VYOTE NDANI GONGA94
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............04 Ilipoishia sehemu iliyopita........ Farasi ilifika Lindiwe pamoja na prince Yao walipanda na safari ikaanza kutoka katika jengo
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
hilo la kifalme kwa njia ya siri,ilikuwa ni huzuni kubwa sana kwa malikia pamoja na mfalme kutengana na mtoto wao......................
ENDELEA ...............
ilikuwa ni huzuni kubwa sana kwa malikia pamoja na mfalme kutengana na mtoto wao,hawajua ni lini tena watamuona.
"Mtukufu mfalme naomba tuelekee katika jumba la kifalme".
Malikia andwaa aliongea baada ya kuhisi upye ndani yake sababu alimzoea sana mwanae
"Ni wakati mgumu sana unaopitia malikia wangu kwa kutengana na kijana wako".
"Mda mwingine kwenye maisha ni kawaida kupitia jambo usilolitarajia mfalme,ilikuwa ni lazima nitengane na Prince Yao mtukufu mfalme,
Utawaambia nini watu wako utakapofika mda wa kumtambulisha prince????"
"Mimi ni mfalme wa ADELI hakuna wa kupinga kauli yangu tutajua cha kufanya".
Mfalme pamoja na malikia andwaa walirejea katika jumba la kifalme baada ya kumkabizi prince Yao mikononi mwa mtumishi wao Lindiwe aliyefanyikiwa kuondoka na Prince Yao katika jumba la kifalme.
*********************
"Ni miaka mitatu sasa tunaanda jeshi la kuja kupindua huu ufalme general huoni kama ni mda sahihi huu wa sisi kuchukua huu utawala?????".
"Wazari mkuu, upo sawa kwa ulichokiongea idadi ya jeshi letu ni kubwa kuliko jeshi la mfalme,na nikiwa kama General nitaliondoa jeshi analolitegemea mfalme nilipeleke mipakani siku ambayo tutauvamia huu ufalme".
"Lakini wewe ni general kwanini usiwashawishi wanajeshi wote wakawa upande wako????".
"Huwa sipendi mtu mwenye mawazo ya kijinga,siku nyingine nitakukata kichwa sitajali kama wewe ni wazari mkuu na upo katika mipango yangu,
Wewe ni waziri mkuu tumia akili, mfalme anawapelelezi wa siri ivyo itakuwa ni vyepesi tarifa kumfikia na iyo itakuwa hatari kwetu,General aliongea"
Hapo ndipo waziri mkuu alipojua kuwa ameingia kwenye mipango na mtu hatari sana na anatakiwa awe makini mana general alionekana hana utani ata kidogo.
Licha ya general kumkalipia waziri mkuu bado waliendelea na mipango yao ya kupindua ufalme na hawakutaka kupoteza mda tena baada ya kuandaa jeshi lao kwa miaka mitatu,walipanga kuvamia usiku unaofata.
**********************
Ni siku nyingine tena Lindiwe akiwa na prince Yao anafanyikiwa kuvuka mpaka wa falme ya ADELI na anaingia kwenye mipaka ya falme nyingine.
"Mbona tangu jana tupo kwenye farasi kwani tunaenda wapi na wewe ni nani???",
Japo kuwa alikuwa haoni na ni mtoto mdogo prince Yao alijaliwa ufahamu wa hali ya juu
"Usijali mtoto mzuri nakupeleka sehemu nzuri ya wewe kutibiwa uweze kuona"
"Unasema kweli????,"
"Ndio mtoto mzuri"
"basi wewe ni mtu mzuri sana na endesha farasi haraka tuwahi kufika nataka nione sura ya mama inafananaje"
Kwa maneno aliyokuwa anaongea prince yao Lindiwe alijikuta anatoa machozi ni huzuni kwa mtoto kama yule kuwa na tatizo la kutokuona.
"Nisamehe sana Prince sikuwa na kingine cha kuongea zaidi ya kukudanganya natamani uweze kuona ila sina uwezo wa kukufanya uone,yalikuwa ni maneno aliyoongea ndani ya moyo wake mwenyewe".
Wakiwa bado wanaendelea na safari na kuzungumza,gafra walizungukwa na kundi kubwa la vijana wenye mikuki na mishale.
Lindiwe na mtoto Prince Yao walishuka kutoka kwenye farasi wakawa wameingia mikononi mwa vijana wale.
"Nyie ni kina nani??, na mnatokea wapi????,moja ya vijana wale aliuliza"
"Tunatokea katika ufalme wa ADELI na huyu ni mtoto wangu haoni nimekuja nchi za mbali kumtafutia dawa ya kumfanya aweze kuona"
Prince Yao alisikia sauti ya Lindiwe akimtambulisha kama mtoto wake ila hakutaka kutia neno lolote lile.
"wakamateni tuwapeleke kwa mfalme".
Lindiwe hakuweza kufanya chochote mbele ya vijana wale zaidi ya kutii amri ya kukamatwa na kupelekwa kwa mfalme wao.
*********************
Baada ya mihangaiko ya kutwa nzima mfalme kojo akiwa amepumzika na Malikia Andwaa katika kitanda usiku wa siku hiyo, walisikie kelele upande wa nje na kumfanya mfalme amke na kutoka nje kuangalia kunatatizo gani.
"Mfalme!!!mfalme!!!!!!mfalme!!!!! tumevamiwa,zilikuwa ni kelele ambazo zilimfanya Mfalme Kojo atambue kuwa tayali hali imechafuka alirudi katika chumba chake".
"Wewe nenda katika chumba cha siri ukatulie huko acha nikamalizane nae huyu mpuuzi alijua mimi ni mjinga kama yeye"
"inamaana ulikuwa unajua mfalme kama kuna huu mpango wa kuja kuvamiwa usiku wa leo???"
Malikia alimuuliza mfalme baada kuona kama hajashitushwa na kuvamiwa kwao.
"Ndio nilikuwa najua kila kitu ila sio mda sahihi huu wa kuongea wewe nenda"
Mfalme alitoka na kuelekea sehemu ya mapambano na kumuacha malikia akiwa na maswali mengi kichwani.
Shambuliaaaaaaaaa!!!! General alitoa amri kwa wanajeshi wake ambao tayali walikuwa wameingia katika jumba la kifalme kupitia geti kuu.
"Nasema shambulia",
Alitoa amri nyingine tena kwa wanajeshi wake cha ajabu walitulia tu wakimwangalia general wao huyo.
"Ivi mumepatwa na nini nyinyi??,"
Hamsikii amri yangu General Tengeli aliongea baada ya kuona wanajeshi wake hawafanyi chochote kile licha ya kuingia kwa bwebwe zote katika jumba la kifalme.
"Kwa mara ya mwisho nasema shambulieniiiii........."
"Hawawezi kutii amri yako hao ata siku moja general",
ilisikika sauti na kumfanya General kugeuka nyuma kuangalia ni nani huyo aliyeongea kwa kujiamini mbele yake tena mbele ya wanajeshi wake na ukizingatia wanajeshi amewafundisha mwenyewe.............ITAENDELEA.
Ni kwanini wanajeshi wa General hawataki kutii amri ya kiongonzi wao??? na vip kuhusu hatima ya Lindiwe na Prince Yao tukutane sehemu ya 05 inamajibu zaidi
ENDELEA ...............
ilikuwa ni huzuni kubwa sana kwa malikia pamoja na mfalme kutengana na mtoto wao,hawajua ni lini tena watamuona.
"Mtukufu mfalme naomba tuelekee katika jumba la kifalme".
Malikia andwaa aliongea baada ya kuhisi upye ndani yake sababu alimzoea sana mwanae
"Ni wakati mgumu sana unaopitia malikia wangu kwa kutengana na kijana wako".
"Mda mwingine kwenye maisha ni kawaida kupitia jambo usilolitarajia mfalme,ilikuwa ni lazima nitengane na Prince Yao mtukufu mfalme,
Utawaambia nini watu wako utakapofika mda wa kumtambulisha prince????"
"Mimi ni mfalme wa ADELI hakuna wa kupinga kauli yangu tutajua cha kufanya".
Mfalme pamoja na malikia andwaa walirejea katika jumba la kifalme baada ya kumkabizi prince Yao mikononi mwa mtumishi wao Lindiwe aliyefanyikiwa kuondoka na Prince Yao katika jumba la kifalme.
*********************
"Ni miaka mitatu sasa tunaanda jeshi la kuja kupindua huu ufalme general huoni kama ni mda sahihi huu wa sisi kuchukua huu utawala?????".
"Wazari mkuu, upo sawa kwa ulichokiongea idadi ya jeshi letu ni kubwa kuliko jeshi la mfalme,na nikiwa kama General nitaliondoa jeshi analolitegemea mfalme nilipeleke mipakani siku ambayo tutauvamia huu ufalme".
"Lakini wewe ni general kwanini usiwashawishi wanajeshi wote wakawa upande wako????".
"Huwa sipendi mtu mwenye mawazo ya kijinga,siku nyingine nitakukata kichwa sitajali kama wewe ni wazari mkuu na upo katika mipango yangu,
Wewe ni waziri mkuu tumia akili, mfalme anawapelelezi wa siri ivyo itakuwa ni vyepesi tarifa kumfikia na iyo itakuwa hatari kwetu,General aliongea"
Hapo ndipo waziri mkuu alipojua kuwa ameingia kwenye mipango na mtu hatari sana na anatakiwa awe makini mana general alionekana hana utani ata kidogo.
Licha ya general kumkalipia waziri mkuu bado waliendelea na mipango yao ya kupindua ufalme na hawakutaka kupoteza mda tena baada ya kuandaa jeshi lao kwa miaka mitatu,walipanga kuvamia usiku unaofata.
**********************
Ni siku nyingine tena Lindiwe akiwa na prince Yao anafanyikiwa kuvuka mpaka wa falme ya ADELI na anaingia kwenye mipaka ya falme nyingine.
"Mbona tangu jana tupo kwenye farasi kwani tunaenda wapi na wewe ni nani???",
Japo kuwa alikuwa haoni na ni mtoto mdogo prince Yao alijaliwa ufahamu wa hali ya juu
"Usijali mtoto mzuri nakupeleka sehemu nzuri ya wewe kutibiwa uweze kuona"
"Unasema kweli????,"
"Ndio mtoto mzuri"
"basi wewe ni mtu mzuri sana na endesha farasi haraka tuwahi kufika nataka nione sura ya mama inafananaje"
Kwa maneno aliyokuwa anaongea prince yao Lindiwe alijikuta anatoa machozi ni huzuni kwa mtoto kama yule kuwa na tatizo la kutokuona.
"Nisamehe sana Prince sikuwa na kingine cha kuongea zaidi ya kukudanganya natamani uweze kuona ila sina uwezo wa kukufanya uone,yalikuwa ni maneno aliyoongea ndani ya moyo wake mwenyewe".
Wakiwa bado wanaendelea na safari na kuzungumza,gafra walizungukwa na kundi kubwa la vijana wenye mikuki na mishale.
Lindiwe na mtoto Prince Yao walishuka kutoka kwenye farasi wakawa wameingia mikononi mwa vijana wale.
"Nyie ni kina nani??, na mnatokea wapi????,moja ya vijana wale aliuliza"
"Tunatokea katika ufalme wa ADELI na huyu ni mtoto wangu haoni nimekuja nchi za mbali kumtafutia dawa ya kumfanya aweze kuona"
Prince Yao alisikia sauti ya Lindiwe akimtambulisha kama mtoto wake ila hakutaka kutia neno lolote lile.
"wakamateni tuwapeleke kwa mfalme".
Lindiwe hakuweza kufanya chochote mbele ya vijana wale zaidi ya kutii amri ya kukamatwa na kupelekwa kwa mfalme wao.
*********************
Baada ya mihangaiko ya kutwa nzima mfalme kojo akiwa amepumzika na Malikia Andwaa katika kitanda usiku wa siku hiyo, walisikie kelele upande wa nje na kumfanya mfalme amke na kutoka nje kuangalia kunatatizo gani.
"Mfalme!!!mfalme!!!!!!mfalme!!!!! tumevamiwa,zilikuwa ni kelele ambazo zilimfanya Mfalme Kojo atambue kuwa tayali hali imechafuka alirudi katika chumba chake".
"Wewe nenda katika chumba cha siri ukatulie huko acha nikamalizane nae huyu mpuuzi alijua mimi ni mjinga kama yeye"
"inamaana ulikuwa unajua mfalme kama kuna huu mpango wa kuja kuvamiwa usiku wa leo???"
Malikia alimuuliza mfalme baada kuona kama hajashitushwa na kuvamiwa kwao.
"Ndio nilikuwa najua kila kitu ila sio mda sahihi huu wa kuongea wewe nenda"
Mfalme alitoka na kuelekea sehemu ya mapambano na kumuacha malikia akiwa na maswali mengi kichwani.
Shambuliaaaaaaaaa!!!! General alitoa amri kwa wanajeshi wake ambao tayali walikuwa wameingia katika jumba la kifalme kupitia geti kuu.
"Nasema shambulia",
Alitoa amri nyingine tena kwa wanajeshi wake cha ajabu walitulia tu wakimwangalia general wao huyo.
"Ivi mumepatwa na nini nyinyi??,"
Hamsikii amri yangu General Tengeli aliongea baada ya kuona wanajeshi wake hawafanyi chochote kile licha ya kuingia kwa bwebwe zote katika jumba la kifalme.
"Kwa mara ya mwisho nasema shambulieniiiii........."
"Hawawezi kutii amri yako hao ata siku moja general",
ilisikika sauti na kumfanya General kugeuka nyuma kuangalia ni nani huyo aliyeongea kwa kujiamini mbele yake tena mbele ya wanajeshi wake na ukizingatia wanajeshi amewafundisha mwenyewe.............ITAENDELEA.
Ni kwanini wanajeshi wa General hawataki kutii amri ya kiongonzi wao??? na vip kuhusu hatima ya Lindiwe na Prince Yao tukutane sehemu ya 05 inamajibu zaidi
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi story-mfalme-kipofu-sehemi-ya
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............08 Ilipoishia sehemu iliyopita........ "Tarifa gani???" "Inasemekana baada ya siku tatu Prince
Story MFALME KIPOFU Sehemi..ya............02 Ilipoishia sehemu iliyopita... "Mbona unazunguka mtabili emu niambie mwanangu niliyemzaa leo anatatizo gani???