VYOTE NDANI GONGA94
MR GENERAL : KUMBE ULINIPENDA EEE SEHEMU YA 11
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Basi nikajinyanyua na kumkiss kwenye shavu, akanivuta kisha akanipa French kiss moja matata kisha akasema “Mimi ni mume wako, hakuna mwanaume hata mmoja kwenye hii dunia ambae anaruhusiwa kukushika hata kucha, sasa jifanye mwenda wazimu, wewe na huyo nitakae kukuta nae mtanijua mimi ni nani, kisha akaondoka zake….
Nikaanza kujiambia kuwa, ukisikia mapenzi ya kibabe basi ndio haya, mwanaume mbabe kama kitu gani, nikajikokota pale kitandani taratibu na kuelekea bafuni, nikiwa bafuni nikaanza kupata wazo, maana kwenye harusi niliambiwa kuwa naolewa kwa niaba ya Eric, na huyu kaka mjeda ameniambia yeye ni Eric, na kuna muda ananiambia kuwa yeye ni mume wangu, nikawa najiuliuza, au mambo yote ambayo anayafanya ni kwa sababu ananipenda na ameniona nini, sasa kama ameniona anashindwa nini kunambia kuwa yeye ni mume wangu, kuliko kuniweka kwenye fumbo gumu kiasi hichi…
Na kama kweli yeye ni mume wangu, je Yule mzee ambae alinioa alikuwa ni nani, na nani ambae alimpa taarifa kuwa naolewa, maana sikuwah kuwa na ukaribu nae hata kidogo na sikuwah pia hakuwah hata kunambia kuwa ananipenda hata mara moja, kuanzia aliponirudishaga nyumban kwetu kibabe ule wakati ambapo nilikuwa natoka sokoni sikuwah hata mara moja kukutana nae, wala kuongea nae jambo lolote lile…
Nilikuwa najiuliza maswali ambayo hata mimi sikuwa na majibu yake sikuwa najua hata napaswa kujibu nini kwa maswali kama hayo, sikuwa najua pia natakiwa kufanya nini ili kuhakikisha kuwa najua hisia za kaka mjeda na siri zilizojificha ambazo sikuwa nazifahamu kabla…
Basi siku hio nikaanza kuangalia nguo ya mitego ila hata sikuipata hata moja, ikabidi nimtumie sms kuwa natoka naenda dukani, hakujibu, akaja kupiga nipo dukani, na kuniuliza “Upo duka gani?..
Ikabidi nimuambia ila akakata simu, sikuwa najua kama alikuja au alimtuma mtu aje kuniangalia maana sikuona mtu yoyote. Nikanunua cha kununua, hapo nikanunua vigauni vifupi vya mitego na mambo mengine yanayohusiana na kumtega mwanaume vizuri, na baada ya hapo nikanunua manukato mazuri na mafuta ya masaage, hapo hata massage yenyewe sijui namna ya kuifanya …….
Basi nikarudi nyumban nikapika hapo, nimemaliza nikatenga chakula mezani baada ya hapo nikaingia mtandaoni kujifunza namna ya kumfanyia mtu massage maana hakuna kitu hata kimoja nilichokuwa nakielewa wakati ule….
Baada ya hapo nikajiandaa na mimi vizuri, kaka mjeda alirudi kwenye saa tano kasoro, nikawa ukumbin namsubiri, kwanza sikusikia hata gari lilivyoingia nashangaa tu mlango unafunguliwa na mtu anaingia, nikasimama na kwenda kumpokea, sasa kwa namna nilivyovaa ni kama alikutwa na butwaa, kisha kwa sauti ya mideko nikasema
“Pole na kazi na karibu ndani mume wangu….
“Happinesss usiniambie kuwa kuna mwanaume wako ulikuwa umempanga aje hapa ndani saa hizi, yan aje nyumban kwangu, embu nambie ndio Yule mpuuzi wa kwa shangazi yako, au ulijua leo sitarudi ili ufanye mambo yako…
Nikaanza kumshangaa huyu vipi, kisha nikamsogelea na kumkiss kwenye lips zake kisha nikasema “Hakuna mwanaume ambae namsubiria mume wangu, nilikuwa nakusubiri wewe tu, naomba usiongee sana, nambie unakula kwanza au unaenda kuoga…
Ni kama kaka mjeda hakuwa amesikia ninachokisema, akaniangalia kwa mshangao kisha akaanza kuingia kwenye vyumba kana kwamba kuna kitu anatafuta, nikawa namshangaa huyu vipi, au ndio ameshachanganyikiwa saa hizi…
ITAENDELEA,……….
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mr-general-kumbe-ulinipenda-eee-sehemu-ya