VYOTE NDANI GONGA94
MTOTO HUYU NI WA NANI? Wanawake wawili mkubwa na mdogo walikuwa na watoto wawili wakiume!
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Walipowaacha kidogo mbwa mwitu akaja na akaondoka na mtoto mmoja!
Waliporudi kila mmoja akasema yule mtoto aliyebaki ni wake!
Wakaenda kwa Nabii Daudi Awahukumu, Akahukumu kuwa mtoto aliyebaki ni wa mwanamke mkubwa!
Mwanamke mdogo hakuridhia, wakaenda kwa Nabii Suleiman mwanawe Nabii Daudi!
Nabii Suleiman akaagiza kisu akasema kwa vile hamukuridhia hukumu ya Baba yangu na munataka hukumu yangu basi nitamkata mtoto huyu vipande viwili kila mmoja nitampa kipande chake!
Akawauliza munaridhia sasa hukumu hii? Mwanamke mkubwa akasema ndio na mwanamke mdogo akasema hapana nimeridhia hukumu ya Baba yako mtoto ni wake!
Mwanamke mkubwa akafurahi na Nabii Suleiman Akahukumu kuwa mtoto ni wa mwanamke mdogo!
MAFUNZO:
Mtu kama kitu ni chake na haki yake atakigombania kwa nguvu zake zote!
Isipokuwa akihisi atakipoteza basi atahakikisha kinakuwa katika mikono salama!
Wakati anakigombania hatokubali kabisa kukidhuru kwa sababu ni chake na yule asiyekimiliki hatojali kwa sababu yeye sio chake!
Atakisamehe tu kwa sababu kukisamehe ndio njia pekee ya kukibakisha salama kwa sababu anakipenda!
Mwanamke huyu mdogo aliridhia mwanawe achukuliwe na mtu mwengine ili tu abakie hai kwa sababu ni mwanawe na anampenda hawezi kuvumilia machungu ya kumpoteza mbele ya macho yake!
Mwanamke huyu mkubwa hakujali kama atakatwa vipande viwili kwa sababu sio wake na haumii/haathiriki kumpoteza kwa kuwa hana mapenzi nae!
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mtoto-huyu-ni-wa-nani-wanawake-wawili-mkubwa-na-mdogo-walikuwa-na-watoto-wawili-wakiume