Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo
Gonga94 · Stories
27 Jan 2026
6 views
VYOTE NDANI GONGA94
Waarusha ni kabila la watu linalopatikana kaskazini mwa Tanzania katika eneo la mlima Meru, Mkoa wa Arusha
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
. Lugha yao ni Kiarusha inayohesabiwa kama lahaja ya Kimaasai[1]. Wakati wa kuja kwa wakoloni hao walikuwa wakazi wa eneo la mji wa Arusha wa leo.
Kuna mawazo mawili juu ya asili ya Waarusha.
Wengine wanasema asili yao ni kundi la Wamaasai walioshindwa katika vita kati ya Wamaasai na hivyo kutafuta kimbilio kati ya wakulima; walianza kulima wenyewe na hivyo kutofautiana na Wamaasai wengine.
Wengine wanasema asili yao ni Wapare waliohamia mlima Meru kufuatana na mapatano na Wamaasai. Hapo walianza kutumia lugha ya Wamaasai na kupokea desturi nyingine. Wakati wa sotoka kubwa ya 1892 Wamaasai ambao mifugo yao walikufa wote walijiunga na Waarusha na hivyo kuimarisha athira ya utamaduni wa Kimaasai kati yao.Waarusha walitokea meru.
Kwa namna yoyote katika eneo la mlima Meru Waarusha walikuwa majirani wa karibu na Wameru wanaosema kwa lugha karibu na ya Wachagga. Wameru waliwahi kufika Meru mapema wakakalia sehemu za juu zaidi mlimani wakati Waarusha walianza chini zaidi. Mwanzoni walipigana kati yao lakini baadaye walianza kushirikiana kwa karibu hadi mwaka 1881 Wameru walikaribishwa kuunga vijana wao katika rika mpya ya Waarusha iliyoitwa "talala".
Zamani ya ukoloni
Katika miaka ya 1880 wakoloni Wajerumani walianza kufika katika eneo la Kilimanjaro kati ya Wachagga. Wakati ule Waarusha walikuwa wakishirikiana na machifu wa Wachagga katika vita vyao. Waarusha ndio wenyeji wa jiji la arusha,ni watu wapole,wachapa kazi,wakarimu kwa wageni, Wastaarabu sana,ni wakulima na wafugaji .
Karibu Kilimanjaro TV tuendelee kukujuza mengi kuhusu Kaskazini
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
Cristiano Ronaldo anafikiria kuondoka kwenye Ligi Kuu ya Saudi msimu ujao. Ronaldo kwa mujibu wa ripoti yuko tayari kulipa kifungu cha euro milioni 50
zilizo kwenye mkataba wake na kuondoka Saudi kutokana na kile anachoona kama upendeleo kwa Al-Hilal. Ronaldo anasemekan...
Je wajua filamu ya Deadly Prey ya mwaka 1987 ilitayarishwa na David Trior ambaye alimpa nafasi ndugu yake Ted Prior kucheza uhusika mkuu(main character)
filamu iliyotengenezwa kwa bajeti ya chini sanaa kiasi mwanzo mwisho wa filamu jamaa alikuwa na kipensi tuu vibanda umiz...
Waarusha ni kabila la watu linalopatikana kaskazini mwa Tanzania katika eneo la mlima Meru, Mkoa wa Arusha
. Lugha yao ni Kiarusha inayohesabiwa kama lahaja ya Kimaasai[1]. Wakati wa kuja kwa wakoloni hao walikuwa wakazi wa eneo la mji wa Arusha wa leo.
Kuna mawazo mawili juu ya asili ya Waarusha.
Wengine wanasema asili yao ni kundi la Wamaasai walioshindwa katika vita kati ya Wamaasai na hivyo kutafuta kimbilio kati ya wakulima; walianza kulima wenyewe na hivyo kutofautiana na Wamaasai wengine.
Wengine wanasema asili yao ni Wapare waliohamia mlima Meru kufuatana na mapatano na Wamaasai. Hapo walianza kutumia lugha ya Wamaasai na kupokea desturi nyingine. Wakati wa sotoka kubwa ya 1892 Wamaasai ambao mifugo yao walikufa wote walijiunga na Waarusha...
👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/waarusha-ni-kabila-la-watu-linalopatikana-kaskazini-mwa-tanzania-katika-eneo-la-mlima-meru-mkoa-wa-a