*MKAKA KAUZU HUYU JAMANI* *SEHEMU YA SABA* Kwakuwa nilikuwa na mihasira yangu na tayali J nikishaamua kujiweka
"Unaniumiza"
Frank akaniachia kwa haraka kisha akaniuliza
"Oooooh pole kwani Bado unaumwa au ?"
"Niko Sawa"
Nilijibu kisha nikasogelea meza yangu na kukaa na kuanza kupitia kazi zangu
"Naona Sina kazi Mpya na Leo ni jumatatu"
Nilimwambia frank.
"Aaah usijali kazi zako zote za Leo nilikufanyia Jana na Leo jioni nitafikisha sehemu husika"
Alijibu frank Tena kwa kunichangamkia sana, Yaani frank alikuwa ni wa tofauti sana sio frank. Yule kauzu, Yaani alikuwa ni frank Mpya kabisa sio Yule ambaye ata salamu yake ilikuwa ni shida kubwa sana kuipata
"Sawa Asante unaweza kunitumia hivyo hivyo ili nipate kuipitia kidogo"
"Bila Shaka Malkia wangu"
Alijibu frank na Kuwal kwenye meza yake.
Ili neni Malkia wangu lilinishtua kidogo na kunifanya nimuangalie frank ambaye alikuwa amechangamka sana na kuonekana Kuwa ni mtu kwenye furaha sana.
Kwa upande wangu nilihakikisha Kuwa nafanya shughuli zangu tu pasi na kumfikilia frank ambaye amenivunja sana moyo wangu baada ya kunipatia maneno machafu siku ambayo niliamua kunipatia mwili wangu..
Muda wa kwenda Nyumbani ulifika na nilikuwa wa kwanza kuondoka, Yaani kitendo cha muda tu kufika nilinyanyua kila kilichokua cha kwangu. na kuondoka pasi kumuaga mtu yeyote Yule.
Ikiwa ni Majila ya Saa 2 nikiwa chumbani kwangu, simu yangu iliita na nilipoangalia Namba ilikuwa ngeni kabisa, nikaiangalia kwa muda kisha nikapokea na kuzungumza.
"Hellow, naongea na Nani ?"
"Hatimaye umepokea simu yangu, me frank Nipo nje hapa kwenu unaweza kutoka tukazungumza
Kwanza nilishtuka sana kisha nikasogea dilishani kwani chumba changu kipo juu hivyo. Nina uwezo wa kuona nje na kweli Nilimuona. frank akizunguka getini kwetu.
"Umekuja kufanya nini frank ?"
Nilimuuliza kwenye simu uku nikimuangalia.
kupitia dilishani,
"Naomba utoke nje tupate kuzungumza please"
"Tutaongea kesho kazini me siwezi kutoka nje"
Nilijibu na pasi na kusubili jibu lake nikakata simu na kwenda kujitupia kitandani na kujikuta nikiwa ni mtu Mwenye furaha sana baada ya kuona Kuwa frank amekuja Nyumbani kwetu.
Baada ya muda nikanyanyuka na kusogelea dilishani na kuangalia lakini sikumuona Tena frank pale getini.
"Kwahiyo ameondoka kweli"
Nilijiuliza kwa huzuni kabisa, muda huo huo dada yangu akaingia chumbani kwangu na kuniambia.
"Kuna mgeni wako sebuleni"
"Mgeni?" Nilijikuta Nikimuuliza dada yangu kwa mshtuko wa hali ya juu.
"Ndio ni mkaka, yuko na baba hapo anakusubili"
Yooooh nilijikuta nikianza kutetemeka Yaani mwanaume amekuja Nyumbani kwetu na amakutana na baba yangu nyie baba yangu uwa apendi kabisa haya mambo.
"NAKUJA"
Nilijibu uku nikiwa na wasiwasi sana, Yaani frank ndio ameamua kabisa kuingia Ndani.
Basi nikajiweka vizuri pale kisha huyo nikatoka nje na kwenda kuonana na frank ambaye nilimkuta akiwa sebuleni akiwa amekaa na baba
yangu.
"Frank Karibu sana"
Nilimkaribisha kwa kumchangamkia sana.
"Asante"
"Baba huyu ni frank ni boss wangu pale ofisini"
Niliamua tu kujiami mbele ya baba yangu kabla ajaanza kuniuliza maswali ambayo yangekuwa magumu sana kwa upande wangu
"Yaaah najua ameshaniambia, sasa mwendelee na maongezi yenu Mimi Nipo chumbani"
Alizungumza baba yangu kisha akanyanyuka na kuondoka.
Kitendo cha baba yangu tu kuondoka. nikamshika frank mkono kwa nguvu na kumkukusa mpaka nje.
"Umekuja kufanya nini hapa?"
Nilimuuliza nikiwa nimeshapaniki.
"Nilikuwa sina ata plan ya kuja Nyumbani kwenu lakini ni wewe ndio umetaka Mimi niweze kuja kwenu"
"Una maanisha nini? Achana na hayo kwanza shida yako nini? Yaani unataka nini?"
"Anaya Mbona Kama uko na hasira sana kuna kosa nimekufanyla?"
Frank aliniuliza, nikimuangalia kwa hasira sana na kumjibu
"Hapana ni life style yangu Mpya tu, Sema shida yako Kijana
"Naitaji tuzungumze kiundanı sana, tunaweza tukatoka mbali na hapa ?"
"Mbali na Nyumbani kwetu ili ukapate muda mzuri wa kunidhalilisha si ndio ? Frank, najua Ndani ya siku hizi ambazo tumeishi mambo. Mengi sana yametokea na kwa sasa nafikilia tufanye Kama historia tu na kila kitu kiendelee"
"Kwanza kabisa Nimekuja kukuomba msamaha kWa kila kitu"
Nilijikuta nilianza kucheka kisha nikamuuliza.
"Yaani wewe frank uniombe Mimi msamaha?"
"Ndio na nafanya yote kwakuwa nimeshaona siwezi kuishi bila wewe anaya nakupenda. sana...
Nika......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi