๐ILA BOSS ANAJUA KUPELEKA MOTO๐ 6 na 7
O6
Umekuja tena ? nilimuuliza . Ndio kwani ni vibaya kuja kukujulia hali wakati wewe ni jirani yangu sasa kwanini jana ulikataa kuwa sio wewe wakati nakufahamu vizuri hadi nimeenda kumuuliza mama yangu kuwa upo wapi siku hizi kaniambia ulishaondoka. Ndio nimeshaondoka pale naishi kibaha kwa sasa, nilimjibu huku nikiangalia pembeni.
Nataka kuongea na wewe ila nikiangalia mazingira naona hayafai tunaweza kutoka hapa kidogo, Siwezi na hii biashara naiacha vipi hapa. Nitanunua mimi hizo zote ili tu unipe muda wako .
Sawa nilimjibu nilikusanya vitu nikamfuata yeye tuliingia kwenye gari ๐ tukaondoka sikujua hata tunaenda wapi yaani kama ingekuwa natekwa sijui ingekuwaje ๐ tulifika mahali alipaki gari๐ tulishuka ilikuwa ni hoteli ๐จ alikuja muhudumu sijui ndio waiter kwa kizungu mnaita . Nelly agiza unachotaka moyoni nikajisemea chizi kapewa rungu na hivi nina njaa ngoja nile tu nikutie hasara niliagiza wali samaki na maji mwenzangu na mie mzungu akaagiza maji tu nikasema potelea mbali itakuwa kala alipotoka.
Kwanini umeondoka nyumbani ๐กkwa wazazi wako unakuja kuhangaika huku juani wakati mna uwezo tu , niliacha kula ghafla nilivyokumbuka mambo waliyonifanyia machozi ๐ญ yakaanza kunitoka. No Nelly kulia ๐ญ sio solution niambie sababu nini , Denis alitoa leso ๐คง akanipa nijifute. Walinisingizia nimeiba hela wakati sijawahi hata kuiba hiyo ndio sababu ya kuondoka pale .
Kwani ni wazazi wako kabisa wale ? ni baba tu mama yangu alishafariki kitambo tangu nipo kidato cha kwanza ,
Dah pole sasa unaishi wapi na nani? Naishi na mama yangu mkubwa . Pole sana kwa mitihani iliyokukuta nilivyokuona tu nilikumbuka nilikuona nyumbani ๐ก kwa mama yangu.
Kama una uwezo wa kunitafutia kazi sehemu yoyote naomba unitafutie tafadhali nitakushukuru sana kaka yangu maana sitaweza kukaa siku zote namtegemea mamkubwa kila siku , kuna siku atanichoka tu. Usijali nipe siku mbili nitakupa jibu nitakutafutia kazi una elimu gani๐ค, Denis aliniuliza hadi nikaona aibu kuongea nimeishia form four tu matokeo yamekuja sio mazuri . mwandishi naah story teller0785540715
Ok sio mbaya hamna kinachoshindikana naona muda umeenda nikurudishe nyumbani ๐ก .
Usipate shida ya kunirudisha nitarudi mwenyewe kaka yangu , Twende usiku ๐ sasa ngoja tu nikupeleke . Sawa ilibidi tu nikubali tulisimama tukaingia kwenye gari ๐ tukaondoka safari ya kuelekea kibaha ikaanza muda wote nilikuwa kimya ๐ค tulivyokaribia kufika akaniuliza nina mzigo wa kiasi nilikataa lakini alinilazimisha hadi nikamwambia elfu hamsini na tano .
O7
Alichukua wallet yake akatoa elfu sitini akanikabidhi nilifika karibu na nyumba yetu nikamuomba anishushe tuliagana nikaenda nyumbani . Nilimkuta mamkubwa anapika , umewahi kurudi kweli umetoka mbezi saa ngapi au biashara ngumu mwanangu.
Yaani we acha tu mama yaliyonikuta leo nimeuza zote ila kimchongo tu , Sijakuelewa una maanisha nini ๐ค. Nimekutana na mkaka mmoja tulikuwa majirani kanitoa out kanunua na korosho zote cha ajabu hajachukua hata moja pia kaniambia atanitafutia kazi ya kufanya. Au mkwe nini ๐ค mamkubwa aliuliza huku anacheka , anhaa wapi atakuwa na familia ๐ช yake lazima nilimjibu mamkubwa .
Ndio akusaidie bila sababu yoyote ngoja tuone mimi mtu mzima naelewa hata ukinidanaganya . Kama ni mna mahusiano au anakutaka huyo mamkubwa nawe kwa kukuza vitu haya ila mimi sio mtu wangu kabisa huyo na sina mpango nae mimi, Usimalize maneno binti haya kaweke ndani uje tule mimi nishamaliza kupika hapa, mimi nishashiba mamkubwa nimekula huko wali na samaki mkubwa tu hapa labda nishushie pepsi ya baridi , Muagize John akakununulie basi nilimuagiza mtoto wake akaenda kuninunulia soda aliniletea nikanywa nikaenda zangu kulala ๐ ili kesho asubuhi ๐ na mapema niwahi kuamka si unajua tena ukikaa kwa mtu tena watu husema ukibebwa jishikilie ๐.
Kesho asubuhi ๐ niliamka mapema nikaenda kwenye biashara nilimwambia mamkubwa apumzike na leo asiwe na haraka, mida ya jioni Denis alikuja hadi nilipo akanunua korosho za buku akaniambia anataka kuongea na mimi moyoni nikajisemea huyu kila siku anataka kuongea na mimi hadi nachoka ila ngoja nikubali tu kwa kuwa niliomba anitafutie kazi labda atakuwa kapata wanasemaga usikatae wito kataa maneno.
Basi nilimsikiliza nikasimama nikamfuata pembeni akaniambia naomba namba yako ya simu๐ฑ, Mimi sina simu kaka nilimjibu. Acha kunidanganya ukubwa wote huo hata simu huna sasa tutawasiliana vipi mimi na wewe ok mambo yasiwe mengi nakuja sasa hivi nenda kaendelee na biashara yako. Nilirudi kwenye meza yangu nikawa naendelea kuuza baada ya nusu saa Denis alikuja na boksi la simu akanipatia alikuwa ashasajili na line, kama hukuwa na simu hata line huna nimekusajilia kabisa .
itaendelea......
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni