MWARABU HUKO MI SIJAZOEA 25 -- 26
Ile sim ya shangazi wala haikunistua, nilishazoea lawama mie, nilimuacha aongee hadi alivyochoka yeye akakata cm, nikatafakari yale maneno ya Mahamood, kuwa huyu ndugu yangu kaja kwangu kwa nia mbaya,, na nilivyoona zile dawa kwenye begi la roby niliamini kabisa kuwa shangazi hana nia nzuri na Maisha yangu,, nilimpigia cm Kaka yangu nikamueleza kila kitu kinachoendelea, alinishangaa sana, akaniambia Mamujee hayo yote umeyataka mwenyewe, iv hao watu kwa wema upi waliokufanyia hadi una waweka karibu yetu?? Nilikwambia tangu mwanzo achana nao,, akaniambia subiri kwanza,, akakata cm,, kumbe akampigia cm shangazi akamwambia achana na Mamujee please, ni ndugu yangu, kama umeona hakuna umuhimu wa kutupenda bc tuachee,, Kaka akanipigia cm, akaniambia shangazi akinipigia cm nisipokee, nikamwambia sawa,, niliendelea na Maisha yangu , Mahamood tulizidi kuwasiliana na alizidi kuwapenda wanae sanaa,, ilipita kama miezi miwili iv Mahamood bdo yupo Dubai kwa mke wake, alinipigia cm akaniambia ananifanyia mpango wa visa na passport ili niende huko nipeleke watoto akawatambulishe ndugu zake maana asilimia kubwa ya ndugu wa Mahamood wapo huko,, nikamwambia sawa,, ila nilikuwa muoga mnoo but sikuwa na jins lazima wanangu wapajue kwao , akaniambia nichague Dada mmoja kwa ajili ya kunisaidia watoto, namshukuru Mungu sana Dada zangu wa kazi wote nimeishi nao vzr kama ndugu zangu, yaan ukifika kwangu huwezi kumtambua Dada wa kazi ni yupi na ndugu ni yupi,, nikamchukua yule nilietoka nae Arusha kwa Kaka, tukaandaa picha kila kitu Mahamood alimuagiza mtu akawa anashuhurikia hilo jambo,, nilitafuta mlinzi wa getini kutoka kwenye kampuni ili nikiondoka niache usalama nyumbani kwangu,, nilimtaarifu Kaka yangu kuhusu safari, alinitakia kila la heri,, bc tukaendelea kusubiri vitu vikamilike ili tuondoke,,, nakumbuka siku hio nipo tu nyumbani kwangu nilikuwa nafua,, huwa nafanya kazi za nyumbani kwangu japo kuwa nina wasichana wawili, napenda sana kufanya kazi,, cm yangu ikaita kuangalia namba ngeni,, nikapokea nikasikia sauti ya mwanaume,, Halow Amamu hujambo?? Nikamsalimia vzr, nikamuuliza nani mwenzangu?? Akaniambia mm ni Baba yako mdogo nikamsikiliza,, akaniambia yupo dar amemleta mtoto wake hospital ya oshen rod anasumbuliwa na kansa, walikuwa Bugando hospital Mwanza ndipo wamepewa rufaa kuja huku,, na amepimwa amekutwa na kansa ya utumbo nikampa pole,, akaniambia anaomba akutane na mm tuongee vzr,, nikamwambia sawa ila nitakujulisha,, nilishangaa sana, nikajiuliza namba yangu kapata wapi,, nikapata jibu ni shangazi tu,, nilikumbuka kile kipigo cha mbwa mwizi alichonipiga hadi nikapoteza fahamu,, wakaniburuza hadi chumbani,, mhhhh!! Dunia hii jamani, haina mwenyewe kwa kweli,, leo hii Amamu mm najulishwa kwenye matatizo,, mhhhh,, nikasema hapa nikimwambia kaka hili Jambo, atampandia gari amfate maana ana uchungu nae sana huyu Baba mdogo, nikanyamaza zangu,, na wao pia wanamuogopa matatizo yao yote wanaleta kwangu mie mnyonge wao,, bc niliendelea kusubiri vitu vikamilike vya safari yetu,, ikaisha kama wiki mbili, sijamjulisha Baba mdogo kitu chochote wala sim sijampigia,,, Mahamood alituambia kila kitu tyr tujiandae kwa safari wiki inayofata tunaondoka, bc tukazidi kufanya maandalizi mimi na Dada, huku tunacheka wenyewe na Dada, tunaambiana huko kwa waarabu tutaenda kuongea vp na watu bc tunacheka wenyewe,, mara tunaulizana iv tukichunwa ngozi jee tunachekaa huku tunajipa moyo, bhana wee liwalo na liwe
Safari iliwadia ilibaki kama cku tatu iv,, nipo zangu kwangu napiga story na madada zangu pamoja na mlinzi,, tupo nje,, nakumbuka siku hio tulikuwa tunabishana Kati ya Diamond na Kiba nani mkali wawili wanamtetea kiba, wawili wapo kwa Mond,, yaan tuligawana, bc ikawa kelele tunabishana haswa,, gafra geti likagongwa,, mlinzi akafungua kuangalia, wakaanza kujitambulisha, maana mlinzi alikuwa mgeni,, akaniuliza niwaaingize? Wanasema ni shangazi yako,, nikamwambia waache wapite,, jamani jamani,, alikuwa shangazi,, Baba mdogo, Roby,, eti wamemleta Baba mdogo nyumbani kwangu aje akae kwa kipindi chote anachouguza mtoto wake, na niwe nampa nauli kila cku ya kutoka Salasala kwenda oshen rod na ya chakula chake na mgonjwa,, kiufupi niwahudumie,, niliwasikiliza vzr hata sikujibu kitu,, nikamwambia Dada awape chakula,, nikaingia chumbani kumlaza mtoto alilala,, nikampigia cm Kaka nikamueleza kila kitu,, akaniambia waache hapo hapo usiwaambie chochote,, Naanza safari mda huu kuja huko,, nataka nionane nao mwenyewe,, usiwaambie chochote kama mm nakuja maana watakimbia,,
Itaendelea
NILIVYOANZA KUINGILIWA KINYUME NA
MAUMBILE
sehemu 26
Jmn wanawake wenzangu nimepitia Coment zote leo, najua wengi wananilaumu kuwa mm nashindwa kujitetea mwenyewe,, kiufupi mm sio muongeaji sn,, tangu nikiwa mdogo najulikana na ndugu wote kuwa Amamu sio muongeaji, nimerithi kutoka kwa Mama yangu, alikuwa mpole mnoo,, ndugu wa Baba walimfanyia kila aina ya vituko lkn Mama yangu hakuwai kunyanyua mdomo,, bc nimerithi kila kitu cha Mama yangu na iv watu wanasema cha kurithi kinazidi bc naona mie nimezidi
Bc nikarudi sebleni baada ya kuongea na Kaka,, nikawakuta wageni bado wanakula,, yaan Roby ndio kamuona Mama yake ndio anazidi kufanya makusudi, mara ashike hiki mara aulize hiki yaan ilimradi tu,, Mara da Amamu nifundishe kuendesha gari kwa gari yako,, au nimpigie rafiki yangu aje kesho anifundishe,, nikamjibu usijali nitakupa,, tumekaa tunaongea namuona Baba mdogo jicho halitulii Mara kangalia huku mara kageukia huku yaan anaonekana ni mtu mwenye maswali mengi kichwani kwake,, nilikaa zangu kimya nawaangalia tu,, ucku umefika nashangaa shangazi na mwanae hata hawaagi kuondoka maana walisema wamemleta Baba mdogo?? Nikashangaa hadi saa nne bdo wapo nikamuita Dada nikamwambia akaandae chumba cha mgeni wa kiume,, hao wengine watalala nao chumbani kwao,, niliwaaga nikawaambia naingia kulala,,, shangazi akaniambia na wao watakao hapa ili asbh tuwahi hospital kwa pamoja nikamwambia sawa,, nikaingia zangu chumbani kwangu,, niliwasiliana na Mahamood kama kawaida huku alinishangaa nisibebe minguo mingi nichukue chache au nisibebe kabisa eti kwenye ndege mizigo inapimwa uzito sasa nisije acha mizigo mingine airport,, bc tuliongea mengi ila sikumwambia kuhusu ule ugeni,, nilivyomaliza kuongea nae nikampigia Kaka nijue kafika wap maana ilikuwa kama saa sita ucku IV, akaniambia ndio anaitafuta charinze,, bc nikamwambia Mungu amlinde nikalala zangu
Asbh kumekucha hata sebleni sijashuka Roby kanifata chumbani,, eti Dada fungua,, nikamuuliza vp kwani?? Eti Mama kasema muanze kujiandaa,, hata sijamjibu na mlango sikufungua nikaendelea kulala,, mara mlinzi ananipigia cm, kuna mgeni getini amejitambulisha ni Kaka yako, nikamwambia aingie, bc kaka akawa amefika kwangu tyr, nikashuka hadi chini, nilifurahi sana kumuona Kaka, akaniuliza vp huyo Baba yako mdogo yupo wp?? Nikawaambia chumbani, akasema nenda kamwambie namwita nikamwambia atatoka mda c mrefu , hadi shangazi yupo hapa,, akasema na shangazi kalala hapa?? Nikawaambia ndio,, akasema kwa sauti,, HUU UKOO MASIKINI HUU nikamwambia Kaka usiseme ivo watasikia,, akaniambia unamuogopa mtu??? Mara shangazi anashuka kwa mbwembwe mwenyewe huku anaimba ( nimeuona mkono wa Bwana nimeuona) ghafra anakutana uso kwa uso na Kaka eti Mwita umelala hapa?? Upo dar hii hii?? Yaan Mwita hajajibu hata swali moja tyr kashamuuliza kumi Mwita akamjibu nimekuja leo,, Mara Baba mdogo nae huyoo,, alivyomuona Mwita akawa mpole,, eti shangazi ananiambia mie, Amamu bado haujajiandaa, nikawaambia bado,, Kaka akauliza kwani mna safari asbh yote hii?? Akasema ndio, Obara anaumwa amelazwa oshen rod wiki ya tatu sasa amegundulika ana kansa ya utumbo,, Kaka akasema sasa Amamu ndio anahusika nn huko hospital?? Shangazi kabla hajajibu, Kaka akamwambia, shangazi iv kwa nn mnapenda sanaa kunyanyasa watu?? Huyu Amamu ana watoto wadogo bado mbaya aende huko kwenye magonjwa ya hatari hatari aje alete shida kwa watoto?? Shangazi akasema amna sio lazima aingie ndani,, Kaka akamwambia shangazi sikia,, huyu Mamujee haendi kokote,, iv we Baba mdogo unakumbuka ulivyompiga huyu Amamu kiasi cha kutaka kumtoa uhai wake?? Sasa ungemuua leo hii ungelala nyumba ya nani? Nani angekupeleka huko hospital?? Baba mdogo kimya,, akamgeukia shangazi, akamwambia shangazi naomba muachane na Amamu please, mumempitisha kwenye shida mnoo na mateso, leo Mungu amempa nafuu bado mnamfata tena? Shangazi akasema Mwita mwanangu, tusikumbushe yaliyopita tugange yajayo,, Mwita akasema yajayo ndo kumfata fata nyumbani kwake? Iv hamuoni hata aibu kuja kujazana hapa? Mnadhani mumewe Amamu atawachukuliaje? Bc walijitetea ila aibu ikawashika,, Kaka akamuuliza Baba mdogo kwani ulivyotoka nyumbani kuja hapa dar ulimtaarifu amamu kama unakuja dar?? Akasema hapana,, Sasa kwa nn unamwambia kwa kumshtukizia kuwa unakaa kwake?? Ba mdogo, kimyaa,, Kaka akawaambia hapa kwa Amamu hakai yeyote kila mtu atakaa kwake au alipofikia, kama msaada unahitajika bc niambieni mm sio Amamu,, acheni kujitia aibu,, mnajidharirisha tu,, mhhhh Kaka aliongea jmn wote kimya,, Kaka akanigeukia mm,, ww Amamu sio unapokea pokea watu tu hapa kwako, umeolewa juzi tu leo mumeo anakuta ukoo wako wote umejaa hapa c atakuzarau?? Acha huruma ya kijinga, hapa mjini kila mtu apambane na familia yake heee Kaka anaongea kihuni tu bc walikubaliana shangazi amchukue ndugu yake akae nae kama misaada tutamsaidia huko huko
Bc tulipanda gari ya Kaka hadi hospital tukamuona mgonjwa kweli hali mbaya
Kaka akasepa zake nikarudi zangu kwangu
Safari ikawadia haoo tukaondoka zetu Dubai
Itaendelea
Soma mpaka mwisho kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni