwapata huku β" Baba aliongea kwa msisitizo kisha akatutakia safari njema
Nilielekea chumbani kwangu ni kachukua nguo tatu tu ni katupia kwenye begi langu.
Kaka yangu alikuwa kashajiandaa tayari
Alinishika mkono tukatoka nje tayari kwa kuondoka
"Nyamizi....." Sauti ya Mama ilisikika ikituita taratibu ni kama alikuwa ana kutuibia siri....
"Vipi Mama π" Kaka Nico aliuliza
"Sijui kama mlikuwa mnayazingatia maneno ya Baba yenu.....lakini msije kufanya uzinzi huko mjini mtang'ang'ania kama Shangazi yenu π" Mama aliongea kisha akarudi zake ndani
Brother Nico alinisogeza karibu akanishika bega
"Twende tuwahi basi, mausia ya baba tutayafanyia kazi baada ya kufika Jijini Dar es salaam β"
Nilitikisa kichwa kumaanisha nimeelewa, tulianza kutembea kama Wanajeshi. Kwa bahati mbaya nilijikwaa π© niliumia kidole gumba. Mie huyu nijikaze π si rahisi niliangua kilio hicho kama nimechomwa sindano kwa bibi ππ
Vile Kaka yangu ananipenda kupita maelezo aliniweka mgongoni
"Nishikirie kwa nguvu zako zote, si unajua kwenye lile pori kunakuwaga na mambo mengi β tunapita pale kama mshale" Brother Nico aliongea
Basi nilifuatisha ushauri wake, nilimshikiria kwa nguvu zote kisha ni kafumba macho, tulipita kwenye hiki kipori kidogo kama upepo......tulipofika sehemu salama alinishusha
"Mbwa wewe ungeenda jeshini tu, sikumbuki hata tumepitaje pale π " Nilimuambia Brother Nico huku nikicheka.
Yeye pia alianza kucheka, sijui ni nini kilinipata nilijikuta nimemuangalia. Kwa kifupi tulianza kutazamana.
Sijui ni pepo au nini kila nikimuangalia kuna hisia fulani huwa zinaibuka π ni hisia mbaya sana. Niligeukia pembeni sikutaka kuonekana mjinga π
Tulitembea kidogo tu tukafika stendi, si unajua ni kijijini basi hata stendi yetu haikuwa imechangamka sana.
Brother Nico alilipia pesa tukakatiwa tiketi moja.
"Huyu nitampakata mpaka tunafika Dar β"
"Acha ukuda, basi ongeza shilingi elfu 20 nitamhesabu kama mzigo π" Mkata tiketi aliongea
Kaka Nico aliachia tabasamu kisha akatoa shilingi elfu 20, nilihesabiwa kama gunia la mahindi π . Kaka yangu alilenga matumizi mazuri ya pesa na si kingine
Basi alikaa yeye kwenye siti kisha Mimi nikaka kwenye mapaja yake.
Ilivyotimia saa tisa na nusu tulianza safari....toba mie nilijikuta nikifikiria uzinzi tu. Namna alivyokuwa ananipakata nilikuwa hoi. Lakini huyu si ni Kaka yangu kwanini nakuwa hivi π«
Nilikuwa nahisi kabisa kama mti wake umesimama hivi.
Sikutaka hatari na fedheha π©, nilikaa Mimi kwenye siti kisha yeye akakaa kwenye mapaja yangu. Nilipitisha mikono yangu kiunoni mwake. Nilifanya hivi kumpa support sikutaka aanguke.
Sijui nini kilimpata alinishika vidole vyangu akawa kama ananipapasa hivi π
Nina uhakika nia yake haikuwa mbaya..... ila kwangu nilijihisi vibaya.
Tuliendelea kukaa kwa kupokezana mpaka tulipofika Jijini Dar es salaam β.
"Nyamizi hapa ndio Jijini Dar es salaam...." Brother Nico aliongea, hakuonesha kutishika na muonekano wa hili Jiji. Kwa kifupi haya mazingira yalionekana kumpendeza kuliko hata ya kule kijijini β
Alinivuta karibu yake kisha akapitisha mkono wake kiunoni mwake.
Kwa mbele yetu kulikuwa na ghorofa refu sana.
"Nyamizi nina ndoto za kuja kumiliki ghorofa kama hili, na kuahidi utakuwa mtu wa kwanza kuingia kwenye hilo ghorofa π" Brother Nico aliongea kisha akaniangalia akiwa kwenye uso wa tabasamu
Moyo wangu ulianza kwenda mbio, hasa baada ya macho yetu kukutana. Sikutaka kugeukia pembeni..... nilihitaji kujua ni kitu gani kitatokea.
My zangu tukutane sehemu ya 02 π
SEHEMU YA 2
Brother Nico alikuwa wa kwanza kuyaondoa macho yake kwangu.
Alirudi kuliangalia ghorofa, aliachia tabasamu ni kama alikuwa anazungumza nalo hivi
"Nadhani utakuwa na njaa, naomba tutafute mgahawa tupate chakula π" Brother Nico alipendekeza
Mitaa ya hii ilikuwa ni ya Kishua, hakukuwa na migahawa midogo kama ile ya kijijini β.
Tuliingia kwenye mgahawa Mmoja hivi, brother Nico aliongea na Mhudumu. Baada ya kuelewana chai ya maziwa na sambusa zililetwa mezani
"Mbona ni sahani moja tu na kikombe kimoja wewe haunywi chai π" Niliuliza
"Usiwe na shaka kula, kwenye begi langu kuna maandazi ya juzi uliyochoma ndio nakula hayo π "
"Aisee wewe ni kichaa, yale maandazi niliyochoma juzi unayo bado π vipi kuhusu chai unakunywa ya nani....."
"Tunatumia wote hiyo π"
Sikuwa na namna tulikuwa tunakunywa kwa kupokezana, dakika ya mwisho Brother Nico alikunywa maziwa yote π alifanya hivi kunikomoa
Kabla hajayameza nilitegesha kikombe anipunguzie, naye si alifanya hivyo π. Bila haya wala kinyaa nilikunywa. Ile naweka kikombe hivi nilikutana na macho yake, ni kama alikuwa haamini kama Mimi huyu naweza kunywa maziwa aliyokwisha yaweka mdomoni
"Nyamizi kuna kitu nataka kukuambia, ujue sijaja tu Dar es salaam kufanyia kazi ombi la Baba. Kuna kitu kimenileta, wacha niende uwani kwanza narudi β" Brother Nico aliongea huku akibeba begi lake
Nilitikisa kichwa kuashiria nimeelewa, alitembea kama hatua tano hivi sijui nilifikiria nini nilijikuta ni kimuita
"Brother Nico"
Aligeuka nyuma kisha akasikilizia ni kitu gani nataka kusema. Nilikuwa na cha kuongea sasa nilimuonesha tu tabasamu π
Aliishia kucheka kisha akaendelea na safari yake, nilikaa hapa kumsubiria kama nusu saa hivi lakini hakutokea.
Nikijipa matumaini atakuwa anatoa haja ya wiki nzima π
Basi nilisubiri na kusubiria lakini hakutokea, nilichoka kukaa hapa niliamua kumfuatilia mwenyewe.
Kila choo nilichofungua hakuemo π....uoga ulinitanda zaidi nilipiga kelele
Security walikuja kunisikiliza, wao pia walinisaidia kwa kukagua choo kimoja baada ya kingine. Hawakuishia hapo walikagua camera, cha ajabu camera hazikuonesha chochote
"Oyaaah fanya kuondoka na uache kutusumbua...." Security waliniruka mita mia.
Sikutaka kusumbua nao, nilichukua begi langu nikaondoka.... nilianza kupita huku na kule ni kimuita π nilijipata ni kichoka kwa sababu nilikuwa naita kitu ambacho sikioni
"Kama tukifuatana kama kumbikumbi huenda tukashindwa kufanikiwa. Nadhani hiki ndio kitu alitaka kuniambia.....sina sababu ya kuhuzunika π" Nilijifariji kisha ni kajifuta machozi
Sikuwa na pa kuanzia lakini kwa kuwa Baba yangu aliamini naweza kupambana kwa ajili ya familia yangu nilijipiga kifua β
Sikutaka kuliogopa Jiji la Dar es salaam, story za Mwantumu niliziondoa zote kichwani mwangu.
Nilitembea kwa kujiamini nikiwa sijui naanzia wapi, nilipita mitaa fulani hivi nikapata kuona migahawa ya bei chee. Bila shaka huku ndiko uswazi kutokana na hadithi za Mwantumu β
"Mpuuzi wewe naomba uondoke kwenye mgahawa wangu π haiwezekani unipikie ugali mbichi kila siku" Mwanamke mmoja mnene aliyepaa hewani alifoka huku akirusha mateke.
Si ndio nilijipenyeza hapa hapa kuomba nafasi iliyobaki wazi
"Una uhakika unaweza kupika ugali ukanukia mtaa mzima π" Niliulizwa
Nilitikisa kichwa changu kuwa naweza, basi nilipatiwa jiko nioneshe mfano. Nyie watu sijui ni uchizi, ile naanza tu kukoroga uji kwa ajili ya kupika ugali nilijikuta nikimuona brother Nico π akitabasamu
Emu tukutane sehemu ya 03 π
SEHEMU YA 3
"Kwani una kichaa hadi utabasamu ndani ya sufuria π€" Niliongea na taswira ya Brother Nico
Taswira yake haikunisikia iliendelea tu kunitazama, ni kama alikuwa ananipa support hivi ya kupika ugali.
Nilikoroga uji mpaka ulipotokota vizuri, nilijipinda ilivyo ni kaanza kusonga ugali.....wacha mmiliki wa Mgahawa aje kunichungulia
"Weee binti mbona ugali unanukia hivi kabla hata haujaiva π"
"Mbona bado haujanukia ndio kwanza nimeanza kupika π " Nilijigamba
Nilijipinda ilivyo mpaka ugali ukaiva, ulikuwa unanukia haswa.... wacha wateja wajazane kula ugali π€
"Ndio ushapata hivyo ajira β...." Mmiliki wa Mgahawa aliongea tena akionekana kuumia kama nitasema kuondoka
"Sina sehemu ya kulala, sijui unanisaidiaje hapo π"
"Ondoa shaka utalala nyumbani kwangu, watoto wangu wote wapo mkoani kutafuta maisha hivyo sehemu za kulala ni nyingi tu β"
Nilifurahia ukarimu wake, basi ikawa ni kazi yangu kupika kwenye mgahawa wake. Kwa kuwa nilikuwa nalala bure kwake hakunipa mshahara π
Kila mara nilijikumbusha kuwa nimetumwa mjini kupambana. Kufanya kazi bure kwenye mgahawa wa Mama ntilie kisa na maana nalala kwake sikufurahishwa hata kidogo.... nilijiahidi kumkwepa kiakili.
Asubuhi moja ikiwa ni siku ya jumapili (hii siku huwa hatufanyii kazi)
Niliingia mtaani kudhurula, bahati nzuri sasa niliparamiana na Mwantumuβ. Uvaaji wake tu ulitosha kuniambia kalizoea Jiji kupita kiasi
"Nyamizi π³ bora hata nimekuona"
"Kuna nini π³"
"Kwanza mara ya mwisho kuongea na familia yako ni lini π"
"Mwezi sasa umepita, simu alikuwa nayo Kaka Nico lakini tumepotezana β"
"Yule si Kaka yako....nasikia Mama yako amewahi kufanya kazi hapa Jijini enzi hizo akiwa binti. Sijui hapo kati kati kulitokea nini lakini boss wake alimpa mtoto amlee, yeye akaenda zake Uzunguni kikazi. Siku moja Mama yako akiwa kwenye mjengo mwenyewe anaishi kama Malkia na Wafanyakazi si alivamiwa, inaonekana Majambazi walimtaka tu mtoto. Ili kuokoa maisha yake na ya Mtoto alitoroka ndio kuja kujificha kule Kijijini. Juzi kati tu hapo boss wake alitimba kumtafuta Mama yako. Nasikia Nico yupo mikononi mwa Mama yake tayari β.....wacha nimuwahi Sponsa wangu tutazungumza kwa wakati mwingine π" Mwantumu aliongea kisha akajitupa kwenye bajaji
Sikuwa nayaelewa maneno yake hata kidogo π.....japo sikuwa na simu lakini namba ya Mama ilikuwa kichwani.
Nilisogea kwenye duka la Mangi ni kaazima simu. Haikuwa rahisi kusaidika lakini baada ya kumpa elfu tano alinisikiliza
Simu iliita kidogo tu Mama yangu akapokea.
Baada ya kujitambulisha alizungumza historia yote kama alivyosema Mwantumu
"Yale ni maisha ya Nico na si yako, endelea kujitafuta huko pekee yako π wacha ni kate simu kabla Baba yako hajaja. Maana kawa mwenye hasira tu bila sababu ya msingi" Mama yangu aliongea kisha akakata simu
Nilimrudishia Mangi simu yake nikiwa siamini kabisa.
Nilijikuta ni kikumbuka namna Brother Nico alivyokuwa akinitendea wema.
Nilijikuta ni kikumbuka mara kwa mara macho yetu yalivyokuwa yanatazamana π sina uhakika kama hisia zake zilikuwa zinateseka kama za kwangu.
Sikuona sababu ya kuendelea kukaa hapa β nilimuaga Mangi kisha ni kaendelea kuuchapa mwendo.
Sikuwa nikitamani kutumika kwa Mama ntilie kibonge.
Hivyo nguvu za kutafuta kazi mahali kwingine ziliongezeka. Si unajua tena mtu akiwa anatafuta kazi anavyogeukaga huku na kule basi ndivyo ilikuwa kwangu.
Wacha niparamiane na Mwanamke aliyekuwa kapendeza sana π©. Niliwahi kumuomba msamaha si unajua tena Mimi ni Mgeni huku
"Umesamehewa π" Aliongea huku akitabasamu....sijui ni kuchanganyikiwa au nini nilijikuta ni kimuona akifanana na brother Nico
Ile anataka kuendelea na safari yake niliwahi kujitangiza
"Naomba niwe Mfanyakazi wako wa ndani π" Nilijichekesha
"Sihitaji Mfanyakazi wa ndani lakini kwa kuwa hauna sehemu ya kwenda nitakuchukua, nifuate β" Mwanamke huyu aliongea
Nilimfuata kwa nyuma, tulitembea kidogo tu ndinga ya maana ikafunga breki mbele yetu.
Milango ilifunguka yenyewe kama yale magari ya waheshimiwa. Mwanamke mrembo alinipa ishara ya kuingia....niliingia kwenye gari nikiwa sina hofu kabisa
Tukutane sehemu ya 04 π
SEHEMU YA 4
Ingawa tumo ndani ya gari haikuzuia chochote kwetu sisi kupata chakula cha mchana..... katika gari hili kulikuwa na Wahudumu. Tulipata chakula kama tuko hotelini hivi.....
"Mara ya mwisho kula kuku ilikuwa ni lini π" Mwanamke huyu mrembo aliyejitambulisha kwa jina la Hannah aliniuliza
Badala ya kumjibu swali nilijipata nikiona aibu isiyo na kifani. Bila shaka alikuwa ananikagau namna navyoivunja vunja mifupa mfano wa fisi π€ si unajua tena kwetu tunafuga kuku ila kula nyama yake sasa ni mpaka washikwe na ugonjwa wa kideli
"Muongezee nyama ya kuku β" Hannah alitoa amri kwa Mhudumu aliyekuwa amekaa na hotpot za vyakula
Basi niliongezewa kuku, kila nilipomtazama Hannah niliiona sura ya Brother Nico π
Safari ilikuwa ndefu kidogo, si unajua tena balaa la shibe nilijikuta ni kipambana na dalili za usingizi, sijui hata ilikuaje potelea pote nilikuja kushtuka baada ya kuamshwa β
"Shuka tumefika " Hannah aliongea
Nyie watu, kuna watu wanamiliki nyumba halafu kuna wengine wanamiliki vikingio vya mvua π€.
Ilikuwa ni nyumba kubwa sana kiasi kwamba nilishindwa kujizuia kuikagua huku na kule.
Ghafla tu nilishtukia mbwa hiyo inavuta gauni langu la kitenge π©
"Punguza kushangaa mazingira unaonekana kama mwizi machoni kwa huyu mbwa β" Hannah aliongea huku akiitimua
"Sa...sa..sawa...." Nilijibu
Kwa pamoja tuliingia ndani, hili jumba lilikuwa na Wafanyakazi wengi, ni kama amenisaidia tu kupata sehemu ya kujisitiri hakuwa na uhitaji wa Mfanyakazi kabisa β
"Bado kajifungia chumbani kwake tu π" Hannah alimuuliza Mwanamke mmoja aliyekuwa anafuta glass
"Ndiyo, hata ulaji wake wa chakula si mzuri π"
"Ni mshenzi sana, huenda ana kitafuta kifo kwa nguvu. Sitajieleza kwake tena acha afe π§" Hannah aliongea kwa sauti ya msisitizo
"Ni mtoto wako wa pekee, hutakiwi kumkatia tamaa mapema kiasi hicho na hata hivyo ana hitaji muda kukubaliana na ukweli π"
"Ukweli upi π? kama unajali kuhusu yeye hakikisha ana kula. Na mambo mengi sana kichwani mwangu na yote yanahitaji muda wangu.....huyu ni Mfanyakazi mpya mpokee β" Hannah aliongea
"Mbona tuna Wafanyakazi wa kutosha π"
"Mpokee hana sehemu ya kwenda, usisahau kama hapa ni Jijini Dar es salaam β" Hannah aliongea kisha akaendelea na safari yake
"Karibu, kule jikoni kuna vyombo vichafu.....fanya haraka kuosha ukimaliza pika ugali na samaki kwa ajili ya first born wa mother house....jina langu naitwa Veronica β nifuate ni kuoneshe jiko lilipo" Basi Veronica aliongea kwa hasira hivi ni kama hakufurahishwa na ujio wangu
Nilimfuata kwa nyuma, weee vyombo vilikuwa vingi sana na vyote hivi nilitakiwa kuosha mie π
Si unajua tena sina asili ya uvivu. Nilijituma kadri ya uwezo wangu kuosha vyombo. Nilipomaliza nilishika sufuria ni kaanza kupika ugali wa kikwetu β
"Ugali mgumu huu wa kuvunja na nyundo sina uhakika kama atakula π.....nikisema urudie kupika ugali mwingine utachelewa. Nitilie hivyo hivyo tupeleke," Veronica aliongea
Basi nilifanya kama alivyo agiza, nilibeba sahani ya matunda kwa pamoja tulipeleka chakula cha mchana
"Boss mdogo, fungua mlango nimeleta chakula π" Veronica aliongea huku akijichekesha, ni kama alikuwa anambembeleza hivi
"Weka hapo mlangoni β" Sauti ilisikika
Nyie watu macho yalinitoka haswa π³π³ baada ya kusikia sauti Kama ya brother Nico.
Nilitamani aongee tena lakini haikuwa hivyo, Veronica alinisihi tuondoke.
Nilipatwa na shauku ya kumfahamu kwa sura Kijana aliyeongea kama brother Nico lakini haikuwa rahisi β
Basi Wafanyakazi wote (tulikuwa nane kwa idadi) tukiwa tuna safisha bustani kwa usimamizi wa Hannah.
Veronica alikuja kwa kukimbia
"Madame Hannah, first born wako amekula ugali wote, siyo hivyo tu yupo anajiandaa atoke out na wewe π "
"Mwanangu Mimi kala ugali wote na anataka kunitoa out π³"
"Ndiyo....."
"Maid aliyepika huo ugali ana zawadi yake π wacha ni kajiandae pia" Hannah aliongea kisha akatoka mbio
"Una zawadi yako π" Veronica aliongea huku akionesha wivu
Mimi wala sikumjali, shauku yangu ilikuwa ni kumuona first born wa Hannah, mwenye kuzungumza kama Nico.
Basi nilivunga kubanwa na haja ndogo, nilitembea taratibu kuelekea uani. Wakati natoka si ndio nilimuona Hannah akiwa na Kijana wake.
Alikuwa ni brother Nico, macho yangu na yake yaligongana tukabaki tumetazamana π³π³π³
Usikose sehemu ya 05 π
SEHEMU YA 5
Nilitaka kumuita kwa jina lake lakini nilivunga β
"Nyamizi utanisaidia kutoa magazeti yangu kule bustanini" Hannah aliongea
"Sawa, shikamoo Kaka" Nilimsalimia Nico
"Nyamizi bhana π huyu anafaa kuambiwa mambo tu ukianza kummiminia salamu unamchanganya" Hannah aliongea
"Marahaba β" Brother Nico alijibu kwa ufupi kisha akamshika mkono Mama yake wakasepa.
Nilitarajia atageuka nyuma lakini hakufanya hivyo π hii ilinipa wakati mgumu sana lakini kwa upande mwingine niliamini ananivungia sababu ya Mama yake
Waliendelea na safari yao nami nilirudi bustanini kukusanya magazeti
"Haya magazeti nitakuja nayo, hebu nenda ukafanye usafi chumbani kwa Nico kule tulipeleka chakula, hakikisha una pasafisha kwa umakini β" Veronica alinituma
Basi nilitembea chapu ni kaelekea chumbani kwa Brother Nico.
Ile naingia tu nilipokelewa na begi lake alilotoka nalo Kijijini. Hapa ndipo nilipata kuamini kuwa huyu ni Nico.
Shauku ya kulikagua iliniijia, mmmh wacha nikutane na picha tuliyopiga wote mwaka jana siku ya Christmas.
Sikuwa nimependeza kusema ila pozi tuliloweka ndilo lilitufanya tuonekane tumependeza π€
Katika kufunua funua si ndio nilikutana na bahasha, niliifungua chapu ndipo nilikutana na picha ya Boss Hannah akiwa kapiga na Mama. Japo walikuwa ni Vijana bado lakini sura zao hazikuweza kupotea
"Huenda brother Nico alikuwa ana fahamu tangu mwanzo kuwa Mimi siyo Dada yake wa damu π€" Nlijiwazia kichwani mwangu
Basi nilirudisha vitu vilivyokuwa kwenye begi, nilianza kufanya usafi kwa moyo mmoja....
"Nyamizi usiniambie hicho chumba kilikuwa ni kichafu sana.... usiniambie sisi hapa huwa hatufanyi usafi ipasavyo..." Sauti ya Veronica ilinishtua
Japo sikuwa nimemaliza ilinilazimu kutoka,
"Ni kama umekuja hapa kutupindua π "
"Siwezi kufanya hivyo π€"
"Haya funga hapo chapu uje tusaidiane kazi β"
Nilifunga kisha ni kamfuata Veronica, tulianza kazi ya kukunja nguo.
Kufika saa moja na nusu kazi zote zilikuwa zimekwisha, uhuru wa manyani ulitangazwa rasmi. Vile nilikuwa nimechoka sasa nilijifungia chumbani kwangu nilale, kwani kulilalika sasa..... nilijikuta ni kimuwaza tu Nico. Vile dirisha la chumba changu limetazamia getini basi nilivuta kiti nikakaa hapa β
Nilihitaji kujua brother Nico anaingia saa ngapi....ikiwa ni saa nne kamili za usiku gari liliingia.
Moja kwa moja niliamini Hannah na Kijana wake watakuwa wamerejea
Nilikaa mkao wa kula, akili yangu iliniambia iwe isiwe ni lazima brother Nico atakuja kugonga mlango wa chumbani kwangu....sijui ni ujinga au nini nilianza kujiremba haraka haraka π sielewi hata kama nilikuwa napatia au na haribu.
Dakika 20 hazikupita mlango wangu uligongwa, akili ya kufungua vishikizo ili nyonyo zangu zionekani iliniijia.
Taratibu nikiwa nimeweka uso wa tabasamu nilienda kufungua mlango
Macho yangu yalipanuka zaidi baada ya kukutana na Brother Nico.
Aliinikumbatia papo hapo π€ sikutaka mambo yaonekane hadharani nilimhimiza aingie ndani.
"Nikiwa na miaka mitano, Mama yako alinieleza ukweli kuwa yeye si Mama yangu. Niliupokea ukweli huo na nikaweza kuishi nao β...... Hannah ni Mama yangu. Sijui imekuaje ukaishia hapa lakini huo ndio ukweli halisi" Brother Nico aliongea baada ya kuchoka kunikumbatia
Sikuwa na namna zaidi ya kuachia tabasamu, nilishtukia tu akifunga vishikizo vya blauzi yangu π si unajua tena niliacha nyonyo zionekane.
Hakuishia hapo, alitoa kitambaa kwenye mfuko wake wa suruali akaanza kunifuta usoni. Si mnajua tena nilijiweka urembo ili nionekane navutia π€
"Kwani hukujiangalia kwenye kioo? usiniambie ulienda kwa boyfriend wako hivyo π "
"Boyfriend π acha kuniambia habari hizo, kwani umesahau kama Wanaume ni kikosi cha waasi, umesahau kama ni kitembea na Wanaume wa huku nitang'ang'aniana.....ujue" Kabla sijamaliza kuzungumza, Brother Nico huyo hapa alinikumbatia kwa nguvu kiasi kwamba nilishindwa kuhimili nikajipata nimelala chini, yeye akawa juu yangu π
Tuliangaliana, moyo wangu ulishtuka na hata nikahisi ngoma za Wajeda zimehamia moyoni mwangu π
"Nafurahi kuona u mzima wa afya, ile siku sikuwa naenda uwani, nilitoka nje ni kutafutie hereni lakini kwa bahati mbaya nilikutana na watu wakanichukua β..... naomba uwe na usiku mwema Dada yangu mzuri, itapendeza kama utaendelea kuvunga hunifahamu....pindi mambo yatakapo kuwa sawa nitamfahamisha Mama kuhusu wewe" Brother Nico aliongea kisha akanichapa busu la kwenye paji la uso π
Alisimama aondoke, nilimvuta shati lake......sijui ni nini nilitaka kifanyike lakini viungo vyangu vya uzazi vilikuwa vinapumua kwa kasi π
Tukutane sehemu ya 06 π
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi