PILOT SITAKI INANIOGOPESHA 1 - - - - - 5
Kwa majina naitwa Lailat Nina miaka 20 nilikuwa naishi Tanzania ila baada ya kumaliza Kidato cha sita wazazi wangu wakanipeleka USA Kwa dadaangu mkubwa. Siwezi sema familia yetu maskini kwasababu nimesoma shule za pesa nyingi sana na sio Mimi tu hata dada zangu wawili wa mwanzo, ambapo mmoja wao alisoma nje ya nchi na akagoma kurudi nyumbani kwasababu alishapata Hadi kazi uko na anaendelea na maisha yake na uyu dadaangu mwengine anaishi Dar es salaam na wazazi wetu yeye ni mkaksi sana Yan sio kama dada Jully ambae yupo marekani uyu Jiana ni yupo serious muda wote ndo maana hata simfagiri Sanaa.
Shule niliosoma Mimi nilichagua masomo kidogo na michezo kwa sana na Nina kabody flani hivi amazing ๐, alafu Nina karangi mashaAllah Kam mnavyojua sisi kabila letu ni wamburu basi mambo ni๐hatujawai kudisappoint kwenye sekta ya uzuri na pia najua kuzungumza Lugha sita za nchi tofauti tofauti ukiachana na kiingereza maana iyo ni Lugha common sana hata shule tulikuwa tunaitumia kwaiyo izo nyingine ni sita.
Kama nilivyowaambia sasahivi nipo marekani na dada Jully, uyu dadaangu ni mvivu sana Yan hata sijui uko kazini wanamlipa kwanini ๐คฃ alafu nilisahau kuwaambia uyu dadaangu anafanya kazi kwenye shirika la mambo ya Anga. Siku iyo nilikuwa zangu nyumbani dada kaenda kazini, nimekaa naangalia tv uku nakula popcorn ๐ฟ Nacheka mwenyw na movie kama chizi ๐คฃdada akapiga simu ghafla nikashangaa maana sio kawaida yake na hata Mimi nikimpigiaga ananifokea anasema kazini kwao haruhusiwi kushika simu ila Leo kanipigia muda wa kazi, somehow nilishangaa ila nikaipokea.
Hata salamu hakuna akaniambia tuu mdogo wangu ingia hapo ndan kwangu chagua nguo nzuri nzuri ya kukushape alafu ivi unaweza kuvaa viatu virefu kwel nikamjibu ndio akasema basi chap vaa hapo kagauni kakukushape vaa na viatu virefu, alafu kaa hapo njee Kuna gari linakuja kukuchukua baada ya dakika 20 kutoka sasa. Yan kabla sijamjibu kashakata simu, aaah nilikasirika ๐กsababu kamovie kangu kalikuwa kameshanoga Yan mpaka Raha alafu ni vile vipindi kikikupita kishakupita kwaiyo nilikasirika ๐ก ila sikuwa na budi. Nikafanya kama alivyoniambia nikatoka njee nikakuta hata gar lenyew halijafika nikazidi kukasirika baada ya dakika Tano ndo gari likafika sikutaka hata kuongea nae maana plate number zake nilitajiwa kwaiyo nikafungua mlango akaanza kuendesha na hamna hata aliemuongelesha mwenzie.
Baada ya kama nusu saa tukafika kwenye jengo kubwaa zuri na limedesigniwa kama ndege flani ivi ukiangalia Kwa haraka haraka utasema ilijengo linadondoka, Kwa jinsi nilivyokua nashangaa mpaka yule dereva akaniambia miss funga mdomo ๐คฃ๐คฃ nikamuangalia hapo ndo nikaanza kumuuliza Kwan hapa wapi akasema kazini Kwa dadaako, nikamuuliza na wewe Nan maana hata hufananii kama ni dereva upo smart ๐ค, akasema mm ni mtu tuu ninaejuana na dadaako nikamjibu aaah kumbe akaniambia twende nikupeleke nikamwambia sawa mkaka wawatu akashuka haraka ili aje kunifungulia mlango Mimi sasa na kiherehere changu nikajifungulia mwenyw mlango yule mkaka akaishiwa Hadi pozi ๐คฃ๐คฃmaana nimemkata stimu akaniangalia mpaka nikajishtukia nilivyochizi nikaingia Tena kweny gar ili anifungulie mlango sasa , Yan mpaka yule mkaka akaniuliza Kwan we unamiaka mingapi nikakaa kimya ๐คฃ maana kaniona mtoto.
Ikambidi anifungulie mlango tu Kisha akaniingiza kweny like jengo, Mimi kazi yangu nikushangaa tuu, mpaka nilivyofika ofisi Kuna watu kama ishirini wabab ndo wengi wamevaa suti na wadada Wachache dadangu akiwa mbele, Yan ni vile mtu anaingia sehemu alafu all eyes on you ๐คฃ mpaka nikataka kurudi nyuma maybe nimeingilia kikao cha watu ila yule mkaka niliekuja nae akanishika mkono akanipeleka mbele kabisa kweny Ile board ambayo projector ๐ฝ๏ธ inamulikiaga.
Mbaba mmoja akaniuliza kwa kiFaransa Jina lako Nan Binti, hata sikujua kama kauliza kwa kiFaransa nikaitikia vzuri tuu naitwa Lailat, akaniuliza kwa kiphilipino unamiaka mingapi hapo ndo nikajua kumbe mara ya kwanz nimeongea kumbe kiFaransa.
Itaendelea....
SEHEMU YA 2
Nikamjibu kwa kifilipino kama alivyotaka nikamwambia Nina miaka 20. Yule mbaba akaniambia unaweza ukatoka njee. Eeeeh๐ณ Kwan awa vipi nafika njee nikachukua simu nimpigie dada maana alikuwa kule ndani Bado, kabla hata sijaipiga dada akatoka njee akanishika mkono nikamuuliza Kwan dada Kwan ni Nini kinaendelea akaniambia kuwa na subira mdogo wangu nikamuuliza Tena sasa huku unanipeleka wapi dada Wala hakunijibu akanipeleka kwenye chumba kina vitu kama miti mirefu wakaja wadada watatu nikaambiwa nivue nguo nikawa sitak ila dada akaja akaniambia usiogope bwana na wewe Kwan unadhani wanapanga kukumaliza au embu vua nguo izo nikawa Sina budi nikavua wakaanza kunipima unene wa hips urefu na sijui magonjwa walinipima na kuangalia kama Nina tattoo hata siwaelewi Mimi walivyomaliza nikaruhusiwa kuvaa nguo nikaambiwa nikae njee.
Baada ya dakika 10 dada akaniita kweny kiile chumba nilichoingia mara ya kwanza mpaka wakaniuliza Kwa lugha zingine yule mbaba naona yeye ndo boss sijui maana Kila kitu anaongea yeye akaniambia Lailat Johnson Wambura umeruhusiwa kuanza kazi rasmi na sisi kuwa kama muhudumu wa ndege zetu za air fryer. Nikabaki nimeshangaa tuu sasa walivyomaliza kuongea nikataka niongee na Mimi maana sikupendezwa na kujiamulia kwao ila kabla sijaongea nikaambiwa na dadaangu nisome kwanza mkataba wao nikaona aah ngoja nisome tuu nionekane msomi nakataa kitu baada ya kukielewa.
Nikafika kwenye sehemu ya mshahara sasa, loooooh sijui kwann nilikuwa nawaza kukataaa ๐๐ maana nimekuta mshahara Kwa mwezi ni millioni 4.5, kwanza nikaanza kucheka mwenyw na dadaangu alijua tuu kwa jinsi ninavyopenda ela mm, nikaulizwa je upo tayr Mimi ni nani nikatae nikajibu chap na nikauliza naanza kazi lini nikaambiwa kesho alafu Leo utapewa uniform na ratiba zako za kesho nikajibu sawa dada akaniambia nitoke njee mara moja yeye akabaki anaongea nao.
Nilivyotoka njee nikawazaaa nikaona Bora niwajurishe nyumban, baba alifurahi baada ya kusikia hivo akasema Yan Bora watoto wangu wote hawategemei mambo ya urithi wanajimanage na kujiendeshea maisha wenyw, wazazi wangu wakanipa baraka nyingi sana mpaka nikaona kuwa nimefanya uamuzi mzuri. Baada ya kama dakika 5 dada akatoka tukaenda sehemu akanipa begi kubwa la nguo nikamuuliza la Nini akaniambia ni nguo zako za kazi, khaaaa๐ณ mbona mizito ivo akasema embu acha ushamba na ww sio nguo moja iyo ni nyingi za kuvaa majira tofauti tofauti. Aaaaah kumbe ๐.
Nikabeba mafurushi yangu tukatoka njee na dada yule mkaka alienileta ambae mie namuita dereva akaja nikaona kazubaa zubaa nikamuita we dereva mbona umezubaa ivo siunisaidie kuweka begi kweny buti, dada akanifinya namuuliza Nini sasa akaniambia wewe uyo ni boss wa department ninayofanyia kazi. ๐ฏ๐ฏNilikuwa surprised kidogo sasa kama ni boss mbona anajituma hivi Kuna nn hapa kati ya hawa watu ๐, nikamuweka dada kipolo baadae tulivyofika tuu nyumban nikaanza na taarifa za boss wake namuuliza Kuna Nini kati yake na boss wake ๐๐ mbona siwaelewi.
Mimi nimezoeana sana na dadangu kwaiyo mambo yake mengi huwa ananiambia na Mimi yangu mengi huwa namuambia pia so hakuona chakuficha akaniambia uyo boss wake anaitwa Jayson na alishawai kumtongoza nikamuuliza vipi umemkubalia akasema hapana, Hiiiiiii huyu vipi huyu mkaka handsome vile ๐ khaaaa ๐. Nikamuuliza sasa dada wewe unataka mwanaume atoke wapi kama uyu Mungu kamleta ila we bando unamringia sasa unataka Nini weee๐ณ.
Dada alivyoona mada zinazidi akanikatisha kwakisingizio nikalale kesho kazini nisije nikavimba macho natakiwa nipate usingizi wakutosha ๐ฉnikamuuliza kwaiyo Leo siangalii movie za usiku, nilivyosema hivo ni kama nilimwambia dada Leo ntaangalia movie usiku kwaiyo toa nyaya zote ๐๐ maana aliinuka akatoa nyaya zote za TV akaingia Nazo chumbani kwake na Mimi nikapelekwa kulala.
Itaendelea...
SEHEMU YA 3
Kesho yake asubuhi na mapema dada akaja kuniamsha Kisha akachukua lile begi langu akanipunguzia nguo akaniwekea vitu muhimu pia akahakikisha nimevaa vizur na make up nikafanyiwa, ila nilipendeza mpaka nikawa najionea wivu, dada akaomba kwanza apige video call nyumbani maana ni siku yangu y kwanza kazini lazima nipate baraka za wazazi na kwel wazazi wakapokea simu nikaongea nao mama akanisisitiza niwe na heshima na niwe mkalimu tu uko kazini nikamjibu sawa, wakaniombea pale maan familia yangu na mambo ya dini ni Pete na kidole. Baada ya kuombewa tukaita Uber mpaka kazini ila nikashangaa dada akanipeleka kwenye ofisi zingine kabisa tofauti na anazofanyia yeye kazi Kisha akataka kuniacha pale njee ya izo ofisi nikamuuliza dada vipi mbona unanitelekeza ๐.
Akanijibu fomu muhimu zote izo hapo we nenda ukajieleze mwenyw uko ndo kazini kwako nenda pale mapokezi mpe izo atakuuliza maswal baadhi Kisha utaruhusiwa Mimi naenda kazini kwangu nshachelewa. ๐ณ๐ณ hii jamni dada Mimi siwezi kujielezea nilivyomwambia ivo dada Kuna mtu akatusikia mkaka tuu kavaaa kawaida ila ni mzur akaaanza kunicheka nikamgeukia Kwa hasira, nikamuuliza sasa na wewe unacheka Cheka Nini hapa yule mkaka akasema hapana nimefurahi nikamuuliza Kwan umeona Mimi nafurahisha hapa yule mkaka mstaarabu akaniambia basi samahani ila sikupanga nikukwaze dear.
Dada Hapohapo akamuita yule mkaka Kendrick naomba unisaidie kunipelekea mdogo wangu uyo uko mapokezi maana kama unavyomuona Bado mdogo hawezi kujieleza Kendrick akasema sawa. Baada ya kusema hivo dada akaondoka akaniacha na uyo mkaka nisiemjua kwakua nilikuwa mgeni sikuwa na jinsi nikakubali kuwa mnyonge yule mkaka akaniongoza njia mpaka reception. Tumefika pale reception yule mdada wa pale hakuwa na furaha hata, ni kama vile unamkuta mtu na furaha ila baada ya kukuona tuu furaha yote ikakata na sikujua ni kwanini. Nikamsikia anamuuliza Kendrick, boss unajuana na uyo Binti Kendrick akamjibu hapana nimekutana nae tu hapo nje, yule mdada akaguna Kisha akasema sawa nikajua mnajuana.
Baada ya Pale nikapelekwa kweny chumba kimoja hivi cha CEO maana pale njee wameandika CEO kweny kile kibango cha mlangoni nikaingia ndani sasa nikakuta Kuna mkaka mzuri Sanaa Tena zaidi ya Kendrick Yan mpaka nikawa nawaza hii kampuni ni ya majini au mbona Kila mtu ni mzuri hivi, nikasalimiana na yule mkaka akanipa ratiba zangu nikaambiwa nizisome nikpewa na Sheria pia nizisome, nikataka kuondoka ila yule mkaka akakataa akaniambia unaweza ukazisoma hapa hapa tuu. Mmmh sasa yule mkaka anaongea mm namuangalia lips ๐๐ ila shetani huyu ๐ alaaniwe na hata yeye pia Kuna muda nilimbamba ananitizama nikawa najichekesha tu kama mlevi mpya. Nikasoma pale ila hamna nilichokielewa zaidi tuu ya taarifa ilioandikwa Ninatakiwa kuwa muhudumu wa ndege ya sikuiyo itakayotoka usiku, maaan muda wote namuangalia yule mkaka Kwa kuibia ibia ๐mpaka nikafumaniwa kwasababu na yeye alikuwa ananiangalia yule mkaka akaniambia unaweza kuniangalia vizur jamani sio sawa kuniangalia Kwa kuibia, daaaah alivyosema ivo akanifanya nipatwe na aibu, nikajitetea hamna bhana nilikuwa sikuangalii wewe akasema mmmh sawa kama ulikuwa huniangaliii Mimi.
Nikasoma zile Sheria Nilivyomaliza akaitwa mdada mmoja hivi ni mzuri uyo na ni mrefu mithili ya twiga, umbo lake sasa Yan inshort she is hot ๐ฅanaitwa Racheal, akaambiwa akanielekeze maana Mimi sijasomea hayo mambo sielewi kitu ni mgeni kabisa na nimechaguliwa kwasababu ya kujua Lugha tofauti tofauti. Nikatoka nae tukaenda kwenye sehemu kuna ndege ya bandia ila kubwa naona ni ya mafunzo ya practical. Yule mdada akawa ananielekeza kupitia Ile ndege ananionyesha ntakavyotakiwa kufanya nianzie wapi na nimalizie wapi. Alikuwa akinifundisha uku tunapiga story akaniuliza Kwan unafahamiana na yule CEO nikamjibu hapana ndo nimemjua Leo akaniambia ujue kwanini nimekuulza ni kwasababu uyo kaka hanaga mazoea na mtu zaidi ya mdogo wake Kendrick ila Leo nimekukuta ofisini kwake na mnapiga story kabisa, nilivyosikia kamtaja Kendrick nikauliza Kendrick gani uyo akasema ni Rubani wa ndege zetu mkaka flani hivi ambae anagombaniwa na anaependwa na wadada wa kampuni nzima. Nikawaza au ndo yule alienileta ila nikajisemea yule mbona haonekani kama ni Rubani nikaamua kupotezea Mimi mambo Yao hayanihusu. Ila nikauliza yule CEO anaitwa nan maana ๐๐, Akanijibu anaitwa Freeman ila anamchumba wake tayari.
๐๐๐Uyu nae kwani nimemuuliza mm mbona anakiherehere. Nikamjibu sawa hongera yake.
Itaendelea..
SEHEMU YA 4
Tulivyomaliza pale nikaambiwa nikapumzike na nile ila sio sana nisije nikaonekana ninakitambi, nikakubali mida ikapita ukafika muda wa kukaribisha abiria nikaja kuamshwa maana mida ya kazi ishaanza Sasa jamani jamani Kuna wadada ni wazuri. Ao wafanya kazi wenzangu duuuh warefu na wanatembea kama twiga Wana madoido Hadi raha na wanajijua ni wazuri Mimi tu wakike binafsi nimeona ni wazuri๐. Wakaja mule ndani nilipo wakabeba mabegi Yao na mie nikafatwa na yule kiongozi tukawa tunaburuza sasa vibegi vyetu kuelekea kweny ndege, hamna moment ambayo mtu unapata bichwa kama hiii, unatamani hata uwapungie watu mkono maana ni mnatembea vizur Kwa madoido alafu Kila mtu anawaangalia unakuwa kama msaanii flani ivi pale airport ๐.
Tukaenda Hadi kwenye ndege mimi kazi yangu haikuwa kuhusu nchi hii, maaana route yetu ilikuwa inaenda France, tukifika huko Mimi ndo nakuwa incharge kweny kuongea kiFaransa, kwaiyo uku wakati wenzangu wanakaribisha abiria na kuwaelekeza, mie nikaambiwa niwahudumie na kuwasikiliza marubani na nikasaidizana na Jane na yeye ni muhudumu mwenzangu yeye alipewa kuhudumia business class, nikaenda sasa kule mbele Kwa marubani nikakuta moja wa Rubani anaepaisha ndege Leo ni Kendrick na uyo mwengine hata simjui nilishangaa ama kwel usimzarau mtu bila ya kumjua maaana mie nilivyomuona muda ule alivyokuwa kavaa baada huwezi zania kama ni rubani, Kendrick alivyoniona tuu akaniambia mrembo vipi ushaweza kujieleza maana upo business class kumbuka, alafu akaanza kucheka.
Yule mwenzie akauliza Kwan hawezi kujieleza Kendrick akamjibu Yan we acha tuu kwanza kaletwa kazini na dadaake, wakaanza kunicheka mie hapo nimefura nikaondoka Kwa hasira nikatoka mpaka alipo Jane uku nimenuna Jane akauliza shida nini kabla sijamjibu nikafatwa na yule alienipa maelekezo Leo akaniambia Rubani anakuita, ๐กuyu nae Nini. Jane alishangaa nikamuuliza na wewe nini akasema Yan unachukia kwenda kumuhudumia Kendrick nikamuuliza kwani vipi akasema Yan nisikufiche hapa wote sisi hamna asie na crush Kwa uyo Kendrick na hata Mimi ninampenda hatri sema tuu kupewa chance ya kumuhudumia na changamoto na nisikudanganye tumekusema sana kwanini sisi tupo muda wote uo hatujapewa iyo chance na nikwambie za chini chini tunaskia Rubani yeye mwenyw ndo kakuchagua.
Mmmh nilishangaa๐ณ, nikasema Amna bhan ila ngoja nikawasikilize ao watu uko nikatoka kwend Kwa Kendrick nafika kule nakuta sijui wanamuongelea mschan gani walikuwa hawajaniona, ila nikamsikia Kendrick anasema Yan uyu Binti sijui hata ntampataje Wallahi, napenda sana mabinti wa rangi nyeusi na nahisi ni muafrica Yan Leo ndo nimeamini Kuna love at first sight, mwenzie akaanza kucheka mm mwenyw nikaanza kucheka ndo wakanishtukia Kendrick alishtuka yule mwenzie nae alishtuka mie sasa ndo nshajua Siri ya Kendrick yeye si alikuwa ananitesa na yangu kuwa siwez kujieleza.
Nikamwambia aaaaah Yan mkaka mzuri handsome ila unashindwa kukoconfess feelings zako Kwa mwanamke ๐ซด๐, aibu yako ivi wazazi wako wanajua kwel wamezaa mkaka bwabwa๐ mtu handsome ila kujielezea huwezi khaaaaa shame on you.
Kendrick akaniangalia Kisha akaingiza mkono mfukoni kwake akatoa babrishi akaanza kutafuna Yan kama vile hakupenda ule utani, ila hata sikujali maana yeye mwenyw alikuwa ananitania vile vile kwanini nimtanie Mimi akasirike, nikaondoka zangu hata shida Yao sikuisikiriza.
Itaendelea....
SEHEMU YA 5
Wale ma airhostess wengine wakawa wanatoa maelekezo sijui watu wanatakiwa kufunga mikanda na pia waeke simu zao kweny aeroplane mode nakadharka, mie hata sielewi nipo sehemu ya kuandalia vyakula, Kwa muda ule nilipewa iyo kazi y kuhudumia vyakula ila upande wa kule first class. Yakapita masaa kadhaa na nilikuw nimechoka kama mbwa ๐ jamani izo kazi kweli zina wenywe. Yakapita masaa mengi Tena ndo tukafika France woiiii nilikuwa sitamaniki kwanza nywele zimevurugika maan nilikuwa nimezibana watu wakaanza kushuka, kwenye zile purukushane mie nikaambiwa nimpelekee ruban kahawa maana wao wanashuka kwenye ndege mpaka pale watu wote watakaposhuka.
Nikawa najisemea moyoni uyu Rubani mwenyw sinilikuwa nimegombana nae duuuh mbona mtihani huu, nikaenda nikawa nimekutana nae anaeleka chooni alivyoniona akasimama nikaenda mpaka alipo kabla sijaongea akanivuta chooni alafu akafunga mlango akawa ananiangalia kama mtu aliechoka macho yamelegea alafu anahema polepole, nikamuuliza Nini mbona ivo akanishika kiuno akaniambia sio kama siwez kujieleza Binti ila mambo mengine hayahitaji kuelezewa umeskia, sasa akawa anaongea ivo uku kanigandamiza pembez kweny Kuta moja ya choo nikawa nahemea juu juu aliponimliza akaja Kwa shingoni akawa anaongea sasa Ile hewa yake inatoka ya motomoto Ile ikawa inanitekenya shingoni, duuh Ile Hali mpaka macho yangu yakalegea ila uyu mkaka ni muhuni Sanaa jamni akashusha mkono wake akawa ananipapasa kiuno akawa anaushusha hivi karibu na kweny papuchi kama anaupandisha kiunoni ๐ซข, akamalizia na kunibinya kiuno nilipiga kelele flani ivi, Kendrick akaniachia Kisha akanipa kikaratasi cha chumba cha hoteli ambapo tunaenda kufikia, akaniambia baadae uje tuongee Kisha akaondoka.
Yan kwanza aliacha mule ndani nimekaa kweny choo maana siamini amini nimekaa najishika shingoo sielewi kimentokea Nini nikawa najihisi kama Kuna vitu vinatoka uku kweny papuchi kama mkojo sio mkojo nikashika simu nikataka nimpigie dada nimuulize maana nimezoeana nae sana sema nikapotezea sikumuuliza asije akaona Nina tabia mbaya Bure.
Nikajiweka vizuri nguo nikatoka kama sio Mimi ila Ile Kadi niliiweka kwenye mfuko wa sketi natoka nje nakuta watu washashuka wote wapo wenzangu wanajiandaa wengine washabeba mabegi na Mimi nikawa najiandaa ghafla akapita Kendrick nyuma yangu, nikabaki nimeduwaaa namuangalia tuu Jane akaniuliza vipi bidada mbona wamtizama Sanaa๐ฌ , nikaona nikamwambia aaah Kuna kitu tuu nimekumbuka sio hata issue kubwa. Akaniambia sawa, baada ya dakika kama Tano akaja mkuu wetu wa kazi Akatuambia muda wa kutoka sasa tukabeba mabegi yetu tukawa tunaondoka, tukaenda kusign maana tupo uwanja wa ndege wa watu baada ya process zote kuisha tukapanda gari kuelekea hotelini ili kujiandaa na safr ya kurudi ya kesho yake usiku Kwa muda up tuliokuwa tumefika ulikuwa ni usiku pia ila sio usiku Sanaa mida ya saa moja.
Tukapelekwa hotelini mule tukapewa vyumba kweny Ile hoteli Sheria zake jinsia moja hawawezi kushare chumba kwaiyo Kila mtu akapewa chumba chake na nilikuwa na kadi ya Pilot Kendrick mkononi ilikuwa imeandikwa chumba namba 390 ya VIP alafu yangu niliopewa pale mapokezi ili namba 300 ya kawaida, Nikaenda tukaweka vitu vyetu Kila mtu akaingia chumbani kwake Mimi sasa nipo nawaza niende au nsiende kwanza nikaenda bafuni kuoga nikajisugua vizuri nikawa nawaza sasa niende au nisiende.
Je nini kItaendelea.....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni