UTANIITA SHEMEJI.* *SEHEMU YA 16*
SONGA NAYO.............
Zilipita dakika kadhaa nikatoka na kumfuata sebleni , akataka kuendeleza story zake nikamwambia aaah 🤚nioneshe kazi za kufanya kwanza ,kama ni maongezi baadae.
Hakuwa na shida akaanza kunionesha mazingira yote ya nyumba ile na kunipa taratibu zao pamoja na majukumu yanipasayo kufanya
Baada ya hayo nikataka kuingia jikoni kwaajili ya kuandaa chakula cha jioni ,akanizuia kwakunambia mara zote juma tano huwa mama yake anarudi na chakula so nyumbani hakupikwi kitu.
Niliitikia sawa na kukaa tu maana hakukuwa na chakufanya.
Mda ulisogea ikafika usiku mama yake akarudi tukampokea ,akauliza kama nimesha elekezwa na kupewa taratibu zote wote tukajibu ndio.
Basi kaingia chumbani sisi tukabaki tukiandaa meza na baada ya mda akatoka tukapata chakula pamoja kisha kila mmoja akaendelea na ratiba zake .
Mimi huwa sio mpenzi wa tv hivyo baada ya chakula Daria na mdogo wake walibaki wanaangalia movie mimi nikaingia chumbani kwangu.
Nilifika na kujitupa kitandani , nikalala chali na kuelekeza macho yangu juu , taratibu akili yangu ikaanza kuzama kwenye dimbwi la mawazo, niliwaza na kukumbuka matukio yote ya nyuma.
Nikashusha pumzi ndefu na kutoka kitandani nikasogea dirishani , ili niangalie nje walau nipigwe kiupepo ,maana mara zote nikiwa nahisi msongo wa mawazo au kutokuwa sawa huwa napenda nikae sehemu nipigwe upepo weee.
Hapo nahisi nafuu kwa kiasi kikubwa sana , hivyo nikasogea pale na kufungua mapazia pamoja na kioo sasa ile nimefungua kioo nilikutana uso kwa uso na yule mkaka niliekutana nae nje mida Ile namkimbilia Alvin.
Nilishtuka maana sikutegemea kumuona pale, sasa nikawaza niendelee na jambo langu au nifunge na kurudi zangu kulala🤔mmmh hapana nikifunga ataona kama namkimbia maana tayari alishaniona .
Kwa hiyo cha kufanya nikuendelea na mambo yangu ila nitajifanya kama sijamuona , kweli nilichukua kiti nikakaa na kula upepo wa Mungu.
Upande wake akawa ananiangalia huku akitabasamu naona alihisi sijamuona ,akaona akae ili aweze kuniangalia vizuri 😏.
Dakika zilisogea ikafika mda nikaona sasa hapa niko sawa , nikainuka na kutoa kiti kisha nikafunga vioo na kurudi kitandani .
Upande wake baada ya kuona nimetoka na yeye akatoka na kuingia ndani, alitembea kuelekea sebleni na kufika anakaa huku uso wake ukiwa bado na tabasamu pana.
Robyn ambae ni kijana watatu wa familia hiyo alikuwa amekaa sebleni huku akiangalia tv , kitendo cha Samuel kuja na kukaa huku akitabasamu mwenyewe kilimfanya akaacha kuangalia tv na kumuuliza ndugu yake.
"Oya vipi mbona unatabasamu mwenyewe umepata mtonyo wa maana nini ?"
Samuel kuulizwa hivyo alimuangalia Robyn na kusema " hii ni zaidi ya mtonyo mzee😊, aaah Mungu fundi bhna "
"Una maanisha nini ??🤨"
"Achana nayo maana hutanielewa " aliongea na kuinuka akaondoka , Robyn alibaki akimuangalia huku akijiuliza ni nini kilichomfanya ndugu yake kuwa na furaha vile.
Aliwaza bila majibu ,akaamua kuachana nayo na kuendelea kuangalia Tv, basi mda ulienda hatmae usiku ukapita na asubuhi ikaingia .
Kama kawaida watu waliamka na kila mmoja akawa bize na majukumu yake huku wakwenda kazini wakiwa bize kujiandaa.
Sasa mmoja kati ya majukumu yangu humu ndani ni kufanya shughuli zote za ndani pamoja na kusimamia mauzo ya mayai pamoja na kuku.
Maana boss wangu alikuwa akijushughulisha na ufugaji wa kuku ,sungura pamoja na ngo'mbe ,ila ng'ombe walikuwa sehemu tofauti na nyumbani hapo.
Hivyo kijana anaehusuka na mifugo asubuhi huwa kule waliko ng'ombe na baadae ndo huja huku nyumbani kwaajili ya kuwahudumia hawa hapa pamoja na kuweka mazingira ya nje sawa.
Sasa mimi huwa niko shap sana kwenye kazi zangu hivyo nilivyo maliza kila kitu nikaona kuliko nikae ndani tu ni bora nimsaidie kijana wawatu walau hata kumwagilia maua .
Basi nikachukua mpira na kuunganisha kwenye bomba kisha nikaanza kumwagilia, ambapo baada ya kumaliza ndani nikatoka nje ya geti na kuendelea kumwagilia.
Upande wa Samuel baada ya kujiandaa na kunywa chai alichukua begi lenye pc pamoja na simu yake akataka kutoka kuelekea kwenye gari kwaajili ya kuanza safari ya kwenda kazn.
Lakini kabla hajapiga hatua kutoka nje aliitwa na mama wa nyumba ile , Samuel aliitika na kuambatanisha na salamu.
Mama yule aliitikia huku akionesha kuchukia na kumwambia " Nipe funguo za gari lako "
Samuel alihisi kama hajasikia vizuri akamuuliza " sorry umesema !!?"
"Nimesema !! Kwamba hujasikia nilichosema 😠 embu nipe bhna unanichelewesha "
"Okay ,lakini kwanini unataka funguo la gari langu ,au kuna kitu ulisahau humo ?"
"Samuel! Unataka kunitibua si ndio , embu nipe bwanaaa 😡" eeeh hii kali, aliwaza Samuel kumpatia funguo mama yule au tumuite Mrs Watson aliichukua kwakukwapua na kuondoka huku akiambatanisha na sonyo kali.
Kwa hatua za haraka alienda maegesho na kuingia kwenye gari la Samuel, hakuchukua mda akawasha gari na kuondoka.
Samuel alibaki amesimama mlangoni huku akijiuliza kwani kuna nini hadi mama yake kaamua kutumia gari lake🤔, aliwaza na kuamua kurudi ndani .
Akamuita binti wa kazi na kumuagiza chumbani kwa wazazi wake ili akamchukulie funguo ya gari la mama yake , binti yule bila kuchelewa aliingia chumbani na kuangalia sehemu zinako wekwaga funguo ila hakuona .
Akajaribu kuangalia sehemu nyingine lakini pia hakuona, akatoka na kumwambia Samuel kuwa hajaona funguo , Samuel akamuuliza.
"Unauhakika hakuna ?" Binti yule alijibu ndio Samuel akaona huyu hayuko serious akatoka na kwenda mwenyewe ila pia hakuweza kuona .
Kwa hasira alitoka na kuchukua simu yake akampigia mama yake, ajabu simu iliita ila hakupokelewa na sio kwamba Mrs Watson alikuwa haoni simu no aliiona ila hakutaka kupokea.
Basi Samuel alivyoona simu zake hazipokelewi aliacha na kwenda chumbani kwa Robyn akangia kufika anakaa kitandani.
Kwa sauti yenye hasira akamwambia Robyn " Mama kashaanza mambo yake, ameondoka na gari langu na funguo zingine hazipo "
"Ohooo mapema hii ! Sasa utafanyaje maana mwenyewe nataka kwenda chuo na baadae nitakuwa na mizunguko mingi "
"Naelewa ila sasaivi inabidi unisogeze hadi kazn "
"Sawa na jioni je ?"
"We sikia nipeleke kazini kuhusu jioni nitajua mwenyewe"
"Poa " Robyn alimaliza kujiandaa wakatoka na kuingia kwenye gari, mlinzi akafungua geti wakatoka , sasa mda ambao wanatoka mimi nilikuwa bado namwagilia .
Hivyo walivyonifikia tu Samuel macho yote kwangu , angalia yake ilimfanya hadi Robyn akageuka kuniangalia na kumrudia ndugu yake .
Akataka kuuliza ila akakausha na kuendelea kuendesha wakanipita , upande wangu nilimaliza nikakunja mpira na kurudi ndani.
ITAENDELEA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni