KICHAA NA MIMBA YA BOSS ________________________________________* *SEHEMU YA KUMI NA SITA* Shahidi alikaa vizuri na kuangalia kwa makini huku akisikiliza
Nini kilitokea mpaka ikawa vile? Mama Farida alishusha pumzi ndefu kisha. akaanza kusimulia ilivyokuwa.
"Shania ni binti ambae amepitia kwenye maisha magumu sana na ameshuhudia mambo makubwa tangia akiwa mdogo.
Kwanza ameshuhudia vifo vya wazazi wake.
Baba yake alimpiga mama yake sababu ya wivu wa kimapenzi na kumsababishia kifo. Baada ya kuona amekuwa nae alikunywa sumu akafa. Nimemleta Shania tangia akiwa na umri wa miaka kumi alikuwa ni mtoto mnyonge sana lakini baada ya kumtafutia mwana saikolojia alianza kusahau yaliyopita akaendelea na masomo yake na alikuwa anafanya vizuri sana mpaka alipofika elimu ya chuo alipata mchumba na mwaka wa mwisho waliamua kufunga ndoa. Aliishi kwa furaha na amani pamoja na mume wake. Wallishi maisha mazuri sana hakuna alichokuwa anakosa kwa mume wake.
Baada ya siku kwenda Shania akibeba ujauzito furaha iliongezeka kwa mume wake mpaka alimpa zawadi ya gari. Maisha yaliendelea mpaka ujauzito wake ikafikishwa miezi tisa Shania akajifungua mtoto mzuri mwenye afya tele. Yule mtoto alikuwa mtoto wa kike na Shania alimpa jina la mama. yake ilham.
Hapo ndipo Shahid alipoanza kupata mwanga, akimkumbuka yule mdoli aliekuwa anapendwa sana na Shania kumbe alikuwa akimchukulia kama mtoto wake ndio maana alikuwa mkali sana pindi mtu alimshika vibaya au kumuweka. chini.
Mama Farida aliendelea kuongea. *Shania alimpenda sana yule mtoto, alikuwa ni kila kitu kwake, alikuwa ni faraja yake Alihisi amepata ndugu na mwenzake wa karibu. Ilham alikuwa mdogo sana lakini ulikuwa ukimkuta anaongea nae utafikiri anaongea na mtu mwenye akili timamu au mtu mzima mwenzie Siku moja shania alikuja hapa nyumbani kwangu akiwa na mume wake pamoja na mtoto wao. Tulikaa hapa mpaka Shania alienda jikoni wakaungana na ndugu yake Farida wakapika chakula cha usiku, tukala pamoja Walipokuwa wanataka kuondoka waliniaga. Shania alisema. "Shangazi mume wangu kachukia likizo kazini hivyo kesho tunasafiri tunaenda tunaenda mapumzikoni, kutalii huko mbuga za wanyama. Niliwaambia sawa tukiachana nikawa taka safari njema wakaondoka wakarudi kwao na sisi zikalala ule usiku. Kesho yake walianza safari kuelekea huko walikokuwa wanaenda. Lakini ile safari haikuwa imepangwa, hawakufika huko walikokuwa wanaenda walipata ajali mbaya sana Ilham na baba yake walifika palepale na Shania alikuwa
kwenye hali mbaya sana. Shania alikimbizwa hospitali na Ilham na baba yake waliohifadhiwa chumba cha maiti..
Mama Farida alishindwa kujizuia akaanza kulia kwa uchungu. Shahidi nae aliguswa sana na hizo taarifa ila alijikaza kiume. "Basi shangazi usilie.
Ilikuwa ni siku nzito sana kwangu nilihisi kuchanganyikiwa moyo wangu ulivuka damu, wasi wasi na hofu vilitawala. Kwanza msiba pili sikuwa na matumaini kama Shania atapima maana hali yake ilikuwa ni mbaya sana yani mbaya mno hakuwa alijitambua wala kutingisha. kidole kwenye wodi zilikuwa ni sauti za mashine tu.
Baada ya siku mbili ziwazika Ilham na baba yake na historia ya maisha yao iliishia hapo tukaanza kupambana na Shania.
Uwezo wa familia yetu ulikuwa mdogo sana na hospitali zilihitajika pesa Ndugu wa mume walitususia hawakuja hata kumuona yani uhusiano wetu uliishia pale. Hatukuwa na jinsi ilibidi tuuze nyumba mbili za Ilham na vitu vyake vyote vya urithi kwaajili ya matibabu lakini haikutosha ikabidi tuuze mashamba ya urithi tuliyoachiwa sisi na baba yetu tukamtibu Shania. MUNGU alisaidia Shania alipoona lakini kitu cha kwanza alitaka kumuona mume na mtoto wake. Tulijaribu kumdanganya danganya lakini uongo una mwisho na dunia haina siri alikuja kujua na hatukuja amejuaje.
Siku hiyo alipiga kelele na kuzimia zaidi ya mara tano hali ilikuwa mbaya sana kwake. Baada ya hapo alikuwa mtu wa kujifungia ndani na kulia huku akiwa na picha ya mume na mtoto wake. Nguo za mtoto wake zilikuwa pembeni yake mdoli wa Ilham alikuwa pembeni yake. Mwisho wa siku Shania alishituka kabisa akawa wa kuzurura na ule mdoli na kuupa jina la Ilham. Tulijitahidi sana kumzuia asitike lakini hatukuweza tulimuacha tu uzuri alikuwa anatupa. kuanzia asubuhi usiku anarudi na kama hajarudi tulikuwa tunaingia mitaani kumtafuta na uzuri alikuwa anafahamika hivyo tulikuwa zinapigiwa simu kuambiwa yupo sehemu fulani.
Kwakuwa tuliishi wa, hatukuwa na pesa hatukuweza kumzibia Shania ndio hivyo akawa kichaa mazima.
Shahidi alishusha pumzi huku akikubali kichwa
chake.
"Poleni sana shangazi. "Tumeshapoa baba yote ni mipango ya Mungu.
Shangazi nakuahidi nitapambana na Shania kwa hali yoyote mpaka awe sawa. Sio kwa pesa tu bali hata kwa dua na maombi nitakesha nikiomba kwaajili yake. "Asante baba wewe ni mtu mwema sana Mungu akubariki.
*Alibariki sote. Shangazi acha niende niende. nikamuangalie.
Shahidi alinyanyuka na kuondoka.
Offer offer offer
Soma yote kwa sh 800
WhatsApp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni