Simulizi : Mke Wangu Nusu Jini, Nusu Mtu Sehemu Ya 2 IMEANDIKWA NA : ALLY MBETU #ILIPOISHIA Nilipata wakati mgumu sana kuwaza kuhusu sambusa, Munil aliniambia amezifuata yeye lakini kusema ule ukweli hakuzileta
"Baba," aliniita Munil baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu.
"Niambie mama."
"Utakwenda kuzika?"
"Kwani mwili unakwenda kuzikwa wapi?"
"Lushoto."
"Itabidi niende sijui? We unasemaje?"
"Twende wote."
"We utaenda?"
"Mimi tena, yaani ndugu halafu nikose?!"
"Basi na mimi nitaongozana na wewe."
"Sawasawa."
#SONGA NAYO...
Siku hiyo baada ya kuachana na Munil nilikwenda nyumbani. Niliwaambia majirani kwamba nitasafiri kwenda Lushoto, Tanga kwa mazishi. Lakini kwa sababu ya uchovu niliamua kutokwenda msibani kulala mpaka kesho yake ambapo ningesafiri, hata kaka nilimwambia hivyo.
Ilikuwa usiku wa saa nne nikiwa kitandani, nilimkumbuka Munil kwamba hatujawasiliana kwa muda mrefu, tangu tulipoachana kule baa, nikachukuwa simu ili nimtwangie lakini kabla simu haijaita, mlango mkubwa uligongwa, nikakata simu na kuuliza.
"Nani?"
"Munil."
Nilishtuka, nikaguna kwanza na kujiuliza mwenyewe:
"Amepajuaje hapa au hanitafuti mimi."
"Nakuja," nilisema kwa sauti nikitoka kitandani.
Nilifungua mlango, nikakutana na macho ya Munil. Safari hii alikuwa mzuri zaidi ya wakati wowote ule. Alizidi kuwa mweupe pee! Aliwaka mtoto kama Mwarabu vile. Akaachia tabasamu.
"Karibu Munil."
"Asante," alisema akiingia ndani.
"Umepajuaje hapa Munil?"
"Nimeulizia."
"Umeniuliziaje? Maana sijawahi kukwambia naitwa nani."
"Si unaitwa Abigael jamani au?"
"Ndiyo lakini lini nilikwambia hilo jina langu Munil?"
"Na wewe bwana, hebu tuyaache hayo."
Niliamua kuyaacha kweli kama alivyotaka Munil, nikamkaribisha chumbani huku nikimuuliza:
"Msibani umeaga unakwenda wapi?"
"Nimesema nakwenda kwangu."
"Kwani we hukai pale?"
"Hapana."
"Unakaa wapi?"
"Si hapo nyuma tu."
"Hapo nyuma tu? Kwenye nyumba ya nani?"
"Nyumba ya mzee Ngurumo."
"Mzee Ngurumo! Kwani pale pana wapangaji?"
"Si ndiyo mimi sasa."
"Mh! Nilijikuta nikiguna tena maana nyumba aliyoitaja kweli ipo. Mzee Ngurumo namjua vizuri sana lakini pale nyumbani kwake hapana mpangaji, ni familia tu na tena ana watoto wa kiume pekee!
"Mbona kama umeshangaa sana, vipi?"
"Sijashangaa sana ila nimeshangaa."
"Umeshangaa nini?"
"Si huyo mzee Ngurumo."
"Kwamba?"
"Kwamba ana wapangaji pale kwake. Nilikuwa sijui."
Munil aliniambia atalala kwangu usiku huo hadi alfajiri ya saa kumi na moja atarudi msibani. Hata asingesema hivyo yeye, mimi mwenyewe nilitaka kumwambia asiondoke ili tuandike historia ya kwanza katika uhusiano wetu.
Tuliongea mengi sana na Munil hadi kufikia kuwekana wazi kwamba nini anataka, nini hataki. Kitu kimoja kilinishangaza sana, Munil alisema katika mambo anayoyapenda maishani mwake ni mafuta mazuri, yaani pafyumu au manukato.
"Ni kwa nini?" nilimuuliza kwa kusisitiza mshangao.
"Basi tu, yaani nimejikuta nikipenda sana. Unajua baba, mama, wadogo zangu na hata ndugu wengine wote wanapenda sana mafuta mazuri.
Wakati Munil ananiambia hayo, alikuwa akinukia mafuta mazuri sana.
Sasa ulifika muda wa mimi na Munil kulala. Nilimwambia apande kitandani, akasema anapenda kulala mwanzo wa kitanda lakini kwa sababu amenipenda sana anakubaliana na mimi. Alitangulia kupanda kisha nikafuata mimi.
Ilikuwa mara yangu ya kwanza kulala na Munil na kukutana naye kimapenzi. Alinioamba tuzime taa, nilikataa lakini akasisitiza kwamba huwa anajisikia vizuri zaidi akiwa na mwanaume kwenye chumba chenye giza nene.
Ili kuzima taa ilibidi mimi nitoke kitandani kuifuata swichi, nikaweka mguu mmoja chini, kabla sijaweka wa pili, Munil akasema:
"Ngoja niende mimi."
Niliona ugumu yeye kwenda kwenye swichi maana kama ni kutoka ingebidi aniruke kwanza. Kilichotokea, nilimwona Munil akiamka kitandani lakini sikumbuki nini atap! Giza!
"Hee!" Nilishtuka, nikapapasa ubavuni kwangu ili kuona kama Munil yupo au, nikamwona amejaa tele!
"Umezimaje taa Munil?"
"Si nilikwenda."
"Siyo kweli Munil. Hujatoka kitandani."
"Ha! Sasa kama nisingetoka kitandani ningezimaje?" Munil aliniuliza akinishangaa.
Niliamua kukubaliana naye lakini kutoka moyoni nilikataa kwamba, Munil aliizima taa bila kutoka kitandani! Sasa nikawa najiuliza alifanyajefanyaje? Ina maana alipeleka mkono mpaka kwenye swichi? Haiwezekani. Nilikataa kimoyomoyo.
Basi, mimi na Munil tuliingia kwenye tukio la kihistoria ambapo kwa mara ya kwanza tulifanya mapenzi tena bila kondom na cha kushangaza sana ni kwamba, Munil nilipomwambia habari ya kondom alisema haina haja kwa sababu kama mimi nina Ukimwi siwezi kumwambukiza yeye na kwamba yeye ni mzima wa afya!
Nilishangaa sana kwa tamko lake hilo, nilianza kuhisi sipo na mwanamke wa kawaida lakini hilo pia nikalivumilia kwa namna nyingine tena.Tulipomaliza, bado kukiwa na giza, Munil alitaka kwenda chooni, akaniambia anaomba kwenda chooni, nikamwambia unapajua? Maana choo chenyewe kilikuwa ndani kabla hujatoka uani.
Aliniambia anapajua, nikashangaa. Nikamuuliza uliwahi kuingia kwenye nyumba hii, akasema ndiyo. Nikamwambia basi nenda nione. Niliamini amesema tu lakini hakijui choo kilipo.Alipotoka kitandani alivaa taulo langu lakini nilishikwa na mshtuko kusikia akitembea kwa kunyata tena kama mwanaume aliyevaa viatu vya mchuchumio, maana vilikuwa vikilia koo, koo, koo.
Alipofungua mlango nikatoka haraka sana kwenda kuwasha taa ili nione alikuja na viatu gani. Nilijua kama sitaona viatu basi nitajua alivaa viatu vya mchuchumio na ndivyo vilivyotia mlio wa koo.
Ile nawasha taa tu, nikasikia sauti ikiniuliza:
"Hivi mbona kama una wasiwasi na mimi, kuna nini kwani?"
Alikuwa Munil amelala kitandani akiniangalia kwa macho makali na yenye hasira.
"Ha! Kwani si ulisema unakwenda nje kujisaidia?" nilimuuliza nikitetemeka.
"Mimi sijatoka kitandani baby. Sasa kama ni kwenda chooni si ningekwambia unisindikize, mi napajua chooni kwenu? alisema Munil.
Nilizima taa ili nirudi kulala lakini wakati nazima kabla ya tendo hilo niliangalia chini na kubaini kwamba hakukuwa na viatu vyovyote. Nilitupia macho kiaina miguuni kwa Munil pale kitandani lakini sikuona kitu kwani miguu yote ilikuwa ndani ya shuka.
Nilirudi kulala, ile namalizia tu kujifunika shuka, mlango ukasukumwa, akaingia mtu. Nilijua ni mwizi sasa, nikauliza:
"Wewe ni nani unayeingia?"
"Jamani baby, kwani si nilikwambia nakwenda chooni, mbona unachanganyikiwa lakini?"
Kabla sijamjibu nilipeleka mkono pembeni yangu kuona kama Munil alikuwepo, lakini hapakuwa na mtu!
?Munil,? niliita huku nikitoka kitandani na kusimama katikati ya chumba nikiwa nahema kwa kasi, woga ulinishika, miguu ilitetemeka kama mtu aliyekutana na kiumbe wa ajabu kwenye njia iliyosonga akiwa peke yake.
?Abee,? aliitika Munil aliyeingia.
?Kwa nini unanifanyia mambo haya??
?Yapi dear?? Munil aliniuliza huku akifunga mlango na kuzima taa.
?Inakuwaje nikuone kitandani halafu pia wakati huohuo nikuone unaingia, halafu kitandani haupo??
nilisema kwa sauti ya juu. Nadhani hata nje walisikia kama kulikuwa na watu.
?Baby hilo ndilo tatizo lako. Yaani wewe umenifanya mimi ni jini siyo? Niwe kitandani halafu niwe nimetoka nje, inawezekanaje?? alihoji Munil akiwa amewasha taa sasa. Alisimama mlangoni akiniangalia kwa macho yaliyojaa mshangao.
?Baby, kwani una nini?? aliniuliza.
Nilimsimulia hali ilivyokuwa, akasema itakuwa nina mawazo mengi juu yake ndiyo maana namuwewesekea mpaka namwona mara mbilimbili.
Basi, nilijipa moyo, nikamshika mkono Munil na kumpandisha kitandani kisha na mimi nikapanda. Niliamua mara hii tulale na mwanga hivyo sikuzima taa.Sikuchukuwa muda mrefu sana nilipitiwa na
usingizi na kuota ndoto. Niliota niko kwenye jumba moja kubwa sana la kifahari. Ukuta wote ulipambwa kwa dhahabu, juu badala ya kuezekwa mabati, kulipigwa madini ya shaba. Ilikuwa sehemu ya peke yake.
Eti humo nilikwenda kuulizwa ukweni kama nitamuoa binti yao au la! Binti mwenyewe alikuwa amenipeleka kwa wazazi wake nikaulizwe vile alisimama katikati ya sebule kubwa akiniangalia kwa macho mazuri huku akiachia tabasamu laini. Alikuwa binti mzuri kwa namna yoyote ile, sura hadi
umbo lakini alionekana si mtu mweusi, kama Mwarabu au Mzungu aliyechanganya damu.
Wazazi wake waliniangalia kwa macho ya kunikubali huku baba mtu akiniambia kama nitakubali kumuoa binti yao atanipa sehemu ya mali yake ili kuendeshea maisha na binti yao lakini kama
sitakuwa tayari kwa ndoa, yule baba aliniambia angenichinja kwa sime akitumia mkono wake.
Wakati anasema kama siko tayari kumuoa binti yake atanichinja kwa sime, alitoa mfano, akaenda kwenye kona ya sebule, alitumbukiza mkono mahali na kutoa sime, akanifuata na kuniwekea shingoni, wakati anaanza kuchinja nikashtuka kutoka usingizini huku nahema sana na jasho jembamba likinishuka mwilini.
?Vipi baby?? aliniuliza Munil baada ya kuamka kwangu huku nikihema kwa kasi.
?Da! Nimeota ndoto mbaya sana,? nilisema.
?Ipi??Nilimsimulia ndoto hiyo Munil lakini kila nilipokuwa namuweka wazi yeye alikuwa akicheka tu mwishowe akasema:
?Baby.?
?Naam.?
?Kwani hujui kwamba ndoto huja baada ya shughuli nyingi mpenzi wangu??
?Ndoto huja baada ya shughuli nyingi wakati umeona mtu anataka kunichinja na sime?? nilimuuliza kwa kumshangaa sana.?Ni kweli, lakini ni ndoto tu. Kwani umewahi kuota ikawa kweli?? aliniuliza.
?Sijawahi.?
?Sasa kwa nini hii unaogopa sana??
?Nahisi kama kweli, si unaona jasho! Tena ngoja niamke niswali,? nilisema lakini kabla sijaamka Munil alinizuia akisema haina haja ya kuswali kwa vile ile ni ndoto tu.
* * *
Alfajiri, Munil aliniamsha akiwa ametoka kuoga, akasema anakwenda msibani. Nilitoka kitandani, akaniuliza kwa nini naamka, nikamwambia nataka kumpa pesa, akacheka sana.
?Sasa sisi wanawake tunataka usawa kila siku, si inatakiwa mimi nikupe pesa wewe badala ya wewe
kunipa mimi?? Wakati Munil akisema hivyo alitumbukiza mkono kwenye mkoba wake na kutoa noti mpya za shilingi elfu kumi, akanitupita kitandani kisha akasema baadaye.
Sikumbuki kama nilimwona Munil akiondoka japokuwa alifungua mlango. Ninachokumbuka ni
kwamba, akili yangu ilihamia kwenye zile pesa, kwamba ni shilingi ngapi.Niliinua shingo kuangalia nje kupitia dirisha ili nimwangalie Munil anavyotoka lakini sikumwona nikashangaa kwani asingeweza kutoka eneo hilo la nyumbani bila kuonekana kwa kupitia dirisha. Halafu, ghafla nilisikia kama sauti
ikiniambia??hivi kwa kumbukumbu zako, Munil alivaa viatu gani??
Nikajiuliza hivi kweli, Munil alivaa viatu gani? Sikupata jibu, nikachungulia chini sikuona. Ghafla kwa nje nikasikia ko ko ko! Munil anaondoka sasa. Nilichungulia tena dirishani, mlio wa viatu chini ulisikika lakini nikawa simwoni mtu na uelekeo ukitokea nyumbani ni mmoja tu, njia inakwenda imenyooka.
Nywele zilinisisimka, nikaa kitandani na kusema:
?Ee Mungu, kama huyu mwanamke ni jini nijulishe, kama si jini pia nijulishe.?
Nilipomaliza kusema, nikaulizwa na sauti akilini.?Hivi, hata Munil alipokuja pale baa kukusaliamia ulimwona amevaa viatu gani??Moyoni nilijijibu kwamba, sijamwona Munil akiwa amevaa viatu tangu nimemfahamu.
Kitu gani kilichoendelea….
Usikose sehemu inayofuata
Jamani twende chapu , bonyeza LIKE-150 sasa hivi ili nipost nyingine chapu chapu .
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni