GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 05 Hatimae nilifika kwa General
"Ingia"
Nikafungua mlango na kuingia, kisha nilimkuta muhimu General akiwa kakaa na raptop take yupo bize kidogo mwenyewe nikamuambia:
"Muheshimiwa, nimeambiwa unaniita"
"Ndio nimekuita rafiki yangu, sasa hivi ni mtu na rafiki yake, tafadhari niite Ethane, usiniite muheshimiwa sawa"
Aliongea huku macho bize kwenye kazi aliyokuwa anaifanya, kwenye raptop yake, nilitabasam tuu lakini niliendelea kusimama hapo, General akaniambia:
"Kaa basi kwenye kiti"
Nilikaa na kisha akaniambia:
"Laura sijakuona kwenye chakula, vipi umekula lakini?
"Ndio nimekula"
Nilimjibu kwa sauti yangu ya upole, huku nikiwa bado sina uhakika nae, nilikuwa namuogopa bado, japo sio sana kama mwanzo, aliendelea kuniambia :
"Laura natamani kukujua, unaweza kuniambia kuhusu wewe"
"Kwanini muheshimiwa"
"Aah! Hapana usiniite muheshimiwa bwana, naitwa Ethane, na kingine kwani nivibaya mtu kumjua rafiki yake?
Nilitabasam tuu kisha nilimjibu:
"Hapana"
"Basi niambie namimi nitakuambia"
"Ok sawa, mimi naitwa Laura Lewis nimtoto wakwanza na wamwisho katika familia ya Mr na Mrs Lewis, ambayo inapatokana mkoa wa dar essalam, wilaya ya ilala maeneo ya tabata , nilimaliza elimu yangu ya secondary mwaka jana, shule ya kigurunyembe mkoani morogoro, nazani umenijua au bado"
"No! Bado bwana, hujaniambia unapenda nini, marafiki zako and everything, si tayari mimi na wewe nimarafiki, niambie basi"
"Mmh! Haya mimi napenda kusafiri, rangi yangu ni blue, chakula napenda ugali samaki, kuhusu marafiki sina marafiki kiukweli"
"Mimi si nirafiki yako tayari au hutaki"
Nilitabasam tuu sikumjibu kitu, kisha aliiweka laptop yake pembeni na kuniambia:
"Ngoja nikuambie kuhusu mimi sasa, mimi naitwa Ethane Deogratias, ni mtoto wa kwanza kati ya watoto wawili wa mzee Deogratias, babayangu mzee Deogratias aliaga dunia miaka kumi iliyo pita, nikiwa bado kijana mdogo, kabra ya kuaga dunia alikuwa mkuu wa mkoa mstaafu mkoani dodoma, mpaka leo hii mama yangu yupo mkoani dodoma, kwani tulisha weka mizizi yetu huko dodoma, mimi kabila langu ni muhehe, nina mdogoangu mmoja tu wa kike, ambae kwa sasa anaishi Canada, aliolewa huko na mzungu, namimi ninaishi dodoma na mamaangu, bado sijaoa, sina marafiki pia, ila kwa sasa ninae Laura, rangi yangu ni nyeupe, napenda ugali na nyama, nakuomba uwe rafiki yangu usiniogope,
Nilimpa pole kwa kumpoteza babaake, kisha nikamuangalia, alafu nikajiku natabasam na kumuitikia, kisha nilimuuliza:
"Mbona umenichagua mimi, niwe rafiki yako kwanini?
"Nitakuambia Laura, ila sio leo"
"Mmh! Haya sawa, na kuhusu mahusiano yako boyfriend and girlfriend, maana kwa umli tayari wewe nimtu mzima, hujaniambia kuhusu hilo"
Alikaa kimya kwa muda kidogo hadi niliogopa, kisha alinijibu :
"Naomba nahilo nalo niweke kiporo, nitakujibu ila sio leo, vipi utakuwa umechoka, ukapumzike kesho mapema mazoezi, nashukuru kwa kampani yako rafiki yangu"
"Sawa, usiku mwema na kwako"
Kisha nilisimama na kutaka kuondoka, aliinika General na kuniita:
"Laura!
Kisha alinisogelea hadi nilipokuwa, akaniambia:
"Naweza kuku kumbatia"
Huwezi amini nilikuwa naogopa sana, kwani sijamzoea bado, nikaanza kujisemea kimoyo moyo:
"Mmh! Mbona anakuja kwa kasi hivi"
Kwakuwa alikuwa tayari mbele yangu, na yupo tayari kwa hug, niliona nisionekane mshamba nilimuambia:
"Unaweza, kwanini isiwezekane"
Kisha alinikumbatia, kiukweli sijui alinifanya nini, nilijikuta ghafla mapigo yangu ya moyo yanadunda kwa kasi, niliamua kumsukuma kuhofia asije akagundua, nikafungua mlango na kuondoka mbio, kwenda bwenini, nilipo fika mlangoni, nilikutana na mkuu wa kikosi changu, akaniuliza:
"Umetoka wapi?
Niliona nikimuambia kuwa nilikuwa kwa General, sijui atanifikiliaje, nahivi muda ulikuwa umeenda sana hivyo niliona nimdanganye, kwa kumuambia:
"Nilikuwa nafanya mazoezi mwenyewe mkuu"
Kisha nilifungua mlango na kuingia ndani, mkuu wetu wa kikosi alibaki kama kapigwa na butwaa, kwani inaonyesha wazi kabisa hakuniamini nilicho muambia kabisa...
Je nini kitafuata ??
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi