VYOTE NDANI GONGA94
CAF YASHUSHA ADHABU NZITO KWA SENEGAL ๐ธ๐ณ NA MOROCCO ๐ฒ๐ฆ KUFUATIA KADHIA KATIKA FAINALI.
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
1- Kocha wa Senegal Pape Thiaw amefungiwa mechi tano rasmi pamoja na faini ya dola 100,000 za Kimarekani sawa na Million 240 za Kitanzania.
2- Mchezaji wa Senegal Malick Ndiaye amefungiwa mechi mbili.
3- Mchezaji Ismaila Sarr wa Senegal amefungiwa mechi mbili.
4- Shirikisho la soka la Senegal limepigwa faini ya dola 300,000 sawa na Million 760 za Kibongo, wakiwapiga Faini kutokana na vurugu za Mashabiki wao.
5- Senegal tena wamepigwa faini ya dola 300,000 za Kimarekani kutokana na vurugu za Wachezaji na benchi la Ufundi.
6- Senegal wamepigwa faini ya dola 15,000 kutokana na Wachezaji wake kupokea kadi nyingi za onyo.
7-Nyota wa Morocco ๐ฒ๐ฆ Achraf Hakimi amefungiwa mechi mbili ila atatumikia moja halafu moja kwa uangalizi wa mwaka.
8- Nyota wa Morocco ๐ฒ๐ฆ Ismael Saibari amefungiwa mechi tatu na faini ya dola 100,000 za Kimarekani.
9- Morocco wamepigwa faini jumla ya dola 315,000 za Kimarekani kutokana na vurugu za Mashabiki, Wachezaji na matumizi ya tochi kwa Mashabiki.
Adhabu kwa Mashirikisho ni SENEGAL ๐ธ๐ณ wanapaswa kulipa dola 615,000 za Kimarekani huku MOROCCO ๐ฒ๐ฆ wanapaswa kulipa dola 315,000 za Kimarekani.
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi caf-yashusha-adhabu-nzito-kwa-senegal-na-morocco-kufuatia-kadhia-katika-fainali