GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 08 Nilimtizama sana nilikuwa natamani niipore simu, lakini nikajisemea kama kweli
"Ethane hujui tuu ninavyo kupenda mwenzio, nashindwa kula nashindwa kulala umejaa akilini mwangu, kwanini unaniadhibu kwa namna hii jamani mbona haya mapenzi sio kitu kizuri kwsngu, kwanini upige simu usiombe kuongea na mimi, mbaya zaidi mbele yangu hata kuuliza hali yangu tuu, inamaana umeamua kunifuta kabisa kwenye kumbu kumbu zako eeh!, General Ethane nateseka mwenzio nione mimi tafadhari, rudi hapa upesi tafadhari na ahidi ukirudi nitakuambia mbela za makamanda wote, kuwa nakupenda sana na sijiwezi juu yako, sindio ulikuwa unataka nikili hivyo basi sawa nitakili kweli tafadhari rudi,
Nancy alisikiliza yoote nilikuwa nikiongea huku nikilia, alinionea huruma na alitamani aligongee mlango lakini aliona sio sawa kuingilia faragha za mtu, hivyo aliamua kukaa mlangoni na kuwazuia watu wengine wasije kusikia, kisha nilinawa uso na kujifuta maji, baada ya hapo nikatoka nje nilikutana nae hapo mlangoni, alikuwa anajifanya nae ndio katoka chooni, akanifuata na kuniambia:
"Laura tafadhari naomba kuongea nawewe"
"Kuhusu nini Nancy nimechoka sana, kama sio muhimu niacha sijisikii vizuri nahitaji kupumzika tu"
"Najua haupo sawa ila nahitaji nikusaidie niruhusu tafadhari"
"Unisaidie? Utanisaidia nini kwamfano eeh! Hahahaaa hembu niache nikapumzike nitakuwa sawa tuu, wewe nenda uendelee na mambo yako"
Siku hiyo ilikuwa siku ya jumapili ni siku yakupumzika, tunafanya usafi kisha kwenda kufanya ibada, ndio maana tulikuwa huru, kisha nilipomaliza kumjibu hivyo Nancy nikaanza safari ya kuelekea bweni, alikuja na kunishika kwa nguvu mkono Nancy, kisha alinipeleka pembeni na kuniambia:
"Unadhani sijui nini kinakutafuna eeh!"
Nilitoa macho kwa mshangao mkubwa, na huku nikisubili kusikia kitu gani anajua kinacho nitafuna mimi, Nancy aliendelea kusema tena kwa hasira na huku akijiamini:
"Najua kilakitu kuhusu wewe na General, na ndio kitu kinacho kutafuana sasa"
Nilimtizama kisha nikambishia:
"Hujui kitu. Eti mimi na General? Haya niambie mimi na huyo katili tunanini yani eeh!?
Nilijibu kwa kujiamini ili kupoteza maboya Nancy, akanijibu:
"Laura......nimesikia kilakitu hupaswi kuendelea kunibishia tena"
Niliishiwa pozi nikachuchumaa na chini huku nikilia, alikuja Nancy kwa nyuma yangu akanikumbatia huku akinibembeleza, na kuniambia:
"Najua Laura unampenda sana General, hata yeye najua anakupenda hadi alishindwa kijizui alipokuwa hapa pia, lakini mbona unaruhusu mapenzi yakutawale namna hii kipenzi, umekuwa kama mjinga sasa unashindwa kuzui hisia zako kabisa, yupo wapi Laura wangu jasiri eeh! Ulikuwa mpambanaji katika mazoezi na kilakitu, ulikuwa hukubali kushindwa, lakini leo hii kitu kidogo tuu kimekushinda mapenzi.
Yaani yamekudhoofisha namna hii eeh! Haya tafadhari jitulize na ujikaze tunakutegemea kipenzi, ulisha wahi kusena huamini katika mapenzi, leo hiii uko wapi eeh! uko wapi Laura"
Alivyokuwa ananiambia hivyo Nancy hayo maneno yalinichoma sana, na kunifanya nizidi kulia na huku nikimjibu:
"Nancy General, General Nancy amenimaliza kilakitu, ameuteka moyo wangu na kuondoka nao, kaniacha nichanganyikiwe na niwe kichaa kabisaa, nahisi kufa kabisa asipo rudi, hata mawasiliano yake tuu sina, sijui nikitoka hapa naenda kumpatia wapi mimi, na muda unaenda sana tunakalibia kumaliza mafunzo yetu, na mbaya zaidi hayupo Tanzania sijui lini anarudi naumia mwenzio Nancy"
"Basi jikaze kwa muda huu mchache, ili tumalize mafunzo yetu kwa amani, kisha tutatafuta namna ya kumpata, tukiwa hapa hapa kambini kabla hatujaondoka, nitakuwa upande wako kipenzi sawa?
"Unasema kweli Nancy?
"Ninamaanisha, usiogope nitakusaidia"
"Sawa, asante Nancy ila naomba usimwambie mtu yeyote tafadhari?
"Naanzaje kipenzi, nimeamua kukusaidia hivyo siwezi kuwa mnafiki sawa"
Kisha alinifuta machozi na kunitia moyo nikainuka na huku akinisaidia akanisindikiza hadi bwenini kisha aliniambia:
"Pumzika kwa muda kisha jioni twende tukapashe kidogo sawa?
"Sawa kipenzi"
Wale wambea walibaki wakinitizama tuu huku wakinongona:
"Hivii huyu amekuwaje sikuhizi hatumuelewi, maana hata kula hali kazi ni kulialia tuu hovyo, sijui kakubwa na ugonjwa gani"
Niliachana nao kisha nikalala usingizi ulinipitia vizuri sana kwani kidogo nimepata nafuu baada ya kumuambia Nancy kinacho nisibu na kunipa ushauli nilipata moyo kiukweli nikajikuta nalala vizuri sana, baadae jioni jioni niliamka na Nancy alinifuata akaniambia:
"Haya sasa twende zetu kipenzi"
Tukaenda uwanjani tulikimbia sana hadi nilikuwa nahema mno, kisha tulianza kufanya mazoezi baadhi kiukweli alinifanya nianze kuimarisha akiri yangu, hadi muda wa kwenda kula ulipofika nilikuwa niko poa kabisa, tukaenda kula sasa wakati tunakula hapo Catrine alianza kuongea na wenzie huku tunasikia kwakuwa tulikuwa kando yao tuu alisema:
"Nikitoka hapa siwafichi vipenzi vyangu, kwani naenda kuolewa na General Ethane, na tayari babaangu kaniambia nijiandae, sijawahi kuwaambia familia yetu na yao ni family friendly, babaangu alikuwa rafiki mkubwa sana wa babaake, hivyo wameamua iwe hivyo ilikuuendeleza urafiki wao, na hao visokoro kwinyo waliokuwa wanajisogeza kwa mumewangu mtarajiwa, nitawanyoosha sio muda mrefu"
Nilihisi kama kunamtu kaingia ndani ya moyo wangu, na kuanza kuuchana chana na viwembe vipande vipande:
Je nini kitatokea kwa Laura, Endelea kufuatilia..............
WhatsApp 0742133100
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi