IN LOVE WITH ZURI* Chapter 8
SONGA NAYO......
Ethan akazungumza
"Hakuna cha kukata tamaa, kwani we nani amekwambia kuwa ameolewa..??"
"Ni mama.."
Nilimjibu huku nikiwa nimekata tamaa zaidi
"Sasa mama wewe unamuamini vipi??, kama amekuongopea?? We cha kufanya anza kumtoa mtoto out huku kila ukienda misele umletee zawadi mbona atamsahau huyo mumewe.."
"We Ethan wewe, ushauri gani unampa mwenzio..??"
Idress alimuuliza Ethan, Jamani msichokijua huyu Ethan huyu ni moto wa kuotea mbali muoneni hivi tu huyu kijana ameanza mapenzi kakiwa bado kadogo yani kana miaka kumi tayari kashabikiriwa
Na sijui hata kalijifunzia wapi haka kajamaa, sasa kitendo cha kunipa ushauri wake kidogo nikawa nimeupokea na kuuweka akilini
"Sasa unataka nimwambie nini??, harafu we nae Frank unamuamini mama hovyo hovyo sana hata kujiuliza tu hapa anatafuta nini kama ni mama watoto na ana mume si saivi angekuwa kwa mumewe huko.."
"Ethan mama ameniambia kwamba, alimtoa huko ukweni kwake kwa sababu walikuwa wanamtesa sana.."
"Ohoooo sasa hapo ndio napapenda mimi, chakufanya zingatia niliyokwambia ndani ya week moja mtoto ataanza kukuelewa na kumsahahu huyo mumewe tena ambavyo alikuwa anateseka mbona fasta tu...."
"Kweli..??"
Niliuliza huku nikiwa siamini amini
"Yap fanya hivyo sasa..."
Frank mimi nikapata nguvu mpya nikanyanyuka na kujinyoosha kwanza na muda huo nikamuona Zuri akiwa anakuja seblen na kapu la nguo chafu.
"Unashangaa nini nenda kamsaidie..."
Ethan aliniambia, eeeh me nawezaje eti jamani , mtu nimetoka kumgombeza saivi tu harafu niende nikamsaidie si ataniona mimi namshobokea.
Nilichofanya hapo ni kutulia tu na wala hata sikujishughurisha na kwenda kumsaidia hizo nguo, nilimuacha tu akanipita kama hanioni vile walah nilikuwa naumia
"Yani we Frank unaniboa kabisa, sasa badala ya kwenda kumsaidia pale unamuangalia tu.."
Ethan alianza kulalamika
"Ethan we hujui tu, yani nimetoka kumgombeza saivi harafu niende nikamsaidie si ataniona kama mjinga.."
"Aaagh unazingua bana.."
"Acha nizingue ila kwa hili hapana kwa kweli.."
Nilisema kisha nikashika njia na kwenda chumbani kwangu, nikimuacha Ethan analalamika hatari, huyu kijana anapenda sana kunilalamikia na huku mie ni kaka yake.
Baada ya mimi kuondoka pale sebleni, Ethan alitoka nje na kwenda sehemu ambapo alikuwa Zuri na kufika akaa pembeni yake
"Nakuona binti.."
Ethan alizungumza
"Ethan siko sawa, naomba uondoke hapa.."
"Ah usiwe hivyo Zuri, unajua wewe ni binti mzuri lakini pia uko na adabu sana so usiruhusu kabisa hasira zikae ndani yako.."
"Ethan ondoka.."
"Lakin.."
"Ondoka nakwambia.."
Ethan kinyonge alinyanyuka na kuondoka huku akiwa anatazama nyuma kama Zuri atamuangalia au kumuita.....
Itaendelea
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni