VYOTE NDANI GONGA94
FORGIVE ME, MOM ๐ญ๐ญ nisamehe mama SEHEMU YA: 07
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO..........
Baba alistuka na kubaki akiniangalia, nilimuuliza Tena kwa sauti ya juu Zaidi
" Kwanini uliikimbia familia yako yaani kwanini ulituacha...??"
"Lakini Sasa hivi SI tunakula matunda pamoja jamani..."
Alijibu baba akiwa ananiangalia
"Mmmh nashindwa kuelewa nahisi kuchanganyikiwa zaidi, Nani mkweli Kati ya wewe na mama , sijui nilikuwa mjinga kiasi gani kushindwa kuelewa upendo wa mama kwangu, hakuwai hata kukusema ubaya lakini baba wewe sasa, sijui niongee Nini unielewe sijui nizungumze kwa lugha gani, ukajifanya unanipenda Sana maneno kidogo ukaenda kuchoma nyumba unajua pale nilimpoteza nani? Nilipoteza Kaka na kumbukumbu zote nzuri kuhusu mama angu, ila Mimi nimpuuzi Sana "
"Kilichotokea kimetokea na najisikia vibaya Sana niamini mwanangu tusahau kila kitu na tuanze maisha mapya kama familia naomba Sana sana "
" Naomba nikuache na familia yako siwezi kuishi maisha haya ya raha na maumivu niliyokuwa nayo"
Nilianza kutoa nguo zangu kwenye kabati na kuweka kwenye bag, muda huo huo mama angu wa kambo akaingia na kuomba kuongea na Mimi , baba akatoka nje
"Waoooooh taarifa za kufurahisha hizi Hatimaye unaondoka leo, saada sikuwai kukupenda hata kidogo na maombi yangu leo yanatimia kwanza ungeniharibia watoto wangu tu"
Nilimungalia bila kuongea chochote nikaendelea kupaki nguo zangu
" Nilikuwa sijui kuwa uko na cheo kingine Cha ukiziwi na ububu "
Aliendelea mama kuongea akitaka kuziona hasira zangu, niliishia kumuangalia tuu, nilimaliza kupaki mizigo yangu nikatoka nje, naye akanifuata nyuma na kuigiza kuwa ananiomba nisiondoke, nilikuwa na hasira sana, niliita tax na kuondoka moja kwa moja nikaenda kwenye nyumba za wageni, niliingia ndani nililia Sana nilitamani kila kitu kiwe ndoto nilitamani kila ninachokiona kiwe ndoto tuu na niamke hiishe lakini ndio ilikuwa ukweli, sura ya mama haikuacha kucheza katika ubongo wangu, nilimkumbuka kamili alivyokuwa akiniitaji lakini sikuwai kabisa kujali kuhusu yeye sikuwai kujali juu ya mwanamke ambaye alikuwa akizurula mtaani kutafuta hela ya kula kwaajili yangu, kiukweli siku yangu ilikuwa mbaya sana.
Baada ya siku tatu nilipata chumba, maeneo ya buguruni niliamua kuanza maisha yangu mapya, nilijaribu pia kumtafuta Julius lakini sikuweza kumpata, nilifungua genge pale nilikopanga, watu wangi walikuwa wakinishangaa inakuwaje msichana mzuri Kama huyu anauza genge, nilikuwa na wateja wa kutosha na maisha yaliendelea, nilifanikiwa kukutana na mkaka ambaye alionesha kabisa Nia ya kuwa na Mimi, tulikubaliana na nikaama nilipokuwa nakaa na kuamia nyumbani kwake tukaanza kuishi kama mke na mume, maisha yalikuwa mazuri sana, nilifurahi na kuinjoy maisha mazuri niliyoishi na mkaka huyu ambaye alijulikana Kama zuberi
Baada ya muda nilienda kupima na kujikuta Ni mjamzito
, Zilikuwa taarifa za kufurahisha Sana baada ya kuona naenda kuongeza familia, lakini Bado nilikuwa na kidonda kikubwa kuhusu mama, nakumbuka ilikuwa usiku tumelala, uku mimba yangu ikiwa na miezi 7 mlango uligongwa sana zuberi akainuka na kufungua alistuka sana baada ya kumuona mtu aliyekuwa akigonga
"Ni Nani usikuu huu...??"
Niliuliza lakini gafla akaingia mwanamke mzuri Sana alikuwa amependeza Sana niliuliza tena
" Samahani wewe Ni nani...??"
"Nikuulize wewe, zuberi huyu ni Nani ..??"
Aliuliza mwanamke huyo alionesha kuwa anamfahamu Sana zuberi
"Baby I can explain"
Alijibu zuberi
"Cha kuelezea Ni Nini na kila kitu Kiko wazi yaani baada ya kukuachia chumba changu na duka ukaamua ulete na mwanamke we mwanaume gani uliziki, anyway beba huu mzoga wako toka nao"
Nilistuka kujua kila kitu kilikuwa Ni Cha yule mwanamke, muda huo Sina chochote mkononi Sina hata mia pesa zote nilimpa zuberi ili akuze biashara tulitolewa nje na kutupiwa vitu nje Kama mbwa akujali hali yangu ya ujauzito.
Zuberi alikuwa kimya wakati wote huo nilikuwa nikilia Sana
" Kwahiyo ulikuwa unanidanganya wakati wote huo..? Haya tunaenda wapi ??"
" Tunaenda wapi na Nani ushaniharibia Mimi unatikili naenda wapi Sina ndugu mjini uku naenda zangu wa masela "
" Halafu Mimi unaniacha na nani na unajua kabisa Sina ndugu"
" We chizi Nini me ndo nilikuzaa au muulize mama ako utaenda wapi Tena usiendelee kunifata"
Alizungumza zuberi kwa hasira Sana nilihisi kuchanganyikiwa nikaendelea kumfuata, alinipiga Sana nikapoteza fahamu.
Nilikuja kuamka nikiwa katika vitanda vya hospital Nina dripu pembeni lakini pia tumbo langu lilikuwa dogo sana pembeni alikuwako Ness ambaye moja kwa moja nilijua ndio alikuwa akinihudumia
" Oooh umeamka jambo la kheri"
"Oooh samahani hi ni hospital gani...??"
"Tulia kwanza sawa, tuliza akili yako nashukuru kwanza umeamka maana ni siku ya tatu Sasa tangu uletwe hapa "
"Siku ya tatu....??"
Nilistuka Sana kusikia nimekaa siku tatu hospital, nilianza kufikilia bill itakuwa kiasi gani.
"Subili nikuletee chakula "
Alitoka Ness tule na kurudi na chakula kizuri sana kwa muonekano tu unajua kuwa hiki Chakula Ni Cha be sana nilipata wasiwasi juu ya malipo ikabidi niulize
" Hiki chakula ni bure au...??"
"Oooh nilisahau mtu aliyekuleta usiku wa juzi alilipa kila kitu na kuomba uchukuliwe uangalizi wa hali ya juu mpaka utakapokuwa sawa, alijitambulisha kwa jina la Julius"
Nilitabasamu baada ya kujua kuwa Kaka yangu ndio ameokoa maisha yangu.
" Na vipi kuhusu mtoto wangu??"
"Pole Sana alifia tumboni hatukuwa na budi bali kukufanyia upasuaji ili kuwaokoa maisha yako, muda huo huo simu ya Ness ikaita akasema
"Anapiga..."
Nikamuuliza
"Nani ....??"
"Julius..........
ITAENDELEA......
SHUKRANI โ Emidee ft. Mbacho Wizzy (Official Lyrics Video) ? Produced by: Gift Record ? Released: 20
Wimbo wenye ubunifu imechanga kiarabu kiswahili na amapiano wimbo wa kushukuru kwa maisha na upendo Sasa sikiliza na ku download hapa gonga94.com
Sikiliza Wimbo Kamili
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi forgive-me-mom-nisamehe-mama-sehemu-ya