kubhaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
wengine walipitiliza na kukimbilia mtoni wengine walipalamia vyakula
Nyuki waliongezeka na kuleta janga kubwa sana kwenye kijiji hali ya dharula ilitangazwa na mjumbe alie valia mifuko mwili mzima ,jamani njia ya kuelekea kijiweni nyuki wamejaa tafadhali msipite alitangaza kila kona ya kijiji kwa kuwa yeye alikuwa kajikinga na mavazi yake ya asili ya kubuni alikuwa na moto kwenye makopo ya mikaa na kulikuwa na mavi ya ng'onge anakwenda huku moshi mkali ukifuka kwenye baiskeli yake siku ya leo yeye ndie mjumbe na barozi wa kila mtaa Msindo
Nyuki waliendelea kugawa dozi gawa dozi vibaya mnoo mubaba nae namuona huyo na dereva wake wakiwa na manundu usoni , kwa dharula hii kukawa tena hakuna taratibu za hawa wafiwa wala nini ikawa ni mchanganyiko tu lakini cha kushangaza watu walio kuwa wanakimbilia majumbani kwao nyuki walikimbiza na walipo geuka na kufuata njia ya msibani nyuki wale hawakuwasumbua tena hivyo kupelekea watu wengi sana kujazana msibani hapa nyumba
Muda nao ukawa unasogea ikawa majira kama ya saa tisa hivi hali ikaanza kukaa sawa
Mwenyekiti wa kijiji alijitokeza na kutaja watu ambao wapo mautiuti walio kimbizwa hospitali lakini cha ajabu majina ya Shangazi mkubwa na Bamkubwa yalitajwa hapo kila mtu alipigwa na butwaa he Bamkubwa wengine walishangaa kuona jina la Shangazi mkubwa nalo lipo
Tuanze kwa Bamkubwa bamkubwa ni mgonjwa wa kupooza mwili yani upande mmoja wa mwili wake ni mbovu kabisa yani hawezi kutembea wala kushika kitu kuoga anaogeshwa kula analishwa sasa imekuwaje ang'atwe na nyuki mbona sisi tulio kuwepo nyumbani hatuja umwa na nyuki kabisa basi ikawa hali ya mshangao kwa kila mtu miguno shonyo na mengine mengi yaliendelea
Mwenyekiti aliendea kutoa pole kwa familia na wanakijiji wote kwa janga kubwa kama hili la leo
"wananchi wenzangu hali hii ni ngeni hapa kijiji kwetu toka kuzaliwa kwangu hadi umri huu sijawahi shuhudia janga kama hili sijui labda kwa baba zetu na babu zutu , wazee wote wa msindo na vijiji jirani walikataa kwa pamoja hapana na sisi hatujawahi kuona kabisa janga kama hili Itaendelea........ .
Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.
Maoni
Click here to login and comments