Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya โ Gonga94 Semajambo
Gonga94 ยท Stories
30 Nov -0001
102 views
VYOTE NDANI GONGA94
Hadithi ya "Mbweha ๐พ na Jogoo ๐
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Hadithi ya "Mbweha ๐พ na Jogoo ๐
Siku moja, mbweha alipita karibu na jogoo.
Akamwambia:
"Ewe jogoo, niliwahi kusikia sauti ya baba yako mara moja, ilinivutia sana na nikatamani kuisikia tena."
Jogoo akamjibu kwa majivuno na sifa;
"Sauti yangu ni nzuri kama ya baba yangu!"
Kisha akafumba macho yake ili apige kelele kwa sauti yake.
Mbweha alipoona jogoo amefumba macho, akamrukia maramoja na kumkamata, kisha akakimbia naye mbali.
Mbwa wote wa kijiji walipoona tukio hilo, wakaanza kumkimbiza mbweha.
Jogoo, akiwa mikononi mwa mbweha, akamwambia mbweha:
"Kama unataka kuwakimbiza mbwa hawa wasikufuate, waambie kuwa mimi (jogoo) sitoki kijijini kwao."
Mbweha alifumbua mdomo wake ili kuzungumza, lakini kabla hajamaliza kusema โ jogoo akaanguka kutoka kinywani mwa mbweha na kukimbia akaokoka!
Mbweha akasema kwa hasira:
"Ulaaniwe mdomo unaoongea wakati ambao unatakiwa unyamaze!"
Jogoo akamjibu akisema;
"Na lilaaniwe jicho linalofumba wakati linapaswa kuwa macho!"
Mafunzo kutoka hadithi hii:
1. Usijivune au kuamini sifa unazosifiwa kirahisi, hasa mbele ya watu wenye nia mbaya kwako.
2. Mtu mjanja hujua wakati wa kunyamaza na wakati wa kusema, lazma ujue kusoma alama za nyakati, na huo ndio ujanja.
3. Uwe makini na hila za watu wenye tabia ya unafiki, mnafiki anahila nyingi pale anapotaka kufanikisha jambo lake lazima uwe makini mno juu ya hila za watu.
4. Usifumbe macho (kihisia au kimawazo) mbele ya hatari โ kuwa macho kila wakati, kamwe usimuamini mtu moja kwa moja ajapokujia na sura nzuri ya Swahaba Abubakri Swiddyq.
5. Ujasiri na busara vinaweza kukuokoa hata katika hali ya hatari sana,.
Ni hadithi fupi yenye hekima nyingi!
Maoni
You're not logged in
X
Login
X
signup
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
JOGOO WA KIENYEJI 1----5
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐ sehemu ya 1 Mwandishi:lissa mwalla Naitwa Talya jones,ni mtoto wa pili katika familia...
โMtu Aliyenusurika Kisiwa cha Wala Watu na Kuwa โMfalmeโ โHadithi ya John R. Jewitt (1802โ1805) 1. Safari ya Hatima: Meli ya โBostonโ (1802)
โขJohn R. Jewitt alikuwa kijana raia wa Uingereza, fundi stadi wa vyuma (armorer). Mnamo mwaka 1802, alijiunga na wafany...
PAMELA NA KIPINI Enzi zile vitabu vingi vya shuleni vilikuwa vizuri sana na vilisheheni hadithi nzuri na zenye kuvutia na vilitia hamasa sana kwa wanafunzi kujifunza.Hadithi zenyewe zilikuwa:-
.Siku ya gurio Katerero .Utamu wa Mua umezamisha meli .Mama mbuzi na watoto Saba .Bibi tarabushi .Kaka kanzi na bibi ku...
โ ๏ธ ONYO: Hadithi hii ina maudhui ya watu wazima. Inafaa kwa wasomaji walio na umri wa miaka 18 na kuendelea. Tafadhali soma kwa tahadhari. โ ๏ธ Post hi inafaa kwa page ya watu wazima ZAWADI Sehemu ya 12
Simulizi za john 0789 824 178 , 1000 Nilikosa pozi, nikashindwa kujibu. Lakini nikawaza, โNamuogopa nini? Mumewe natemb...
๐ Onyo: Hadithi hii inafaa kwa watu wazima tu (18+). Ina maudhui ya kihisia na maisha ya shule yenye mchanganyiko wa mapenzi na changamoto. KAYLA Sehemu ya 6
Mwandishi; maramoja the great Simulizi za john @topfans 0789 824 178 1000 Akasema ndio anakuja madam akasema una uwakik...
๐ Onyo: Hadithi hii inafaa kwa watu wazima tu (18+). Ina maudhui ya kihisia na maisha ya shule yenye mchanganyiko wa mapenzi na changamoto. KAYLA Sehemu ya 6
Mwandishi; maramoja the great Simulizi za john @topfans 0789 824 178 1000 Akasema ndio anakuja madam akasema una uwakik...
Hadithi ya "Mbweha ๐พ na Jogoo ๐
Siku moja, mbweha alipita karibu na jogoo.
Akamwambia:
"Ewe jogoo, niliwahi kusikia sauti ya baba yako mara moja, ilinivutia sana na nikatamani kuisikia tena."
Jogoo akamjibu kwa majivuno na sifa;
"Sauti yangu ni nzuri kama ya baba yangu!"
Kisha akafumba macho yake ili apige kelele kwa sauti yake.
Mbweha alipoona jogoo amefumba macho, akamrukia maramoja na kumkamata, kisha akakimbia naye mbali.
Mbwa wote wa kijiji walipoona tukio hilo, wakaanza kumkimbiza mbweha.
Jogoo, akiwa mikononi mwa mbweha, akamwambia mbweha:
"Kama unataka kuwakimbiza mbwa hawa wasikufuate, waambie kuwa mimi (jogoo) sitoki kijijini kwao."
Mbweha alifumbua mdomo wake ili kuzungumza, lakini kabla hajamaliza kusema โ jogoo...
๐ Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/hadithi-ya-mbweha-na-jogoo
Maoni