GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 19
0742133100
Aliendesha na kuanza safari yakurudi dar, japo kuwa muda ulikuwa umeenda lakini hakujali, alifika dar mida ya saa saba ya usiku, na kwenda moja kwa moja kwake alilala hadi palipokucha asubuhi na mapema, alitoka na kwenda kwa General mstaafu anamuheshimu kama babaaka, alienda kuongea nae na kumuomba jioni ya leo akamsaidie kupeleka barua ya kunichumia mimi, yule mbaba alikubali na kufurahi sana, kwani amekuwa akimsisitiza kupata mwenza wa maisha sasa ndio kamfurahisha sana, hatimae muda ulipofika nikiwa nyumbani mimi na shangazi yangu pamoja na mjomba, tulisikia kunawageni wamekuja hivyo mjomba alimuambia dada wa kazi awakaribishe ndani, alifanya kama alivyo ambiwa hivyo wageni waliingia ndani, wakasalimia na kisha walijitambulisha mimi nilikuwa tayari nimeenda chumbani kwangu muda huo,
"Mimi naitwa Mr Donald John ni General mstaafu, nipo namwenzangu nae ni kanali mstaafu anaitwa Mr Luis, sisi niwageni wa binti yenu Laura"
Mjomba alijua wamekuja kikazi hivyo akafurahi kuwaona na kuwaambia:
"Ooh! Kumbe karibuni sana Laura yupo chumbani kwake ngoja tuwaitie"
"Hapana bado hatujaelewana vizuri, sisi tumekuja kuleta barua ya kumchumbia binti yako Laura, kijana wetu Ethane kamuona na kavutiwa nae tunaomba kuunganisha undugu"
"Ok sawa hakuna shida karibuni sana, namimi nimjomba na huyu ni shangazi yake, ndio walezi wake tunaipokea barua kwa mikono miwili, msijali tutawaambia siku mje kuchukua majibu"
"Sawa tunashuka na tunaomba tuwaache, kwani tumewavamia tuu bila kuwaanda, mlikuwa na ratiba zenu tusizivuruge"
"Hamna shaka mnakaribishwa sana hapa ninyumbani"
Kisha waliaga na kuondoka, mjomba aliwasindikiza hadi getini, kisha akarudi ndani, na kumuambia shangazi:
"Ulikuwa unajua kama kunaugeni unakuja?
"Hapana sikuwa najua"
"Muite Laura"
Alikuja mdada wa kazi na kuniambia:
"Mjomba wako anakuita"
Niliinuka na kwenda sebreni nikiwa kawaida tuu, kwanj tangu jana nimeizima simu yangu, baada ya kufika dar na sijawasiliana kabisa na Ethane kiukweli, sikuwa na raha kabisa nilipofika sebreni nilimuambia mjomba:
"Mjomba umeniita?
"Ndio"
Shangazi akanishika mkono nakuniambia :
"Haya kaa hapa kipenzi changu"
Nilikaa na kuwasikiliza wameniitia nini, mjomba akaanza kuongea:
"Kunawageni wako walikuwa hapa Mr Donald na mr Luis, wanadai wao ni washenga wa Mr Ethane, je unamjua Mr Ethane?
Nilishtuka kusikia nilibaki nikiwa nimetoa macho tuu, mjomba akaniita"
"Laura, nimekuuliza swali mama?
Nilijikuta najisikia vibaya sana, baada ya kukumbuka nilichokisikia kutoka kwa mamaake, mwisho niliinuka na kukimbilia chumbani tena huku nikilia, shangazi alimuambia mjomba :
"Ngoja nikaongee nae ukiona hivyo hayupo sawa"
Mjomba alibaki akisubili, na shangazi aliinuka na kuja chumbani nilipokua, akanikuta nimejilaza kitandandani huku nikilia, kisha alikaa pembeni yangu na kuniuliza:
"Laura kwani huyu sindio Ethane wako yule General eeh!?
Nilimuitikua kwa kichwa, kumaanisha ndio yeye, kisha shangazi akaniambia:
"Sasa siulipaswa kusherekea, kwani unaenda kuolewa na mwanaume ulie mpenda, sasa kulikoni hembu naomba ufute machozi na uniambie nini tatizo?
Shangazi alinifuta machozi na kunituliza kisha aliniambia:
"Niambie nini tatizo nitamfuata nikamzubue makofi mimi, wewe niambie tuu kakufanya nini?
"Mama wewe achatuu tulipoenda dodoma kwa mamaake ili akanitambulishe, kumbe mamaake alishamuandalia mchumba mwanae mwingine anaemtaka yeye, sasa tangu nipo hapo nyumbani yule mamaake hakuwa hata anataka kupiga story namimi, sikuwa namjua nilijua ndiontabia yake, kumbe hakuwa ananipenda, jana alikuja mmama mmoja na binti yake hapo nyumbani, tena niliitwa niwape vinywaji mimi huyuu, baada ya kuwapa vinywaji niliwaacha wenyewe, muda sio mrefu nae Ethane alipofika alitumwa dada wakazi kumuita, akaenda sasa niliona kakaa sana nikasema niende namimi, kwani labda wanapiga tu story namimi kukaa pekeangu nilikuwa tayari nimeboreka, nilipokuwa nakaribia hapo sebreni nilikuwa namsikia mamaake akiongea, mama huwezi amini maneno aliyokuwa anamuambia mwanae, na huku akijua mimi nipo na ninani yake mwanae, nilihisi kumchukia na kuamua kuondoka kurudi dar"
"Nimaneno gani hayo ndio nataka kuyasikia"
"Alikuwa anamuambia yule binti aliekuja na mamaake ndio mchumba aliemchumbilia yeye, na hataki kuona hao wengine aliowaleta yeye"
"Vipi, Ethane nae alijibu nini"
"Hakujibu kitu, ndio mnanishangaza kusema kuwa kaleta washenga"
"Sasa ndio uelewe kuwa Ethane hakukubaliana na uamuzi wa mamaake, na kama angekuwa kaukubali asingekutumia barua yakuomba kukuchumbia, upo kipenzi haya mpigie mchumba wako sasahivi na umuunge mkono anahangaika kwaajili yako wewe"
"Sawa mama"
"Fanya haraka"
Kisha mama aliinuka na kwenda sebreni akamsimulia mjomba kilakitu, kisha mjomba aliamua kumkubali Ethane, aliona kuwa huyu ndio mwanaume anaestahili kunioa mimi, kwani ni mwanaume mwenye msimamo na maamuzi pia, anaweza kunilinda kwa chochote kile hata kukabiliana na ndugu zake, kisha akasema:
"Tuwaambie waje wachukuwe majibu yao kesho kutwa, sawa mkewangu sitaki kuwa chelewesha, kwani nimwanaume anaestahili tusije kumpoteza"
Shangazi alicheka sana na kisha aliniita mimi, nilikuwa chumbani nikatoka na shangazi akaniuliza:
"Vipi umesha ongea na Ethane?
"Bado mama nimempigia simuyake inaitatuu"
"Usiogope uenda akawa yupo bize au kalala, akiwa sawa atapokea tuu kipenzi sawa?
"Sawa mama"
Kisha mjomba alinivuta na kunikumbatia hapo, tukiwa tumekaa kwenye kochi na huku akiniambia:
"Ethane ni mwanaume bora kipenzi sawa?
Nilibaki nikitabasam tuu, wakati tunaongea mala simu yangu ikaita, na mjomba akaichukua na kuipokea yeye, kisha akamuambia:
"Hallow "
"Ethane wewe ni mwanaume wakweli, haya watume hao washenga wako kesho, waje wachukue majibu ya barua uliyowatuma sawa?
"Sawa mjomba, Shikamoo mjomba"
"Marhabaah, haya ongea na mwanangu nisimsubilishe sana"
Tulifurahi sana, nikachukua simu na kwenda chumbani kwangu, huku tukiwa tunaongea na Ethane, nifuraha isiyo na kifani kwakweli,
Je nikweli Ethane atamuoa Laura ambae mamaake hamtaki au atabadili maamuzi endelea kuifuatilia ilikujua..........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi