Simulizi : The Return Of The Ambrosy Sehemu Ya Kwanza (1) IMEANDIKWA NA : ALEXIS WAMILLAZO Walemi binti kutoka makao makuu ya Nchini, mkoani Dodoma
Lakini baada ya miaka kadhaa kupita, hatimaye Walemi anabahatika kukutana na mpenzi wake wa zamani sana wa kipindi hicho yupo mkoani kwao Dodoma. Mwanaume huyo ndiye aliyemtoa bikira huku wakiwekeana nadhiri kuwa katu hawatokuja kuachana maishani mwao. Ila mwishowe nadhiri hiyo ikaja kugeuka asidi mara baada mpenzi wake huyo kwenda DAR-ES-SALAAM kutafuta maisha na kisha kulowea. Walemi hakuamini machoni mwake kile akionacho, machozi ya furaha yalimtoka hasa walipokumbushana mambo kadhaa ya nyuma. Na hivyo Walemi akahitaji kujua anapoishi mwanaume huyo, alipopafahamu akawa anaenda kulala huko mara nyingine anafanya naye mapenzi huku akimuachia pesa nyingi ya matumizi pasipo Ambrosy kujua. Siku kadhaa mbele Walemi na huyo mwanaume walipanga mikakati ya kufanya mapinduzi juu Ambrosy ili wapate nafasi ya kufurahia penzi lao pasipo buguzi wala hofu yoyote. Walemi aliamini kufanya hivyo atabaki na amani na mpenzi wake huyo wa zamani, akasahau Ambrosy alipomtoa mpaka Kufika hapo alipo,wema Ambrosy ukawa kikwazo kwake na hatimaye Walemi alimuua Ambrosy kwa kumuwekea sumu kwenye chakula. Miradi yote sasa ikawa chini yake na mwanaume huyo, raha mstarehe wawili hao ikatamaraki mioyoni mwao. Ila baada miaka minne kupita tangu kifo chake Ambrosy, ajabu usiku mmoja Walemi alishtuka kusikia simu yake ikiita,alijikakamua akainuka na kisha akaichukua simu hiyo ili ajue ni nani aliyempigia. Namba ilikuwa mpya, hivyo kwa sauti iliyoonyesha bado anausingizi alibonyeza kitufe cha kijani kisha akaweka simu sikioni akasema "Hello nani mwenzangu? Na kisha kwanini unapiga simu usiku" Ajabu Walemi hakujibiwa, mtu huyo aliyempigia alikaa kimya kitendo ambacho kilimfanya Walemi kutoa simu sikioni na kisha kuitazama namba hiyo kwa mara nyingine tena. Ghafla alishtuka akaitupa simu chini, kijasho chembamba kikaanza kumtoka huku mapigo ya moyo wake yakienda mbio mfano wa chura apumuapo. Namba ili ilimshtua sana, aliogopa Walemi akilini akajiuliza "Ambrosy? Si kasha kufa? Sasa iweje ten anipigie?.." Wakati Walemi akijiuliza maswali hayo punde si punde uliingia ujumbe mfupi (sms) Kwa mara nyingine Walemi alitaharuki ingawa mwishowe alipiga moyo konde akaichukua simu ili ajue ujumbe huo unasema nini. Alipofungua alikutana na jumbe iliyoandikwa THE RETURN OF THE AMBROSY... "
{Kurudi kwa Ambrosy}
"Mungu wangu marehemu karudi?.." Alijiuliza Walemi huku akihema juujuu asiamini kile alichokisisoma. Aligeuka kumtazama mumewe ambaye naye muda huo alikuwa amelala fo fo fo hata asiwe na habari kwamba mtu yule waliyedhurumu nafsi yake sasa karejea. Walemi aliogopa sana habari hiyo, maswali kibao akajiuliza pasipo kupata majibu.
"Ambrosy? No. Hapana sitaki kuamini kama kweli Ambrosy kafufuka,hii ni imani potofu kabisa na mambo haya hutokea kwenye senema na sio vinginevyo. Inawezekana vipi mtu aliyekufa akarudi tena duniani? Je, inamaana kwamba hakuna pepo ama jehanamu?.." maswali yote Walemi alikuwa akijiuliza kichwani mwake wakati huo mapigo ya moyo wake yakienda kasi,na punde si punde simu ile ikarudia kuita kwa namba ile ile aliyokuwa akitumia Ambrosy enzi ya uhai wake. Walemi kuona hivyo akafikiria heri kuizima simu hiyo, na sio kuizima tu bali alitenganisha kabisa betri na simu kisha akalala na kuanza upya kutafuta lepe la usingizi huku kiakili na kimwili akionekana kutokuwa sawa, Sula hilo la la kurudi kwa Ambrosy lilimchanganya mno.
Baada Walemi kusinzia, muda mchache baadaye mwanaume wake naye aliamka kwa dhumuni la kuelekea chooni kujisaidia. Mwanaume huyo ambaye aliitwa Daniel alijitahidi vema kushirikiana na Walemi kumuua Ambrosy ili wafurahie vizuri penzi lao kama zamani walipokuwa Dodoma. Hivyo Daniel alipoamka alijinyoosha kwanza kisha akainuka pale kitandani akatundua taulo yake kwenye enga tayari kwa safari ya kuelekea chooni. Lakini kabla hajafungua mlango wa kutokea chumbani alishtuka kuona simu ya mkewe imetenganishwa betri. "Mmh" Aliguna Daniel kisha akatikisa kichwa kama ishara ya kukataa jambo fulani halafu akazipiga hatua kuelekea chooni kujisaidia. Muda huo ulikuwa usiku wapata saa saba ikikimbilia saa nane. Daniel alizipiga hatua kuelekea chooni,ila kabla hajafika alistaajabu kutozikuta ndala maalumu za kuingia nazo chooni,hivyo kiashiria hicho kilimanisha kuwa chooni kuna mtu. Lakini ni nani wakati nyumba nzima anaishi yeye na mkewe tu? Kitendo hicho kilimfanya Daniel kupigwa na butwaa lakini mwishowe akaona hakuna haja ya kuogopa, aliusogelea mlango wa choo ili ausukume ajihakikishie kama kweli ndani kuna mtu ama lah! Ila kabla hajukaribia nafsi ilimsuta, haraka sana Daniel akarudi nyuma kisha akageuka akarudi chumbani kumuuliza Walemi kama kuna mahala ameziweka ndala hizo.
"Walemi, Walemi.. Walemi.." Daniel alimuamsha Walemi. Punde Walemi aliamka ndipo Daniel alipomuhoji suala hilo la ndala swali ambalo lilimshangaza sana Walemi ambapo kwa sauti yenye usingizi ndani yake akasema "Hivi ni ndoto ama? Dani unawezaje kuniamsha kisa ndala za chooni huku chumbani? Kuwa mstaarabu bwana niache nilela" Walemi alipokwisha kusema hivyo alijivutia shuka kuanzia miguuni mpaka kichwani kuonyesha kuwa hataki kubuguziwa. Hapo Daniel alishusha pumzi ndefu huku akiishia kumtazama Walemi pasipo kuongeza neno lolote, lakini mwishowe alirudi tena kule kule chooni. Safari hiyo aliziona zile ndala ila cha ajabu ndala hizo zilikuwa zimelowa maji kumanisha kuwa muda mchache uliopita kuna mtu alizitumia kuogea. "Mungu wangu" Alijisemea Daniel huku akizisogelea pole pole pale mlango,hali ya kuwa nyuma yake zilionekana nyao za maji zikiambaa kule alikotoka. Bado alizipiga hatua za woga kusogea pale kwenye mlango wa choo huku moyoni akiwa na woga wa hali ya juu uliompelekea kugeuka nyuma yake ambapo ndipo alipoziona zile nyao. Nyayo zile zilizidi kumchanganya Daniel, ghafla kijasho kikanza kumtoka na ile haja ndogo aliyokuwa nayo ikamshukia pasipo yeye kujua. Balaa lilizidi kuwa nzito upande wake pindi aliporudisha macho yake kule kwenye mlango wa choo, ghafla kwenye mlango akayaona maandishi yaliyo andikwa THE RETURN OF THE AMBROSY.
Maandishi hayo makubwa yaliandikwa kwa michirizi ya damu. Muda huo huo akaonekana Ambrosy akiwa ndani ya mavazi meupe. Aliangua kicheko Ambrosy kisha akasema "Daniel.. Damu yangu haina hatia.. Mwambie Walemi kwamba mimi ni mgeni wenu.." Alipokwisha kusema hivyo akapotea..
##
๐๐ข๐ญ๐ฎ ๐ ๐๐ง๐ข ๐ค๐ข๐ฅ๐ข๐๐ก๐จ๐๐ง๐๐๐ฅ๐๐โฆ.
๐๐ฌ๐ข๐ค๐จ๐ฌ๐ ๐ฌ๐๐ก๐๐ฆ๐ฎ ๐ข๐ง๐๐ฒ๐จ๐๐ฎ๐๐ญ๐
๐๐๐ฆ๐๐ง๐ข ๐ญ๐ฐ๐๐ง๐๐ ๐๐ก๐๐ฉ๐ฎ ๐, ๐๐จ๐ง๐ฒ๐๐ณ๐ ๐๐๐๐-150 ๐ฌ๐๐ฌ๐ ๐ก๐ข๐ฏ๐ข ๐ข๐ฅ๐ข ๐ง๐ข๐ฉ๐จ๐ฌ๐ญ ๐ง๐ฒ๐ข๐ง๐ ๐ข๐ง๐ ๐๐ก๐๐ฉ๐ฎ ๐๐ก๐๐ฉ๐ฎ ๐๐ฅ.โ
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni