Simulizi za Maisha,Mafunzo,Mapenzi ,Chombezo Habari za Michezo na Burudani vyote kwa Kiswahili ndani ya – Gonga94 Semajambo
Gonga94 · Stories
29 Nov 2025
138 views
VYOTE NDANI GONGA94
NAWACHUKIA MASHANGAZI, SHANGAZI YANGU ALISHIRIKI KUNIUMIZA KIHISIA NA KWA KUNIVUA UTU NA THAMANI YANGU
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Nilikuwa nakaa kwa SHANGAZI YANGU baada ya mama angu kufariki na baba angu kuondoka kwenda machimboni. Shangazi yangu hakuwa na mume ila alikuwa na watoto wa kiume wawili ambao walikuwa wanaishi kwa baba yao.
Kuna siku akaja na mwanume fulani nyumbani akaanza kumwambia huyu binti nimempenda nipe basi nimuoe. Shangazi akasema ongea naye akaja kuongea naye nikakataa. Shangazi akaniambia mkubali tu ana hela atakupa na atakusomesha mimi nimechoka kukusomesha. Jiongeze
Siku mmoja akaja na soda akanipa nikanywa kumbe ilikuwa na madawa nikalewa nikawa nasikia maumivu kwa mbali kushutuka niko kitandani na yule baba niliyemkataa na damu akinifanya damu zikanitoka. Bikra yangu ilitolewa na mwanaume ambaye alimlipa shangazi yangu pesa na akaniambia nikisema kwa mtu yeyote ile damu aliyoichukua atanifanyia kitu kibaya nife. Nilitamani kufa au kuondoka ila nikawa naogopa. Siku mmoja nikamkuta wanaongea na simu akimwambia nimalize pesa yangu sasa wewe nimekufanikishia mpango wako wa kumtoa bikra mbona humalizii pesa yangu lasivyo nitakushitaki umembaka. Nikasikia leo tena unataka ulale naye lasivyo uje na hela ya ziada halafu soda hatakubali tena kumpa kwasababu alishajua hilo. Nikasikia akisema nitaweka kwenye maji ya kunywa jagini basi nilivyosikia hivyo nikajua tu nikaa nje kwa muda kisha nikaingia ndani nikamkuta pale akanituma kwa rafiki yake ni mbali kidogo anajua mpaka nikarudi atakuwa ameenda mazingira yake sikurudi
Nikaenda kwao rafiki yangu nikamuita mama ake nikamwambia kwasababu yule mama alikuwa anafanyakazi hospital na alikuwa ananisaidia siku zingine hata nguo akimnunulia mwanaye nami ananinulia nikamwambia ukweli akasikitika sana na akanipeleka hospital nikapimwa magonjwa nikakutwa sina. Usiku ule akampigia baba angu akamwambia nimekuwa malaya hata silali nyumbani kisa sikurudi nyumbani basi kesho yake yule mama akasema hawezi kukaa na mtoto wa mtu bila wazazi wake kujua nikampa no ya baba akaongea naye kumbe shangazi alikuwa tayari kanitangaza umalaya kwa baba
Yule mama akamwelezea ukweli wote baba akaja nikamwambia kisa chote kile baba akasema nitakula nao sahani moja ila yule mama na mume wake wakamsihi asifanye kitu kibaya dada ake ila mimi nina kisasi kwa SHANGAZI nimeshindwa kabisa kusamehe na kusahau ule unyama wake nimekuwa nikisali sana nimesikia ana kansa ya shingo ya kizazi blind haikati anatoka damu mwanzo mwisho naamini ni Mungu kampa adhabu. Natamani sana nikae sawa nimemaliza masomo yangu ya kidato cha nne natamani niende mbali sana ambako hakuna mtu asiyenifahamu nikaishi huko ninapoishi sasa wananipenda sana ila sina amani kwasababu wanajua unyama niliotendewa najiona mtu kwao natamani niende mazingira mageni kabisa
Nimefikia hatua nawachukua mashangazi au nikisikia mtu anamuita mtu shangazi au anaowazungumzia watu hao kabisa natamani nisahau hilo tukio ila nashindwa kuna wakati namlaumu baba kunipeleka kwa shangazi bora angelipeka kwa bibi😭
Maoni
You're not logged in
X
Login
X
signup
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa
+ Endelea kugundua zaidi
mwanzilishi mwenza wa YouTube Karim mwenye umri wa miaka 25 wakati huo katika Zoo ya San Diego akizungumza kuhusu
Ukurasa wa kutazama wa YouTube unaangazia upakiaji wa kwanza kabisa unaoitwa "Me at the zoo," ikionyesha mwanzilishi mwe...
NAWACHUKIA MASHANGAZI, SHANGAZI YANGU ALISHIRIKI KUNIUMIZA KIHISIA NA KWA KUNIVUA UTU NA THAMANI YANGU
Nilikuwa nakaa kwa SHANGAZI YANGU baada ya mama angu kufariki na baba angu kuondoka kwenda machimboni. Shangazi yangu hakuwa na mume ila alikuwa na watoto wa kiume wawili ambao walikuwa wanaishi kwa baba yao.
Kuna siku akaja na mwanume fulani nyumbani akaanza kumwambia huyu binti nimempenda nipe basi nimuoe. Shangazi akasema ongea naye akaja kuongea naye nikakataa. Shangazi akaniambia mkubali tu ana hela atakupa na atakusomesha mimi nimechoka kukusomesha. Jiongeze
Siku mmoja akaja na soda akanipa nikanywa kumbe ilikuwa na madawa nikalewa nikawa nasikia maumivu kwa mbali kushutuka niko kitandani na yule baba niliyemkataa na damu akinifanya damu zikanitoka. Bikra...
👉 Soma zaidi hapa: https://www.gonga94.com/semajambo/nawachukia-mashangazi-shangazi-yangu-alishiriki-kuniumiza-kihisia-na-kwa-kunivua-utu-na-thamani-yang
Maoni