*AFANDE NILEGEZEE KAMBA ππ«π«* 17 -- 18 Chapter 17 Mapenzi yangu na Elton yalikuwa mazuri kupita maelezo. Nilifurahia kila dakika niliyoitumia naye. Kila kukicha tulikuwa tunazidi kuwa karibu zaidi
Elton alianza kunifundisha mambo mengi hasa. mapishi. Akanifundisha kupika wali, pilau, ndizi pamoja na mchuzi wa nyama & kuku. Aliniambia anataka niwe nampikia siku akichoka baada ya kurudi kazini.
Apo tayari mwezi ukaisha na ule mkataba wetu uliishia pale. Elton alilipa deni langu lote na Nilikuwa huru kusafiri nje ya Arusha. Ila sikuona kama kuna haja ya kuondoka ikiwa furaha yangu. ilikua ni Elton. Hata ule mpango wa kurudi nyumbani niliuhairisha.
Sasa siku moja ilikuwa Jumapili, Hatukuenda popote. Tuliamka mapema, tukapika chakula cha mchana pamoja, tukala kisha tukakaa sebuleni kuangalia movie.
Nililaza kichwa changu kwenye mapaja ya Elton yani full burudanil Ilikua ni kawaida yetu kujiachia kiasi kile. Mara ghafla mlango ulifunguliwa na mtu ambaye hakubisha hodi.
Nilipogeuka nikamuona mwanamke mmoja mwenye umri sawa wa mama yangu. Elton alipomuona, alishtuka Akasema taratibu, "Mom"
Ndo nikajua oooh kumbe huyu ndiye mama yake Elton. Nilifurahia kumuona mama mkwe wangu mtarajiwa ila sasa Mama mkwe mwenyewe alini nyali. Hakufurai kutuona pamoja akauliza, "Na huyu mwanamke ni nani?"
Elton akatabasamu "Mama, huyu ni Gina mpenzi wangu"
"Mpenzi wako?! Kwa ruhusa ya nani? Nani amekuruhusu uwe na mwanamke wa namna hii?" Mama ni anafoka huyoo
Elton akasema "Hakuna aliyenipa ruhusa lakini Mom, mimi nampenda Gina"
"Noooo! Siwezi kukubali huu uhusiano. Chochote kinachoendelea baina yenu kiishe. mara mojaaa!....na wewe binti! Kesho nisikuone kwenye hii nyumba! Uondokeee kama sijakuondoa mimi
Elton akasimama "Mom, huwezi tu kuja nyumbani kwangu ghafla na kuniambia nivunje uhusiano wangu"
"Kama mimi ni mama yako, utasikiliza. ninachosema. Kama sivyo, basi endelea na huu upuuzi wako. Kufikia kesho asubui nataka huyu
msichana awe ametoka hapa. Na unajua nilivyo Elton Baada ya kusema hivyo, mama yake akachukua begi lake na kuelekea chumba cha wageni.
Nilibaki nimesimama pale, nikitokwa machozi. Elton akanigeukia na kuanza kunibembeleza "Please usiweke maneno ya mama moyoni. Nitazungumza naye"
"Lakini Elton, ni mama yako. Lazima umsikilize. Sitaki kuwa chanzo cha nyie kugombana"
"Gina nakupenda Manaa. Sitaki mwingine zaidi yako. Nataka uwe mama wa watoto wangu. Nitazungumza na Mom vizuri, ataelewa! Please niamini okay??"
Nikatikisa kichwa "Sidhani kama ataelewa Elton. Alinionyesha chuki tu kwa macho. Ila maybe ukiongea atakuelewa kama ulivyosema basi ngoja tuone Nilijikuta nikitoka sebuleni nikielekea chumbani uso umelowa machozi.
Elton hakuweza kuvumilia machozi yangu, alimfuata mama yake kwenye chumba cha wageni. Nikaanza kusikia wanabishana na kwa. jinsi Elton ana hasira za karibu nikaona niende nikaamue ugomvi kabla hajafanya jambo baya. Nilisogea hadi mlangoni ila nikasita kuingia baada ya kusikia kile walicho kiongea
Mama Elton alisema "Umesahau kwamba tulishapanga ndoa yako? Tushachagua msichana mzuri, mwenye heshima, kutoka familia nzuri. Sasa ni upuuzi gani huu unafanya??"
"Sijali kuhusu iyo ndoa. Huyo msichana
mwenyewe hujawai kumuona, sijawai kumuona na yeye pia hajawai kunional Unaongea tu na wazazi wake kwenye simu, una hakika gani kama ana heshima na adabu! Come on Mom. Nampenda Ginah ama huoni??"
"Yawezekana kweli sijawal kumuona huyo binti ila Baba yako na Baba wa huyo binti walikulia kijiji kimoja walipokua wadogo. Yani sio urafiki tena bali ni undugu walionao. Na toka zamani
waliapa na kuahidiana kuwa lazima watoto wao waje kuoana. Kwa bahati mbaya walipokuja mjini wakapotezana, ila walipokutana tena. wakapanga kuendeleza ndoto zao. Kwaiyo Elton
hili swala haliepukiki! Lazima utamuoa uyo binti utake usitake. Alafu Huyu msichana ulie nae. hana hadhi ya kuwa mkwe wa familia yetu!"
Elton akapiga kelele, "Mom please! Nampenda Gina, siwezi kumuacha"
Mama yake akamwangalia kwa ukali "unanifokea sio?? Kwa taarifa yako ndoa lazima Itafungwa na Kesho asubuhi nataka huyu Gina. asiwepo hapa. Usinifanye nifanye kitu kibaya. Unajua vizuri nikiwehuka nakuaje"
Niliposikia maneno hayo, moyo wangu ulivunjika vipande vipande. Nilirudi haraka chumbani, nikaanza kulia kwa uchungu zaidi. Elton alikuja. baadaye usiku akajaribu kunifariji.
"Please usiogope. Nitazungumza na mama tena, usije ukafikiria kuondoka"
"Sawa" niliitika Lakini ndani ya moyo wangu nilijua kuwa nilipaswa kuondoka. Sikupenda kuona mama na mwana wanagombana kwa ajili yangu.
Asubuhi ilipofika, niliandaa kahawa ya Elton kama kawaida! Alikunywa kahawa kisha alinibusu na Akaniambia nikae tu ndani, atarudi mchana then akaenda kazini.
Sikujali alichosema, Nilianza kukusanya virago vyangu haraka haraka maana Nilijua njia pekee ya kumaliza ule ugomvi wa mama na mtoto ni mimi kuondoka.
Mama Elton alikuwa bado amelala kwa hiyo nilivyo ondoka yeye hakujua kabisa. Nilikodi boda ikanipeleka mpaka stendi nikiwa sijui niende wapi. Nikawaza nirudi nyumbani??? Ama niende kwa nani??
Nikiwa kwenye mawazo mara kuna gari jeusi lilisimama mbele yangu. Mwanzo nilidhani ni
Elton kanifuma ila baada ya kioo kushushwa nikahisi kujikojilea. Alikuwa ni Baba yangu, Nikajiuliza "amejuaje niko hapa?"
Unajua nini kilitokea baada ya hapo? Subiri kidogo... nakuja.
Sehemu ya kumi na nane
Nilikuwa na hofu sana nusu nikimbie "Ginah, Ingia kwenye gari sasa hivi" Baba alifoka nikaona hapa hakuna haja hata ya kukimbia.
Dereva alishuka na kuchukua mizigo yangu akaipakia kwenye gari, akanifungulia mlango ambapo nilikaa siti ya nyuma pamoja na baba.
"Unajua nimekuwa nikikutafuta kwa muda gani? Ulidhani sitakupata sivyo?"
Nikasema "Sorry Dad, Samahani sana".
"Wewe kweli niwa kutia aibu familia yangu. Umenirudisha nyuma kwa namna ambayo sikuwa nadhani unaweza kufanya. Ulidhani kukimbia nyumbani ndio suluhisho? Shida ilikuwa ni wewe kubadilika. Kama ungebadilika, kila kitu kingekwenda vizuri lakini hukutaka kubadilika. Uliamua kuongeza mafuta kwenye moto. lia sasa hivi sijali, tunarudi nyumbani na unaolewa mara moja. Hakuna kusubiri"
Nilikaa kimya Nikilia kwa sababu nilikwenda kuolewa na mtu ambaye sikua namjua. Pia nililia kwa sababu niliondoka bila hata kumuaga Elton
Wakati tulikuwa safarini kuelekea Dar es Salaam, simu yangu ilianza kuita, Ilikuwa ni Elton anapiga. Baba alichukua simu yangu na kuizima,
akasema
"Huyu ndo mwanaume anaekupa kiburi sio??"
"Hapana, baba"
"Tutaona mwisho wake! Sikio kamwe haliwezi kuzidi kichwa
Sikujibu Nikaamua kimya maana nilikua nina mawazo sana na nguvu ya kubishana na Baba sikua nayo.
Haya bhana Tukafika Dar es Salaam saa tano usiku. Baada ya mwezi mzima na wiki mbili za kukimbia, hatimaye nilirudi tena nyumbani. Mama alikuwa akitusubiri nje.
Aliponiona, akaangalia kwa huzuni! Kikubwa Alifurahi kuona niko sawa lakini hakuweza
kuficha hasira yake kwangu. "Ah, sawa basi kama uko salama, Sasa tuanze maandalizi ya harusi Akaingia ndani huku baba akimfuata nyuma.
Mimi Nikaenda chumbani kwangu, nikaoga kisha nikalala. Kwa jinsi nilivyo mmiss Elton wangu sikupata usingizi kabisa. Nilitaka angalau kusikia sauti yake ila ndo ivyo, Mzee alininyang'anya simu.
Kesho yake Asubuhi wazazi wangu hawakutaka nile nao breakfast mezani sababu bado walikua wamenikasirikia ivyo walituma dada wa kazi aniletee chai yangu chumbani.
Hata sikula sana, nilidonoa donoa kidogo Kisha
nikarudisha tray jikoni. Nilivyoviacha niliviweka kwenye friji kisha vyombo vichafu nikaviosha. Hili ilishangaza kila mtu mnajua?? Mpaka mama alishangaal Apo mwanzo Sikuwai kuosha hata kijiko changu, nilikua nawaachia wafanyakazi.
Lakini leo eti naosha vyombo, nasafisha kabisa. na sinki! Hill ni maajabu
Mchana napo nikaingia jikoni kumsaidia dada mpishi kupika. Wakati huo baba alikua kazini ni Mama na mimi pamoja na wafanyakazi ndo tuliokua nyumbani..
Basi Mama akawa ananiangalia bila kunimaliza. Mwishoni akashindwa kuvumilia akaniita, tena akawa anaongea kwa upole kushinda jana alivyo nipokea
"Nini kimekubadilisha? Umekuwa tofauti sana, Gina"
"Ni Maisha tu mama"
"Umebadilika kuwa mtu bora, Hilo ndilo. tunalotaka kutoka kwako Ginah! I am happy for you!"
"Sawa mama"
"Kuolewa pia ni suluhisho pekee tuliloliona. Alafu kingine, Baba yako na huyu rafiki yake wametoka mbali sana na hii ni ahadi
waliyowekeana kitambo sana kwaiyo ni ngumu mno kuvunja ahadi! Kwalyo sitaki usituchukie mimi na baba yako"
"Siwachukill Na mimi nipo tayari kwa lolote"
"Nafurai kusikia ilo" mama alitabasamu kisha akaenda sebuleni
Jioni pia niliendelea kusaidia jikoni. Tukapanga
meza pamoja, na Baba aliporudi aliona nikipanga na kuandaa chakula, akashangaa lakini haikubadilisha mpango wake wa mimi kuolewa.
Hali ilikua ivyo ivyo kwa wiki nzima, niliamka mapema, nikafanya usafi, nikawa nafua na kupasi nguo zangu mwenyewe! Mchana nilienda kupika pamoja na Dada Mpishi mpaka tukaanza kuzoeana.
Mbali ya yote hayo nilimkumbuka Elton! Nilimuomba Mungu huko alipo ampe nguvu sababu najua alikua akipitia kipindi kigumu mno. Najua pengine nilimkosea kuondoka bila taarifa lakini sikua tayari kuona anagombana na familia yake kisa mimi, especially mama yake mzazi.
Basi ijumaa jioni Baada ya chakula cha usiku, Baba akaniambia nijitayarishe kwa sababu kesho yake tulipaswa kwenda kukutana na familia ya mume wangu mtarajiwa. Kutakua na utambulisho mfupi kisha siku hiyo hiyo. nitavalishwa pete ya uchumba.
Niliitikiwa tu "sawa" Nikaenda kulala.
Kesho yake pilika pilika zikaanza. Mama alininunulia gauni zuri la kuvaa kisha wakaja watu wa make-up wakanipodoa pale nikatoka chicha kama sio tembele
Ilipotimu saa tisa kila mtu alikua kashajiandaa hadi Shangazi angu wa Dodoma alifika kumsapoti Mama.
Tulitoka tukiwa kwenye msafara wa magari matatu. Moja liliwabeba, mama, baba na shangazi! Gari la pili lilinibeba mimi peke yangu!
Gari la tatu lilibeba majirani zetu wachache ambao Mama hakutaka kuwaacha nyuma.
Unajua nini kilitokea baada ya hapo? Subiri kidogo... nakuja.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi