MICHEZO YA WANAWAKE(WOMEN MIND GAMES) AMBAYO UNATAKIWA UIJUE KWENYE MAHUSIANO ILI USIINGIE MKENGE.
1. Wanaume wengi wamejikuta wakiingia katika kumi na nane za wanawake na kujikuta wakinaswa na mitego ya wanawake.
2. Mwanamke unapoingia naye kwenye mahusiano Hasa ha kimapenzi lazima akuchezee mind games(michezo ya akili) kama sehemu ya mitego ya kukunasa.
3. Wanaume wengi wamejikuta wakifeli mapema Kabisa. Na hapo ndio wanawake huwashinda akili wanaume wengi na kuwatawala.
4. Mwanamke akishakuchezea mind games ukafeli huwezi kumtawala tena. Yeye ndiye anakutawala. Wewe ni kirunguyeye tuu Mdogo mwenye miiba lakini huwezi kuitumia kama silaha.
5. Moja ya dalili mwanamke amekushinda kwenye Mind games na unatawaliwa na mkeo au mwanamke, ni kama pamoja na na dalili zifuatazo;
a) Anauwezo WA kukupimia na kukupangia kufanya mapenzi/ngono.
Mwanamke akishakuzidi akili na akikutawala utajua kwenye kukupimia michezo ya kitandani. Mwanaume mwenye akili na mtawala hapimiwi. Na hapohapo halazimishi. Yaani mwanamke anajileta mwenyewe na anatamani umuombe. Ukiona mwanamke anakuringia kwenye ngono ujue mitego yake na mind games alizokuchezea ulifeli.
b) Anajiamulia Mambo bila kumpa ruhusa.
Yaani unashangaa tuu kafanya, mara kakopa Sijui manini huko, haombi ruhusa. Hana haja ya kufanya hivyo Kwa sababu Siku zote mtawala haombi ruhusa. Kikawaida wanawake hujua wanaume watawala wasiotaka mchezo linapokuja suala la heshima na mamlaka ndani ya nyumba. Na yeyote anayeenda kinyume na kanuni anafukuzwa bila kusita bila kujali.
c) Anasikiliza wanaume au watu wengine kuliko wewe.
Mwanamke wako lazima akusikilize wewe iwe Kwa hiyari au kwa nguvu. Hawezi fukuza. Moja ya dalili mkeo amekushinda akili na ulifeli mind games zake ni kutokukusikiliza. Alishakupima akaona huna utakachofanya, huna lolote, huna mamlaka yoyote. Si chochote sio lolote.
Kwa Sisi Watibeli mwanamke asiyekusikiliza hapaswi kuwa mkeo hata kwa masaa 24.
6. Zipo sifa na dalili nyingi lakini kutokana sio mada Leo Acha niendelee na michezo ya wanawake ambayo unatakiwa uijue na uweze kuidhibiti ili mambo yako yaende sawasawa.
Kama ifuatavyo;
a) Mbinu ya Silent Mode. (Kujikausha)
Wanawake sio kwamba hawapendi, sio kwamba hawavutiwi na wanaume. Sio kwamba hawawezi kuchat na wewe. Nope!
Wanaweza. Ila wanatumia mbinu ya Silent mode au silent treatment kukuchezea akili yako.
Unakuta hakutafuti. Anataka uwe wa Kwanza kumtafuta.
Ukimtext anachelewa kujibu.
Anajifanya yupo busy ati hatakuwa na muda.
Huo wote ni Utapeli.
Lengo la Mind game hii ni kukufanya wewe mwanaume uwe mfuasi wake, umfukuzie, uwe kama mkia wake badala ya kuwa kichwa. Wanakutengenezea kitu inaitwa Chasing behaviour na wasiwasi.
Usimtafute kama hakutafuti. Kuwa busy na KAZI zako.
Usimtumie tumie text, pia usitume meseji ndefu.
Kumbuka huo ni mtego.
Asije kukudanganya unavyomtafuta mara kwa mara ndio unaonyesha Nia na kuwa upo serious nope! Watibeli hatufanyi hivyo.
Mtongoze, akikuambia yupo busy mwambie fresh, akimaliza akutafute. Kata simu tafuta mademu wengine zaidi na zaidi. Hii ni Kwa wanaotafuta wachumba. Usiwe na mwanamke mmoja kama hujaoa. Tena mwanamke huyo hajitambui na anataka umtafute tuu yeye. Au anachelewa kujibu text. Watibeli hatufanyi hivyo. Kuwa na Wanawake Lundo na usione aibu Kwa sifa hiyo. Asiyetaka akae pembeni.
b) Wanavuka Mipaka kimakusudi kukupima.
Mind games nyingine wanayotumia wanawake hasa mwanzoni NI kukuvunjia heshima kidogo kidogo kupima unajielewa, kujitambua na mamlaka yako unaweza kuitetea au kuilinda Kwa kiwango gani.
Anaweza kukuonyesha dharau, kuongea shit, au kuchelewa appointment mliyowekeana. Usikubali.
Mmeagana mnakutana saa 12 jioni iwe 12 jioni ikizidi labda dakika tano au kumi hivi. Tofauti na hapo hizo ni dharau. Cancel hiyo appointment. Mwambie Una mambo mengi ya kufanya. Usikubali kuvunjiwa heshima yako hata kama ni kitu kidogo. Hakikisha from beginning ajue wewe ni MTU unayemind vitu anavyoviita au ambavyo wengi wanaviita vidogovidogo.
C) Kutafuta Uhakikisho (Validation Fishing)
Hii ni tabia ya mtu kutoa malalamiko ya kificho na kijanja au kuonyesha kutokujiamini ili uweze msifia.
Mfano:
“Nahisi sifai…”
“Labda hunipendi tena…”
Lengo si kutatua tatizo, bali kuvua maneno ya kumbembeleza, kumtukuza, kutaka kumthibitisha yeye ni zaidi yako, kukuona kuna majukumu huyafanyi ipasavyo.
Wakati wewe muda huo unahangaika na unapambana kutimiza wajibu wako kama mpenzi au mume wake.
Msikilize Kwa utulivu. Usitake kutumia nguvu kubwa kuthibitisha chochote kuonyesha wewe ni mwema. Mwambie Kwa kifupi umemwelewa na utafanyia kazi hoja zake. Kama anatabia ya kulaumu laumu. Mwambie asikusumbue kama hayawezi aondoke. Hapo utaongea kama mtawala na sio kama Mwenza.
Familia inaendeshwa Kwa Utawala na Upendo. Lazima kuwe na uwiano.
d) Kusifia Wanaume wengine Mbele yako Makusudi.
Hii ni mind games ambayo wanaume wengi hufeli. Wanawake huweza kujifanya wanamuelezea mume wa Rafiki yake jinsi alivyo muwajibikaji. Akamsifia wee. Lengo lake ni kupima na kupandisha kiwango cha wivu wako.
Ukishafeli ukaonyesha wivu lengo lake la pili ni kuku remote ufanye anachotaka kwani utataka Ku prove wewe NI mwanaume Bora kuliko wanaume wengine.
Kufikia hatua hiyo UMEFELI Mtihani na umeshindwa mind game na mwanamke.
Hutakiwi kuwa na wivu au tuseme hupaswi kuonyesha wivu Kwa mkeo au mpenzi wako. Hilo ni kosa ambalo wanaume wengi wanalifanya. Wivu ni kiashiria upo controlled. Huwezi zuia mihemko yako.
Akisifia mwanamke mwingine, wewe mwambie aende kwa hao anaowasifia. Mwambie Siku nyingine akirudia kusifia wanaume wengine utampeleka wewe mwenyewe Kwa hao wanaume akakae huko. Au utamundoa hapo. Kisha kata hiyo mada leta Stori nyingine.
e) Kukusifia na kukujaza sifa za kijinga ili akutumie.
Wanaume wengi wamegeuzwa misukule na watumwa na wanawake Kwa kuzidiwa akili na wanawake. Mind games za wanawake hasa hii ya kukujaza sifa za kijinga ili uingie kwenye mfumo wa utumwa wanaitumia Sana.
Mfano, Wanakuambia mwanaume lazima utoe pesa, alafu anakupiga msumari. Unatoa. Chali. Unatoa elfu 50 Kwa demu wakati hujawahi kununua hata kiatu chako cha elfu 50. Wewe kama Sio chizi ni nani?
Anakusifia wewe ni mtoaji mzuri, wewe ni jembe, kumbe anakuona huna akili.
Hakikisha mwanamke anakuona unapenda pesa kuliko unavyompenda Yeye. Unapenda KAZI yako kuliko yeye. Hiyo ni kanuni.
Wanawake huwasifia wanaume insecure yaani wanaume wasiojiamini. Wasioamini uanaume wao. Kwamba uanaume wao unathibitishwa na maneno au kauli za wanawake.
Mwanaume anayejielewa huwezi kujazwa sifa na wanawake kijingajinga.
Mtego wa kukusifia na kukujaza ujinga lengo lake ni kupima kujiamini kwako. Kama unajiamini huwezi zichukua hizo sifa kwani unajua zipo intentionally.
Anaweza kukuambia, Juma wewe ndiye mwanaume SASA embu ninunulie Bia hapo. Lengo la kukusifia ni ili akupige kibomu. Kwa Sisi Watibeli hatutoagi pesa Kwa vipimo vya wanawake wajinga wanaotumia vipimo vya kitoto.
Kukupa pesa au kukununulia kitu haihusiani na uanaume. Hizo ni akili za wasiojiamini au wenye upeo Mdogo.
f) Kukuchokoza Kihisia (emotional provocation)
Anaweza kukutegea mtego Kwa kukuchokoza au kukukejeli ili kujua akili yako inavyofanya kazi. Je unaweza kudhibiti mihemko yako?
Usipende kugomba gomba, kubishana na wanawake, kuwatukana.
Ukishaanza kutukanana na mwanamke jua umeshaingia kwenye mfumo wake. Ashashinda mins game hiyo
Wanawake hupenda attention. Unapotukanana naye tayari umeshampa attention yako. Umeonyesha kujali.
Njia sahihi ni kukaa kimya,
Kuondoka na kuondoa mazoea,
Kuwa mbali na mwanamke huyo,
Kutompa nafasi wala kumsaidia,
Kutoonyesha kutomjali, n.k.
Kufikia hapa wazee sina la ziada.
Kwa makala Kali njoo WhatsApp channel Yangu kisha follow bonyeza haps 👉🏼👉🏼👉🏼https://whatsapp.com/channel/0029Vb278CM2P59fD18MyJ01
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi