"Nenda wewe, unaonekana kuwa na shida sana ya kuzungumza na Mfalme... Mimi nitakuja kesho " Niliongea kisha ni katega mgongo nisepe.
Lakini Malkia Shamsa alinidaka mkono.
"Pamoja na yote lakini Mimi ndio Mke wake wa kwanza wa Mfalme. Naheshimika pande zote za hii Nchi" Malkia Shamsa aliongea.
"Unaweza kuwa una heshimika lakini ukapoteza nafasi ya kusikilizwa, wewe hapo tayari ushapoteza nafasi ya kusikilizwa " Niliongea kisha ni kaendelea na safari yangu.
Nilielekea malangoni kwa Mtabiri Mkuu, nilimkuta akifanya ibaada. Sikutaka kumsumbua nilikaa pembeni yake nikawa nafanya ibaada pia.
"Umekuja kwa wakati sahihi " Mtabiri Mkuu aliongea kisha akakaa pia.
Nilitega masikio kusikia ni kitu gani anataka kuzungumza na Mimi.
"Huko nje Raia wana changamoto sana, kuliko ushinde malangoni ukirushiana maneno na Malkia Shamsa au Malkia Ada itapendeza kama utatoka nje kusikiliza watu wako "
"Watu wangu?"
"Ndiyo, huenda ulikuwa hujui lakini Raia wa Taifa hili ni watu wako "
"Sawa, ingawa sijawahi kujifunza mambo ya siasa lakini nitajitahidi kadri ya uwezo wangu "
"Kusikiliza watu hakuna tofauti na unavyo sikiliza matatizo ya watu wa familia yako au marafiki zako. Mbinu ni zile zile"
"Kwanini umenichagua Mimi na si Malkia Shamsa"
"Miungu ndio imekuchagua na siyo Mimi. Kazi yangu ni kufuatisha kile miungu wanataka"
Nilifurahishwa na maongezi yake, kulivyo pambazuka asubuhi niliondoka pamoja na Vijakazi wangu na Askari ishirini kwa ajili ya usalama.
Haikuwa ngumu kama nilivyo fikiria. Nilizungumza na watu wangu kama navyoongeaga na watu wa familia yangu.
Nikiwa katika kuhojiana nao nilishtuka baada ya kumuona Mfalme akiwa kavaa nguo za Kiraia.
Alionekana kufurahia namna navyo endesha mambo.
Baada ya ziara yangu kuisha Mimi na yeye tulielekea Ikulu ndogo iliyokuwa pembeni kidogo ya Mji.
"Nina ujauzito wako " Niliongea.
Mfalme alinikumbatia kwa mahaba yote.
"Mimi na wewe tumewahi kuonana tulipokuwa watoto " Mfalme aliongea na hata ni kashangaa tumewahi kuonana wapi.......
ITAENDELEA..........
Maoni
You're not logged in
X
Login
X
signup
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
MIMI SIKUACHIπ₯° Sehemu ya 54 na 55
54 MPAKA 55 π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Aseeeee, nikaanza kuelezea mm. Akaja yeye. Ahaa aka...
49 MPAKA 50 π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘π‘ Basi nilimuacha kama mwez lemi anendeelee kumfatili...
"Nenda wewe, unaonekana kuwa na shida sana ya kuzungumza na Mfalme... Mimi nitakuja kesho " Niliongea kisha ni katega mgongo nisepe.
Lakini Malkia Shamsa alinidaka mkono.
"Pamoja na yote lakini Mimi ndio Mke wake wa kwanza wa Mfalme. Naheshimika pande zote za hii Nchi" Malkia Shamsa aliongea.
"Unaweza kuwa una heshimika lakini ukapoteza nafasi ya kusikilizwa, wewe hapo tayari ushapoteza nafasi ya kusikilizwa " Niliongea kisha ni kaendelea na safari yangu.
Nilielekea malangoni kwa Mtabiri Mkuu, nilimkuta akifanya ibaada. Sikutaka kumsumbua nilikaa pembeni yake nikawa nafanya ibaada pia.
"Umekuja kwa wakati...
π Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/usiku-mmoja-tu-alidata-sehemu-ya-19
Maoni